MUNGU MKUU 2

 


SCENE 2: -

(Asubuhi njema tena ya kupendeza tena Zaidi imefanywa na bwana, baba muumba mbingu na nchi, Ken na mkewe wanaenda kituo cha polisi wakiwa wamembeba mtoto mchanga kabisa na anaonekana amezaliwa siku si nyingi, wanapofika mahala pale kwakuwa wanajulikana na watu wengi wanasalimiana na watu wengi sana katika kituo hicho, mara baada ya salamu wanaenda moja kwa moja mpaka kwa mkuu wa kituo hicho)

Mkuu wa kituo:(anasimama kusalimiana na Ken pamoja na mkewe) ah...mkurugenzi…habari yako bwana

Ken: nzuri kabisa za kazi mkuu?

Mkuu: nzuri za huko kwenu?

Ken: tunamshukuru Mungu

Mkuu:(kwa mke wa Ken) shemeji? habari yako?

Keddy: salama shemeji

Mkuu: tafadhali ketini

(Wanaketi)

Mkuu:(nae anaketi maana muda wote huo alikuwa amesimama) ndio niwasaidie nini ndugu zangu? naona mmebebelea mtoto…wa nani?

Ken: sisi hatujui huyu mtoto tulimkuta jana nje ya nyumba yetu tukamuweka ndani na tukaambiana tuje tutoe taarifa polisi

Mkuu: mmefanya vyema sana…kwahiyo hamjui ni wa nani?

Ken: ndio...hata hatujui ni wa nani?

Mkuu: sawa kwanini msimuache hapa tutatangaza kwa yeyote aliyepoteza kichanga basi atamkuta hapa

Keddy: hapana mkuu…nadhani mama yake alitaka kumuacha kwetu….

Mkuu: okay…kwanini mmekuja kutoa taarifa

Keddy: unajua wanadamu tuna mambo mengi anaweza kurudi tena na kusema labda kaibiwa mtoto na kuleta kizungumkuti ndo maana tunataka kuepukana na hilo

Ken: tuko tayari kukaa na huyu mtoto mpaka mama yake atakapojitokeza

Mkuu: sawa…nyie kaeni nae tu mama yake akitokea maana ni lazima atakuja basi akija basi nitawaambia

Keddy: sawa hiyo imekaa vizuri

Mkuu: mtoto gani?

Ken: wa kike

Keddy: anaitwa Miriam

Mkuu: mpaka jina mmeshampa? (anacheka kidogo)

Keddy: ndio… (anacheka pia)

Mkuu:(anacheka) sasa Ariana amepata mtu wa kubaki nae nyumbani pindi anapokuwa hayupo shuleni

Ken:si yeye tu hata sisi tumepata mtoto

Keddy: njia za Mungu hazichunguziki….

Ken: kwakweli

Mkuu:(anashusha pumzi) sawa…nyie nendeni kukiwa na chochote nitawashtua au sio

Ken: sawa mkuu…

Mkuu: mtunzeni vyema Miriam

Keddy: atatunzwa kama Ariana hatokosa chochote katika haya maisha

Mkuu: vizuri sana

(Ken na mkewe wananyanyuka kujiandaa kuondoka)

Mkuu:(huku ananyanyuka) sawa malezi mema

Ken:na wewe kazi njema

(Wanapeana mikono kisha Ken na mkewe wanaondoka zao na kwenda)

Ken: tumepata mtoto mke wangu shetani muongo sana walipokutoa kizazi…alitudanganya na kutuaminisha kuwa hatutapata tena mtoto ila leo tuna mtoto tena mrembo (anatabasamu)

Keddy: haswa (anapanda kwenye gari kisha anampokea mume wake mtoto)

Ken:(nae anapanda kwenye gari)

Keddy: ila umegundua kuwa Ariana hajafurahishwa na ujio wa Miriam

Ken: shetani Muongo mke wangu anajaribu kukushawishi kuwa mwanao mkubwa hajampenda mwanao mdogo, ili ukate tamaa nae…wewe mpe muda Ariana ataelewa tu mke wangu acha kabisa kuwaza mambo yatakayokukosesha Amani

Keddy: sawa mume wangu nami nakubaliana na wewe honey

Ken: nina mpenda sana bwana Mungu wangu maana hajawahi kuniacha na hatawahi kufanya hivyo…

Keddy: hakika mume wangu

Ken: amina (anaondoa gari)

(Kuna mwanamke mbele ya gari na sio mwingine mama mzazi wa Miriam)

Ken:(anashtuka) Yesu wangu

Keddy: nini baba Ariana…?

Ken: unajua ningemgonga vibaya huyu dada… (anashuka kwenye gari) dada vipi mbona unataka kujiua?

Dada: sina mahali pa kwenda sina wazazi sina chochote naomba mnisaidie…

Keddy:(anashuka) unataka msaada gani?

Dada: hata niwe msichana wa kazi za ndani…

Ken: (kwa mkewe) mke wangu sikukwambia kuwa Mungu anaweza? si tulikuwa tunatafuta msichana wa kazi leo amejileta mwenyewe

Keddy: kabisa… (anatabasamu)

Ken: unaitwa nani?

Dada: Mary…

Ken: mama wa Yesu...wow

Keddy: nakwambia…(anacheka)

Ken: sawa panda kwenye gari twende nyumbani

(Wote wanapanda kwenye gari, wanaanza kuondoka)

Mary: naomba nimbebe mtoto…

Keddy:(anampa)

Mary:(anamchukua kisha anajisemea moyoni) mwanangu mzuri…hatimaye tena nimekushika nitakulea chini ya uangalizi wa hawa watu mpaka utakuwa mwanangu…

(Gari linaendelea kwenda na baada ya dakika kadhaa hatimaye wanafika katika jumba la kifahari la Ken na mkewe)

Ken: tumefika nyumbani…karibu

Mary: asante sana

Keddy: shuka…

(Wanashuka kisha wanaingia ndani)

Keddy: karibu nyumbani…

Ariana:(anaandika homework)

Keddy: Ariana…msalimie ma mdogo…kuanzia leo atakuwa anawalea wewe na Miriam

Ariana:(haonyeshi uchangamfu) shikamoo… (huku anaangalia pembeni)

Ken:(anaingia chumbani kwake)

Keddy:(anamuonyesha Mary, chumba chake cha kulala) humu ndo utakuwa unalala

Mary: sawa…

Keddy: hujaja na nguo?

Mary: ndio

Keddy: usijali nitakupa zangu ambazo sizivai tena?

Mary: asante dada

Keddy:(anabaki anatabasamu)

Post a Comment

0 Comments