SCENE 12: -
(Jeremy amekaa nyumbani kwake
akiwa peke yake na anaonekana ana mawazo mengi sana, ameshika simu yake kama
mtu anayesubiri kupokea ujumbe Fulani, wakati amekaa amezuba na anaonekana ana
mawazo mengi, mama yake anaingia)
Mama
:( anamshika bega) baba…
Jeremy
:( anashtuka)
Mama:
mbona sikuelewi?
Jeremy:
shikamoo mama
Mama:
marahaba
Jeremy:
hunielewi kivipi mama?
Mama:
watumishi wako wanasema siku hizi huendi ofisini na watumishi wa nyumbani kwako
nao wanasema una mawazo mengi sana baba…vipi kila kitu kipo sawa?
Jeremy
:( kimya)
Mama:
au unafirisika mwanangu?
Jeremy:
bora ningekuwa nafirisika ningeomba hata mkopo niokoe biashara yangu
Mama:
kwahiyo nini tatizo baba?
Jeremy:
iam in love mama
Mama:
hilo wote tunajua…je mchumba wako anakusumbua?
Jeremy:
sio yeye…
Mama:ni
nani?
Jeremy:
mdogo wake
Mama:(anashtuka) wewe Jeremy
Jeremy:
yes, mama nampenda Miriam kupita kiasi, siwezi kuwa na mwanamke mwingine
Mama:
huruhusiwi kuwa na huyo mtoto
Jeremy:
kwanini mama?
Mama:
sababu wewe ni mchumba wa dada yake
Jeremy:(anaongea kinyonge) lakini simpendi
Ariana mama
Mama:
hapana mwanangu wewe muoe tu Ariana
Jeremy:
mama, No…sitaki halafu mbaya Zaidi (anataka
kulia) Miriam kabadilisha simu…. namba yake haipatikani
Mama:
what’s wrong my son…yaani unataka kulia kisa mtoto kama Miriam?
Jeremy:
mama please help me mama yangu nakuomba…mimi ni mtoto wako nisaidie mama yangu
Mama:
hapana najua wewe ni mwanangu...ila siwezi kukusaidia labda kama ingekuwa
hujamchumbia Ariana hapo ningekusaidia
Jeremy:
mama nitajiua I swear!!! Sikutanii
Mama:
umekuwaje Jeremy embu tulia…lala kidogo tuliza akili yako halafu (anamnusa) mbona kama vile umekunywa
pombe…. yaani umelewa wewe mtoto jamani loh, umeanza lini kunywa pombe Jeremy?
Jeremy:
nimeanza leo mama nataka nipunguze na kusahau maumivu yote niliyo nayo
mama…nisipompata Miriam najiua…I swear
Mama:
wewe mtoto utaniletea matatizo ngoja nimpigie baba yako sasa hivi
Jeremy:
niambie mama utanisaidia au hunisaidii (anachukua
bastola anajiwekea kichwani) nitajiua sasa hivi
Mama:
Mungu wangu (simu inaita inapokelewa)
baba Jeremy naomba uje haraka Sana nyumbani kwa mtoto wetu
Baba:
kuna nini…nakuja mke wangu
Mama
:( anakata simu) tulia mwanangu…
Jeremy:
utanisaidia au nife?
Mama:
baba jamani embu acha masihala
Jeremy:
unaona natania?
Mama:
jamani baba
(Wakati wanaendelea kujibizana
baba Jeremy anafika)
Baba:
kuna nini? (Anamuona mwanae kajiwekea
bastola) wewe mtoto tatizo nini?
Mama:
huyu mtoto anataka kutuletea matatizo
Baba:
yapi?
Mama:
anamtaka mdogo wake Ariana
Baba:
kivipi, kwanini?
Jeremy:
nahesabu mpaka kumi…nikiwa sina jibu najilipua haki ya Mungu tena
Baba:
jamani
Jeremy:
moja…
Mama:
baba Jeremy tufanyeje?
Baba:(anatumia ukali) embu acha ujinga
Jeremy…shusha hiyo bastola mara moja
Jeremy:
mbili
Baba:
nimekuambia shusha hiyo bastola
Jeremy:
tatu…
Baba:
mimi si baba yako na unaniheshimu?
Jeremy:
nne…
Mama:
Jeremy…Jeremy baba, yule ni mtoto mdogo miaka 18 tu jamani, hayupo tayari kuwa
mke wa mtu
Jeremy:
tano
Baba:(anawaza kitu)
Jeremy:
sita…
Baba:
Jeremy unadhani tutafanyaje? unadhani ile familia itatuelewaje?
Jeremy:
saba… (anaiweka sawa bastola)
Baba:
sawa baba tutakusaidia
Jeremy:(anaacha kuhesabu na kuwaangalia) kivipi
Baba:
ila iwe siri mwanangu…mtakuwa wote kisiri sawa eeh…nitaenda mimi mwenyewe
kuongea na Miriam atanielewa tu haya shusha bastola mwanangu mzuri…eeh baba
yangu tulia mwanangu mzuri jamani
Jeremy:
kweli au unaniambia tu ili nishushe bastola
Baba:
nimekuahidi mimi baba yako
Jeremy:(anashusha bastola) sawa…utaenda lini?
Baba:
hata kesho please relax baba
Jeremy:
sawa
Mama:
sawa mwanangu utakuwa nae
Jeremy:
poa…kama mnanidanganya mtakuta maiti yangu
Mama:
hatukudanganyi
Jeremy:(anaingia chumbani kwake)
Mama:
huyu mtoto anataka kutuletea shida jamani loh!!!!!
Baba:
sijui itakuwaje…mzee Ken hatonielewa kabisaaaa…. yaani mimi najuta
Mama:
kwahiyo utaenda?
Jeremy:(yupo kwa ndani anawasikiliza)
Baba:
itabidi nikaongee na Miriam…wawe tu hata kwa muda wakati tunafikiria cha
kufanya ila Ariana na wazazi wao wasijue chochote
Mama:
huyu mtoto katukomesha loh!!!kazini haendi anakunywa tu pombe…
Baba:
mwanaume kampenda mwanamke... (anatikisa
kichwa) balaa hili jamani
Jeremy:(anatabasamu) ilibidi nitumie njia hii
ili niwe na kipenzi changu (anaangalia
ile bastola) bastola yenyewe toi(anacheka)nisameheni
wazazi wangu…nampenda Miriam kupita kiasi
(Wazazi
wanaendelea kuongea, huku Jeremy akiendelea kuwasikiliza)
0 Comments