I KILLED MY LOVER 8

 


SCENE 8: -

(Asubuhi ya kesho yake Anna anafika shuleni anaonekana akiwa na mawazo mengi sana kichwani kwake)

Anna: Liliana anahangaika sana na haya maisha najiuliza kosa lake nini? je kosa lake labda ni kufiwa na wazazi wake akiwa katika umri mdogo? namuonea huruma sana…halafu baba si ni ndugu yake wa damu bora mama unaweza kusema kwakuwa hawachangii damu ndo maana anamtesa namna ile…

Bella: dada Anna unaonekana una mawazo sana kulikoni?

Anna: hamna mbona nipo kawaida sana?

Bella: haya kama uko kawaida…

Shangazi:(mama yao) hata mimi nakuona hauko sawa kama kuna kitu kinakusumbua niambie mwanangu tuna pesa na magari ya kutosha kila kitu sasa ni chetu sio maisha tuliyokuwa tunaishi mwanangu…niambie chochote nitakununulia

Anna:ni kweli tuna magari nyumba nzuri na pia tuna pesa maisha yetu ni mazuri sana tu ila vyote hivi sio vyetu mama ni vya yule tunayemuacha nyumbani anafanya kazi na kwenda kwenye shule za kawaida

shangazi: funga bakuli lako kabla sijakupiga vibaya sana…we mbwa wewe

Anna: Mungu hapendi tunachomfanyia mtoto wa watu mama

shangazi: nenda darasani mbwa wewe

Anna:(anaondoka na kuelekea darasani)

Shangazi:(kwa Bella) na wewe unataka kuniambia nini mimi?

Bella: aku!!! Mi naona uko sawa tu mama

Shangazi:(anatabasamu) wewe mwanangu ndo mjanja…(anacheka)haya mama waweza kwenda tu darasani baadae nitakuja kuwachukua…

Bella: sawa mama… (anakimbia darasani)

Shangazi :(anapanda gari na kuondoka)

(Upande wa Anna anafika ofisini kwa mwalimu wake wa darasa)

Anna:(anagonga mlango)

Mwl Monica: Karibu Anna…

Anna: asante mwalimu… (anaingia kisha anakaa katika kiti kilicho karibu na meza ya mwalimu huyo) shikamoo mwalimu

Monica: marahaba mama hujambo?

Anna:(kinyonge) sijambo…

Monica: vipi? mbona unaonekana huna raha?

Anna: kuna shida mwalimu sina mtu wa kumwambia Zaidi yako mwalimu…

Monica: nini tatizo mwanangu…mbona unanitisha?

Anna:(anasikitika kidogo) hivi huwa hakuna taasisi ambazo zinaweza kusaidia mtoto anayenyanyaswa…kihisia, kimwili na kadhalika?

Monica: zipo…ila kwanini unaniuliza? je unateswa?

Anna: hapana sio mimi mwalimu…

Monica:ni nani?

Anna: binamu yangu…ni mtoto wa shangazi yangu…wazazi wake walikufa katika ajali ya gari na walipokufa wazazi wangu wakajitolea kumlea maana sisi ndugu zetu wengi wanaishi nchi za nje…kwahiyo wakaona nyumba ya marehemu shangazi yangu isikae bila watu ndo tukawa tumehamia hapo, cha kushangaza binamu yangu anateseka sana…ananyimwa chakula, analala stoo

Monica:(anasikitika sana) maskini

Anna: anafanya kazi zote za hapo nyumbani…anasoma shule ambayo ni ya serikali na hapo anaenda shule mara baada ya kufanya kazi nyingi sana ufaulu wake uko chini sana kutokana na kwamba anaenda shule akiwa amechoka analala akifika shule yaani anasikitisha sana jamani

Monica: aisee…unaonekana unaumia sana

Anna:na kilichoniumiza sana na Zaidi nan do nikaona nitafute mtu anisaidie…ni kwamba baba yangu anambaka binamu yangu mara kwa mara

Monica:(kwa mshangao) eti!!!!???

Anna: ndio mwalimu…binamu yangu anabakwa na mjomba wake kila usiku…

Monica: hii imekuwa too much…ngoja... (anachukua simu yake na kubonyeza namba Fulani) ngoja inaita…ngoja nimwambie huyu wa haki za watoto na wazee…atatusaidia ni rafiki yangu sana

Anna: sawa mwalimu utakuwa umenisaidia sana

Monica: hello Eliza…mambo vipi?

Eliza: poa wewe za siku?

Monica: nzuri…upo ofisini?

Eliza: ndio nipo ofisini…my dear

Monica: nataka kuripoti unyanyasaji wa mtoto

Eliza: yes nambie…

Monica:(anaanza kumsimulia kama alivyosimuliwa na Anna)

Eliza: Duh...hii nayo kali yaani nyumba ni marehemu wazazi wake yeye anakaa kama hausigeli humo? eeh yaani jamani kwani wafu huwa hawaoni waje wamuokoe mtoto wao?

Monica: yaani acha tu na kali kuliko yote sasa, mtoto anatumika yaani anabakwa na mjomba wake

Eliza: aisee hiyo sasa tutachukua hatua mara moja…lazima tuende kwenye nyumba hiyo na kujionea hayo wenyewe

Monica: sawa haina shida rafiki yangu na nilijua utanisaidia tu na ndo maana nikaona nikupigie wewe

Eliza: usijali mtoto huyo hataona tena mateso…sisi tupo kwa ajili yake

Monica: shukrani (anakata simu na kumgeukia Anna) usijali mwanangu binamu yako hatakuwa na tabu tena yaani umemuokoa sana…

Anna: sawa mwalimu nami nafurahi kusikia hivyo maana si kwa kuteseka kule jamani yaani

Monica: usijali hayo yameisha…

Anna: sawa mwalimu ngoja mi niende darasani ila wakienda nyumbani wasiwaambie mimi ndo nimekuambia

Monica: usijali na wala hawatajua tutaenda kiakili sana

Anna: sawa mwalimu…mi naenda(anaondoka)

Monica: maskini huyo mtoto anaonekana anateseka sana, yaani mali za wazazi wako lakini unakaa kama sio zako na hao wazazi jamani hawajui hata kuvunga hata kidogo yaani wanamtesa waziwazi…eeh Mwenyezi Mungu nipe maisha marefu niwatunze wanangu hata wakuekue kidogo wajitegemee na sio jinsi huyu mtoto alivyoachwa

(Upande alipo Anna)

Anna: natumaini mwalimu atamsaidia binamu yangu maana si kwa kuteseka huko…

Bella :( anamjia) dada…ulikuwa wapi mbona nimekutafuta Sana?

Anna: nilikuwepo mbona?

Bella: sijakuona kabisa

Anna: nipo (anaelekea darasani kwake)

Bella :( anamsimamisha) dada…uko sawa?

Anna: nitakuwaje sawa huku binamu yangu anateseka kwenye nyumba yake?

Bella: kwani wewe dada yote hayo yanakuhusu nini? Si umuache?

Anna: mimi na wewe tunatofautiaana sana…mimi inaniumiza sana hii hali…. ile nyumba ni yake, magari yote ni yake…leo hii yeye ndo kawa mtumishi anasoma shule ya ajabu ajabu amabyo haieleweki?

Bella:(anaonyesha kupuuzia maneno ya dada yake) aah… (anaondoka na kuelekea darasani kwake maana wanasoma madarasa tofauti tofauti yeye yupo la tano na dada yake yupo la saba)

Anna:Mungu atusamehe sana mimi na familia yangu hasahasa baba yangu kwa kitendo cha kumbaka mfululizo malaika wa Mungu…(anaonyesha huzuni sana)Mungu naomba kitu kimoja Mungu wangu…umsaidie binamu yangu apate haki yake…tuishi nae ndio ila akae kama mwenye nyumba na sio mtumishi wa nyumbani inaniumiza sana jamani na kila kukicha lazima apigwe na kutukanwa matusi mengi kama mbwa…hana Amani je atakuwa mtu wa namna gani kama kila siku lazima apigwe vidonda kila mahali…namuonea huruma sana Mungu kama  unaishi naomba uonekane kwa binamu yangu ili aishi maisha aliyoyazoea…nampenda sana binamu yangu na ninajua wakati wa bwana umekaribia na ataenda kutenda sawasawa na mapenzi yake

Mwl wa zamu: we Anna mbona hauingii darasani?

Anna: samahani mwalimu (anakimbilia darasani)

Post a Comment

0 Comments