MUNGU MKUU 13

 


SCENE 13: -

(Siku ya pili baada ya Jeremy kuwatishia wazazi wake, baba yake anaamua kwenda chuoni kwa kina Miriam ili aongee nae mawili matatu kuhusu Jeremy, anapofika anapiga simu yake)

Baba: simu imeita muda mrefu sana si cha ajabu yuko darasani na ana kazi (anakata na kutaka kuanza kuondoka, lakini kabla hajapiga hatuai)

Miriam:(anamuita) baba

Baba:(anageuka) mwanangu

Miriam:(kwa heshima kubwa) shikamoo baba

Baba: marahaba mama kwema?

Miriam: kwema

Baba:(anarudi na kukaa kwenye kimbweta kinachotumika na wanafunzi kujisomea)

Miriam: (nae anakaa pembeni yake) nimeona missed calls zako nikaona nitoke nje nije nijibu…nimetoka tu ndo nikakuona

Baba: ndio mwanangu nilikuwa na shida na wewe

Miriam: shida gani baba? na je unahisi mimi nitakusaidia

Baba: sio nahisi mwanangu najua kabisa utanisaidia kwa asilimia 100

Miriam:(anacheka kidogo) nambie sasa…nakusikiliza baba

Baba: una mahusiano na Jeremy?

Miriam:(anashtuka) hapana baba…nani amekuambia?

Baba: hamna aliyeniambia nakuuliza tu mama

Miriam: hapana baba Jeremy ni shemeji yangu alikuja nyumbani kumchumbia dada yangu na ninaheshimu hilo

Baba: sawa…kama huna mahusiano nae naomba uwe na mahusiano nae

Miriam:(anashangaa) baba...

Baba: ndo hivyo…. nakuomba lakini kama unaniheshimu mimi kama baba yako

Miriam: nakuheshimu sana baba lakini siwezi kuingilia uchumba wa dada yangu…

Baba: usijali utakuwa tu unajifanyisha tu mbele ya Jeremy

Miriam: hapana baba…hakuna kujifanyisha

Baba: Miriam nakuomba mwanangu, unajua mimi nina mtoto mmoja tu, akifa mimi sitakuwa tena na mrithi

Miriam: hapana unachoomba ni kitu ambacho hakiwezekani sio kitu rahisi kabisa

Baba: mwanangu anakupenda sana na anataka kuwa na wewe alitaka mpaka kujiua kisa wewe mpokee Miriam hata kwa kujifanya unampenda huko mbeleni tutajua

Miriam: siku dada yangu akijua itakuwa mwisho wangu, hata wazazi hawataelewa

Baba: najua hawataelewa ila naomba mwanangu…ikiwezekana nitakuwa nakulipa basi…nisaidie Miriam…mtulize tu afanye kazi zake jamani kila siku amekuwa ni mtu wa kulia na kutofanya kazi mwenzio ni mfanyabiashara na asipokuwa makini basi biashara zake zitayumba mama,msaidie huyu mzee aliyoko mbele yako

Miriam: lakini baba

Baba: hapana usiseme chochote kile, kaa utafakari…hautakuwa unafanya kitu kibaya sana…mkubali tu…hata kama wewe hutaki…yeye atajua umemkubali atatulia na kufanya kazi zake bila tatizo lolote na lile wazo lake la kujiua litaisha

Miriam: alitaka kujiua?

Baba: ndio…hiyo ni baada ya kumkatalia asiwe na wewe ndo akaamua kutaka kujiua…kiukweli sisi na mali zetu zote hizi tuna mtoto mmoja tu…yaani akifa jamani sijui tu itakuwaje

Miriam:(anakaa kimya huku kama kuna kitu anafikiria)

Baba: wewe fikiria tu mama lakini nipe jibu la uhakika nikamwambie

Miriam: tatizo wazazi wangu…

Baba: hawana shida bwana

Miriam:na dada yangu je?

Baba: hatajua kama una mahusiano na Jeremy we ukifika muda Fulani unamuacha tu na kusema kuwa humuwezi

Miriam: hapana baba kwanza hiyo sasa ndo itakuwa mbaya sana bora hata nimkatae ajue kabisa kuwa simtaki kuliko kuja kumkataa mbeleni…kaa tu ufikurie

Baba: jamani Miriam usiwe na roho hiyo jamani, nisaidie mimi baba yake Jeremy

Miriam: haya ni maisha baba…ni maisha ya watu watatu unataka kuyachezea

Baba: I don’t care…ninachojali ni maisha ya mwanangu…

Miriam: vipi kuhusu dada yangu?

Baba: mwanangu anamheshimu sana dada yako na sio kwamba anampenda…anakupenda wewe na yupo tayari kwa lolote ili awe na wewe…sasa mimi nakuomba unisidie jamani Miriam hutaki jamani?

Miriam: sio kwamba sitaki…

Baba: okay…ukweli ni kwamba Jeremy wala hampendi Ariana…je unataka Ariana aolewe na mwanaume asiyempenda unadhani mwisho wa siku itakuwaje?

Miriam: watapendana tu…kwani wakati mnaleta habari nyumbani kuwa Jeremy anataka kumuoa Ariana mlikuwa mnafikiria nini?

Baba: wala Jeremy alikuwa hatumii akili alitaka tu kuoa apate mwenza wa kuishi na kumuangalizia biashara zake wakati amesafiri kwenda ulaya na kadhalika…

Miriam: ameshamuona Ariana si amuoe

Baba: alikupenda tangu siku ya kwanza anakuona…hata mimi nilimuona amejutia haraka alizofanya

Miriam: maji yakishamwagika hayazoleki…hata ikiwaje hayazoleki, mlikuja nyumbani kumuoa Ariana muoeni mimi naomba mniache msije mkanigombanisha na ndugu zangu

Baba: kaa ufikirie kisha utamjibu yeye

Miriam: nenda tu ukamjibu kuwa Miriam kasema hapana

Baba: wewe unaogopa nini?

Miriam: sitaki tu…

Baba: aisee (huku ananyanyuka) basi sawa mama…mimi naenda mwanangu ila kama una lolote utanipigia au utampgia yeye…asante kwa muda wako mwanangu na Mungu akubariki

Miriam: amina baba, karibu tena

Baba:(anaondoka huku anaonekana hana raha)

Miriam: iam sorry yaani siwezi

Vanessa:(anakuja aliposimama) wewe mbona unaongea peke yako?

Miriam: yaani acha tu rafiki yangu…huyu Jeremy anataka kuniletea matatizo

Vanessa: yapi tena?

Miriam: amemtuma baba yake aje aniambie ananipenda

Vanessa:na wewe ukamjibuje

Miriam: unadhani ningemjibuje? huku wewe unajua kuwa Jeremy mimi ni shemeji yangu mtarajiwa

Vanessa:ni kweli humpendi?

Miriam: sio kwamba simpendi nampenda kama shemeji yangu tu

Vanessa:(anaguna) yaani hii ipo serious…mpaka baba mtu kaja kumuombea ujue ipo serious

Miriam: halafu anasema kuwa nijifanye tu nisiwe serious

Vanessa: kisa?

Miriam: eti Jeremy alitaka kujiua kisa mimi!!!

Vanessa: wewe Miriam embu mkubali mtoto wa watu hata kwa kujionyesha tu bwana

Miriam:(anaguna) are you sure hiyo haitakuwa tatizo?

Vanessa: nani atamwambia Ariana?

Miriam: hakuna siri kwenye hii dunia

Vanessa: ukiitunza vizuri inakuwa siri kubwa sana tu, mimi sitamwambia mtu na nina uhakika hata wazazi wake hawatamwambia mtu itakuwa ni siri yetu tu

Miriam: wewe Vanessa…unamjua dada Ariana

Vanessa: wewe usimuwaze…we angalia kumpa Amani kaka wa watu

Miriam: yaani wewe una kichaa kweli yaani nikishampa Amani

Vanessa: halafu unampenda moja kwa moja tunakula harusi

Miriam: hicho ndicho nachoogopa mwenzio

Vanessa: haitakuwa mbaya…kwahiyo utamjibu?

Miriam: sawa…ila tu akinihakikishia kuwa itakuwa ni siri

Vanessa: hayo ndo maneno…kwanza Ariana na Jeremy wanalingana haipendezi mwanamke na mwanamume walingane

(Wanacheka kisha wanarudi darasani)

 

Post a Comment

0 Comments