I KILLED MY LOVER 55

 


SCENE 55: -

BAADA YA MIAKA MINNE: -

NYUMBANI KWA RAPHAEL: -

 (Raphael amewakusanya watu mbalimbali ikiwemo mama yake, kaka zake na baadhi ya marafiki zake nyumbani kwake wanaonekana kusherekea jambo Fulani)

Raphael: (amembeba mtoto Bianca ambae amekuwa na umri wake ni miaka minne) kwanza kabisa namshukuru Mungu kwa kunifikisha siku hii (anambusu mtoto Bianca)

Lydia: (anatabasamu)

Rafiki 1: leo kuna nini Rapha? Ni birthday yako?

Gabriel: (anatabasamu)

Raphael: (Anacheka) hapana leo sio birthday yangu

Rafiki 1: ila kuna nini?

(Honi ya gari inasikika kutoka nje)

Raphael: wamefika (anamuweka Bianca chini)

Bianca: (anamkimbilia Michael)

Raphael: (anaenda kufungua mlango)

(Liliana pamoja na binamu zake wanaingia)

Lydia: (anafurahi kumuona Liliana) wow…karibu mama Bianca

Liliana: (anatabasamu) asante sana

Anna: (kwa Raphael) ndo nini kutuacha peke yetu tumemchukua ameachiwa jamani Mungu ni mkubwa sana

Bella: sana

Raphael: samahanini sana sikuwa na nyie ila ilibidi nije nyumbani niandae mazingira ya kusherekea huu muujiza

Bianca: (anamkimbilia mama yake)

Liliana: jamani ka mama kangu (anamkumbatia na kumbusu)

Gabriel: (kwa Liliana) karibu shemeji

Liliana: asante shemeji

Michael: karibu Liliana

Liliana: asante sana shemeji

Raphael: karibu nyumbani my love (anambusu)

Bella: awwwh jamani

Anna: mapenzi mazuri sana

Bella: sana

Liliana: (anacheka) mmeanza majungu

Bella: (anacheka)

Raphael: (anacheka pia) karibu my love…karibu nyumbani nimefurahi sana

Lydia: sio peke yako sasa (anacheka) wote hapa tumefurahi

Michael: kabisa

Raphael: (anatabasamu) haya kwa yule aliyeniuliza leo kuna nini? Jibu hili hapa kwamba mpenzi wangu ameachiwa huru baada ya kutumikia kifungo kwa miaka minne

Rafiki 1: wow

Rafiki 2: huyu si alikuwa mpenzi wa baba yako? Raphael unachangia mwanamke na baba yako?

(Wote waliopo hapo wanaishiwa uchangamfu)

Raphael: (anakaa kimya)

Rafiki 2: mbona mna mambo ya ajabu hivyo hamuoni aibu yaani (kwa Liliana) hivi huoni aibu kuliwa na baba na mtoto?

Liliana: (anaangalia chini kwa aibu)

Rafiki 2: (kwa Lydia) unaruhusu vipi mwanao kuja kuishi na hawara wa mume wako? Au ulikuwa umefurahi? Na pia kumbuka ya kwamba huyu ni muuaji wa mume wako

Lydia: kijana umeongea sana nashukuru kwa mchango wa maneno yako sana ila mwisho wa siku haya ni maisha yetu na maamuzi haya tumeyafanya tukiwa na akili timamu

Raphael: (anashusha pumzi)

Lydia: lililotokea lilitokea na hatukuwa na uwezo wa kubadilisha chochote hapo ni sawa alikuwa ni hawara wa baba yake Raphael kwani yeye sio mtu mpaka asipate nafasi ya kupendwa na kupenda pia?

Raphael: mama achana nae tulijua tu yataongelewa haya lakini pamoja na kuongelewa sitaachana na mpenzi wangu eti kwasababu watu wanataka hivyo…moyo hauchagui pa kuangukia sikupanga kama nikionana na Liliana nitamtongoza na awe wangu ilitokea tu

Rafiki 2: uwe na aibu

Raphael: (anapaza sauti) uwe na aibu wewe unayeingilia mambo yasiyokuhusu

Rafiki 2: nakusikitikia sana unadhani jamii inakuchukuliaje?

Raphael: I don’t care watu wanawaza nini au wanafikiria nini nampenda Liliana na nitamuoa yeye

Lydia: (kwa rafiki 2) naona hapa hapakufai kaka unaweza ukajiondokea mwaya hapa ni kwa watenda dhambi

Rafiki 2: naondoka ndio (anaondoka)

Anna: duh kwani huyu mtu ni wa wapi? Mbona ana gubu

Raphael: achana nae (kwa Liliana) baby

Liliana: lakini anachosema ni sawa yuko sahihi

Michael: shemeji usimsikilize

Liliana: (anacheka) hapana shemeji (kwa Raphael) mi naona tuishie hapa

Raphael: no Liliana huwezi kunifanyia hivi mpenzi wangu nimekusubiri miaka minne vipi kuhusu mipango yetu ya kumlea mtoto wetu pamoja yaani maneno ya mtu asie na akili yakubadilishe mawazo?

Liliana: (anakaa kimya)

Gabriel: shemeji relax waelewe wasielewe ni nyie na maisha yenu jamani tutakuwa tunafanya mambo yetu kwa kujali watu sawa ulikuwa na mahusiano na baba sasa hiyo isiwe fimbo ya kukupigia wewe milele relax shemeji yangu

Liliana: (anafuta machozi)

Raphael: (anamshika bega) baby karibu nyumbani

Lydia: yaliyopita si ndwele tugange yajayo

Anna: kabisa

Liliana: asanteni sana kwa ushirikiano kweli kabisa Mungu awabariki sana

Michael: ubarikiwe pia shemeji

Liliana: jamani lets celebrate

Raphael: yes, baby

Lydia: tule, tunywe, tusahau ya nyuma yote yaliyotuumiza yale yote yaliyotuwekea uadui na tuwaombee wapendwa wetu waliotutangulia wapumzike kwa amani

Wote: amina

Liliana: (ananyanyua glasi yenye shampeni) kwa mambo mazuri yote yanayokuja mbele yetu cheers

Wote: cheers (wanagonga glasi)

Liliana: (anaonekana ni mtu mwenye furaha sana)

Raphael: (anamkumbatia mpenzi wake)

Anna: aaawwhh love is such beautiful thing

Bella: sanaaaaa

Liliana: (anacheka) embu huko

(Wanaendelea kufurahia na kusherekea kwa kunywa, kula kucheza muziki na michezo mbalimbali, hali ni shwari kabisa)

Post a Comment

0 Comments