I KILLED MY LOVER 56

 


SCENE 56: -

NYUMBANI KWA RAPHAEL: -

(Asubuhi na mapema, Liliana anafika kwa mpenzi wake akiwa ni mtu mwenye wasiwasi sana)

Liliana: baby

Raphael: (anaonekana amezidiwa na ugonjwa Fulani)

Liliana: (anakaa pembeni yake) baby ni nini? Au hunywi dawa tena? Usichoke haya ni maisha yetu

Raphael: (anacheka) no baby nilitaka uwahi kuja my love najua ningekuita kawaida ungekawia kuja au usingekuja kabisa

Liliana: baby I don’t understand

Rapahel: baby it has been four years my love

Liliana: (anaonekana kutoelewa kitu)

Raphael: (anacheka) baby...it has been four years my love

Liliana: yeah baby

Raphael: na ndani ya muda wote huo umekuwa mtu mzuri sana yaani best girlfriend

Liliana: (anatabasamu) hata wewe umekuwa best boyfriend and best daddy to my child

Raphael: our child my love

Liliana: yes, our child

(Wanacheka)

Raphael: asante kwa kuwa mwenza mzuri mwenye upendo wa dhati na muelewa

Liliana: wewe ndo asante kwa kuwa mvumilivu umenivumilia nilipokuwa gerezani mpaka nikatoka bado tu umenionyesha upendo

Raphael: No baby wewe ndo umenionyesha upendo pamoja na kwamba jamii halikulichukulia suala la mimi na wewe kuwa wapenzi but still ulichagua kuwa na mimi…asante sana Liliana nakupenda sana

Liliana: nami nakupenda Zaidi Raphael wangu

(Wanatabasamu)

Raphael: hivyo basi kwa kusema haya yote (ananyanyuka anatoa mkebe mfukoni kisha anapiga goti) Liliana

Liliana: (anatabasamu) yes baby (anaweka mikono mdomo ishara ya kushangaa)

Raphael: will you be my wife?

Liliana: seriously baby? (anatabasamu)

Raphael: yes, baby will you marry me?

Liliana: oh my God baby yes (anamkubatia)

Raphael: (anamvalisha Pete ile yenye urembo mzuri na yenye thamani sana) she said yes

(Ndugu zao wanakuja kutokea vyumbani)

Anna: wacha weeee raha sio raha

Wote: (wanaitikia) Rahaaaaa

Raphael: (anatabasamu)

Liliana: (anashangaa) mlikuwepo?

Anna: tunakosaje kwa mfano?

Liliana: (anacheka)

Bella: ofcourse lazima tuwepo

Raphael: (Anafurahi sana) asante sana Liliana kwa kukubali kuwa mke wangu

Liliana: (anatabasamu)

Raphael: (kwa watu) haya muanze kujiandaa na harusi sitataka ichelewe

Michael: dogo relax unapania sana

Raphael: sio kweli bwana

Lydia: imekuwa so soon

Gabriel: mama umeanza waache bwana najua wewe bado hukubali kwasababu Liliana aliwahi kuwa mpenzi wa baba mzazi wa Raphael but mama this is love na ikija imekuja na tunatakiwa kukubaliana nalo

Lydia: unaongea sana Gabriel kwani mimi nimekuambia sitaki waoane?

(Wanacheka)

Gabriel: sasa ulimaanisha nini uliposema kuwa imekuwa ghafla sana?

Lydia: I mean hajamuacha mwanadada akae hata mwezi adange kidogo

(Wote wanaangua kicheko)

Lydia: anataka kumfunga mapema (anacheka kwa nguvu)

(Wote wanaangua kicheko)

Raphael: jamani mama

Lydia: njoo mziwanda wangu hongera baba kwa kuchumbia (anamkumbatia)

Raphael: Asante mama yangu (anamkumbatia kisha anambusu kwenye paji la uso)

Michael: na kisha tusherekee

(Watu wanasherekea kwa kucheza muziki na kadhalika)

Gabriel: hakuna bia?

Lydia: na wewe utaacha lini pombe wewe mtoto (kwa Anna) naomba umuokoe mwanangu

Anna: (anacheka kwa aibu)

Liliana: mambo hayo

Gabriel: (anacheka kwa aibu pia)

Lydia: unadhani sijawaona? Au unadhani sijui kinachoendelea kati yenu?

Gabriel: ni Michael na Bella mama

Lydia: hata nyie

Raphael: (anashangaa) mazito

Lydia: na ndo maana mling’ang’ania kubaki huku mnadhani sijui?

Liliana: what?

Raphael: ndugu wanaoa ndugu

Lydia: mnaendeleza ukoo…pambaneni

(Wanacheka)

Lydia: ndo vizuri lakini hatujatupana

(Wanacheka)

Michael: DJ weka mambo (anaangalia huku na huku) alaaah!! Kumbe hakuna cha Dj wala baba yake DJ ngoja niwe mimi

Lydia: utakuwa umetusaidia sana mwanangu

Michael: (anaenda kuchukua vinywaji kwenye friji kisha anawasha muziki)

Anna: watu weeeweeeee

(Wanaanza kucheza na kufurahia maisha yao)

Lydia: (anashusha pumzi) haya ndo maisha anayotakiwa kuishi Liliana ameteseka toka akiwa mdogo na Zaidi baba wa watoto wangu alimsababishia maumivu makubwa sana ila pamoja na yote Mungu atabaki kuwa Mungu

Raphael: yes, mama

Liliana: (anafurahi sana)

Raphael: happy baby?

Liliana: very happy

Raphael: (Anambusu mdomoni)

(Sherehe inaendelea huku kila mmoja wao anaonekana kuwa na furaha isiyo na kifani na mwenye furaha zaidi sio mwingine bali ni Liliana)

Post a Comment

0 Comments