MUNGU MKUU 14

 


SCENE 14: -

(Asubuhi ya siku ya pili, Jeremy amekaa ofisini kwake anaonekana ana mawazo mengi sana, kwa mbali anamuona mtu kama Miriam anashangaa)

Jeremy: naota, nawaza au naona kweli? au? yule si Miriam?

Miriam:(anaingia mapokezi na kusalimiana na dada wa mapokezi) mambo

Dada wa mapokezi: poa karibu

Miriam: namuulizia mkurugenzi

Dada: una appointment nae?

Miriam: hapana

Dada:(kwa nyodo) kaa hapo nimwambie

(Wakati huo Jeremy anakuja)

Jeremy:(kwa sauti ya chini) Miriam?

Miriam:(anageuka na kuachia tabasamu)

Jeremy:(anajikuta anatabasamu pia)

Dada: ndo nilikuwa nakupigia nikuambie kuwa kuna dada anakutafuta

Jeremy:(kwa Miriam) karibu Miriam…twende tukaongee ofisini kwangu mama

(Wanaongozana kuelekea ofisini na baada ya hatua chache wanafika ofisini kwa Jeremy)

Miriam:(anasimama pembeni)

Jeremy: karibu keti...mbona umesimama?

(Ofisi ya Jeremy ni ya kifahari, fenicha zilizomo zinaonekana ni za gharama sana, hata kompyuta na runinga zilizomo ni za kifahari sana)

Miriam:(anakaa) asante sana

Jeremy:(anacheka) utakunywa nini?

Miriam: maji tu

Jeremy: maji na asubuhi yote hii?

Mirriam: inatosha tu… (anacheka kidogo)

Jeremy:(anatabasamu kidogo kisha ananyanyuka na kuchukua maji kutoka kwenye friji)

Miriam:(anaiangalia mandhari ya ofisi hiyo) ofisi yako nzuri sana

Jeremy:(huku anakuja alipo) asante, umeipenda? (anampa maji)

Miriam:(anapokea) ndio nimeipenda sana ni nzuri sana unajua
Jeremy:(huku anakaa) karibu Miriam

Miriam: asante sana

(Kimya kinapita huku kila mmoja wao anatafakari cha kuongea)

Jeremy:(anavunja ukimya) nambie

Miriam: well, nilipata ujumbe wako, nadhani kwanza kutoka kwako lakini pili kutoka kwa baba yako

Jeremy…. ndio

Miriam: nimeona ni sawa tu

Jeremy: sawa nini?

Miriam: sawa kwamba mimi na wewe tunaweza kuwa wapenzi

Jeremy:(anapata furaha kubwa na bila kutegemea ananyanyuka kutoka kwenye kiti chake na kumbeba Miriam) kweli Miriam

Miriam: yes...kweli

Jeremy:(anambusu shavuni) asante Miriam, I swear, you have me the happiest man, I love you so much my queen…

Miriam:(anajaribu kushuka maana amebebwa)

Jeremy:(bado amembeba na anamnyima nafasi ya kushuka) usiogope…nakupenda Miriam, sasa nitakuoa utakapokuwa tayari

Miriam: nishushe watu wanaweza kuja

Jeremy: sioni vibaya kumwambia kila mtu kuwa wewe ni mke wangu mtarajiwa

Miriam:(anacheka kidogo) okay najua kuwa huoni vibaya ila naomba nishuke please

Jeremy: okay darling(anamshusha)

 Miriam:(anakaa kwenye kiti)

Jeremy:(anavuta kiti na kukaa pembeni ya Miriam) siamini my love kama hatimaye umenikubali…unajua umenisumbua sana…yaani wewe muone

Miriam:(anacheka) kawaida tu

Jeremy: I will make you the happiest woman in the world…I will surely marry you

Miriam:(anajisemea moyoni) iam sorry nakudanganya ila sitaki ujiue Jeremy kisa mimi halafu nionekane mimi ndo chanzo cha kifo chako, ninaumia kuwa nina msaliti dada yangu

Jeremy: najua kuna kitu unawaza…na ninajua kuwa unawaza kuhusu dada yako Ariana…labda sijakuambia kitu…mimi na Ariana tumeachana muda mrefu sana…yaani tangu nimeanza kukufukuzia, alikubali na kusema kuwa atawaambia wazazi wake

Miriam: usingemuacha, ungeendelea kuwa nae tu hata kwa kujifanyisha

Jeremy: siwezi

Miriam: dada yangu…ataumia sana… (Anaanza kukasirika)

Jeremy: no baby usikasirike okay nitarudiana nae Kwa kujifanya tu najua tutakuwa tunaudhulumu moyo wake ila kwakuwa pia najua hiyo itakuwa raha moyoni mwako

Miriam :( anajisemea moyoni tena) yaani huu mchezo sijui utakuja kuishiaje tu

Jeremy: nini tena?

Miriam: hamna mbona mimi nipo sawa kabisa?

Jeremy: yaani naona una mawazo kweli... (Anamsogelea) please Miriam this is our lives hatutakiwi kuwaza wengine watafikiriaje

Miriam:(katika hali isiyo ya kawaida anamuona Jeremy ni wa tofauti sana, anaanza kumuangalia vingine)

Jeremy: I swear nitakupenda na kukutunza sana…nitakupa chochote utakachotaka na mwisho nitakuoa

Miriam:(anamuangalia usoni huku anajisemea kitu fulani kichwani mwake) namuonaje? mbona naanza kumpenda? Mungu wangu this is wrong…

Jeremy: baby, you don’t have to worry about anything… (anaibusu mikono yake) nakupenda Miriam na utaona tutakavyokuwa na raha baby…utaenjoi

Miriam: okay haina shida… (anajisemea moyoni) mbona najichanganya?

Jeremy: umekaa kimya najua unamuwaza Ariana sana…ok nitakuwa nae ila I promise nitatunza penzi letu

Miriam: okay(ananyanyuka)baadae

Jeremy: una haraka ila naelewa kuwa unataka kuwahi chuoni…tutakula dinner pamoja au sio

Miriam: nitakuambia…

Jeremy:(anamshika mkono) mawasiliano ndo nguzo yetu, najua itakuwa ngumu kwetu, ila naomba tujitahidi kuwasiliana baby

Miriam: okay

Jeremy: i love you baby

Miriam: I love you too (kisha anatoka)

Jeremy :( anabaki anashangilia sana) yes…finally nimempata…ni wangu sasa..nimepata mke(anajitupa sofani huku anashangilia kama mwendawazimu)I love her so much…leo nitaenda kwa baba na mama na kuwaambia kuwa nampenda sana Miriam na tayari tumeshakuwa wapenzi maana amenikubali na Oh My God!!!au naota?hii itakuwa ndoto…amka Jeremy ni muda wa kuamka…Oh My God,I can not believe ni kweli…kumbe Mungu unajibu maombi sana unajua ee(anasimama yaani kwa kifupi hatuliii)najua nimetumia  njia ya udanganyifu  kumpata Miriam ila ukweli ni kwamba nampenda sana huo ndo ukweli,sasa maisha yamekuwa maisha sasa,yamekuwa na maana kabisaaaaaaaaa…maana nimempata wangu wa ubani…I will take care of her forever…nitamsomesha,nitamtunza,nitamjengea nyumba,nitamsubiri mpaka atakapokuwa tayari nitamuoa I swear atakuwa malkia wa himaya yangu..yes(anachukua simu yake na kuingia katika akaunti ya Miriam ya Instagram na kuanza kuangalia picha zake)wow look at my girlfriend,she is just so beautiful(anabusu moja ya picha za Miriam)my wife..(Anarudi kukaa kwenye kiti chake cha kuzunguka) nitaikuza hii picha na kuiweka hapa mezani...Kwangu (anatabasamu kidogo)

 

Post a Comment

0 Comments