MUNGU MKUU 15

 


SCENE 15: -

(Ni usiku, kila kitu kipo kimya kasoro sauti za wadudu waliao usiku, Jeremy yupo nyumbani kwake, ametulia anapata kinywaji chake huku anaangalia mpira kupitia runinga yake kubwa iliopo katika sebule yake ya kifahari)

Jeremy:(anatabasamu kidogo) iam so happy, finally Miriam ni wangu… (anacheka kidogo) sitaruhusu kitu chochote kiharibu furaha nayoisikia sasa hivi…sio wazazi wangu, sio wazazi wa Miriam na sio Ariana (anakunywa kinywaji kidogo) Ariana anatakiwa akubali kuwa siwezi kumpenda yeye kama ninavyompenda Miriam (anachukua simu) ngoja nimpigie kipenzi changu, tangu nilivyomuona asubuhi sijamuona tena(anapiga)

(Simu inaita)

Miriam:(anatoka kuoga, anaichukua simu kisha anaipokea) hello

Jeremy:(sauti nzito Zaidi) baby? umelala?

Miriam:no sijalala

Jeremy: unafanya nini?

Miriam: ah nipo tu nimetoka kuoga

Jeremy: okay…mi naangalia mpira hapa, nikaona sio mbaya nikusalimie

Miriam:(anacheka kidogo) asante sana

Jeremy: nimekumisi sana. sijakuona tangu asubuhi ulipokuja kunipa habari njema

Miriam:(anatabasamu) hata mimi nimekumisi(anajishangaa)

Jeremy: kweli?

Miriam: sikudanganyi

Jeremy: asante honey…nataka nikulipie chuo

Miriam: No Jeremy…

Jeremy: kwanini?

Miriam: kumbuka haya mahusiano ni siri kubwa sana…nadhani nilikuambia

Jeremy: nakumbuka umeniambia yawe siri lakini je unadhani yatakuwa siri milele?

Miriam: kwa sasa hivi naomba usinifanyie chochote…

Jeremy: usinifanyie hivyo Miriam...

Miriam: tulikubaliana leo asubuhi kuwa itakuwa siri…kumbuka wewe unachukuliwa kuwa ni mkwe yaani mchumba wa Ariana…maana hata kama umeachana na Ariana bado Ariana hajatuambia sisi kama familia

Jeremy: okay…Ariana akiwaambia je utaniruhusu nikulee kama mke wangu mtarajiwa

Miriam:(anakaa kimya)

Jeremy: naomba jibu...utaniruhusu?

Miriam: uhusiano wetu, ni forbidden passion

Jeremy: ukimaanisha nini?

Miriam: haturuhusiwi kuwa pamoja hata iweje…maana hata baba na mama yangu hawataruhusu yaani uachane na Ariana halafu uwe na mimi…kwanza haitaleta picha nzuri

Jeremy: kwahiyo unataka kuniambia haya mahusiano yatakuwa ya siri milele hata ndoa yetu itakuwa ya siri?

Miriam: tutajua mbele kwa mbele

Jeremy: sawa baby ilimradi tu usifikirie kuniacha

Miriam: sitakuacha milele…nakuahidi

Jeremy: nakupenda Miriam

Miriam: nakupenda pia…(anacheka)

Jeremy:(anatabasamu) lala sasa…na mimi nitalala mpira ukiisha

Miriam: unaangalia mpira peke yako?

Jeremy: ndio…

Miriam: pole…

Jeremy: ndo maana nataka uje tuwe tunaangalia wote

Miriam:(anacheka sana)

Jeremy: umefurahi mwenyewe natamani ningekuwa hapo nishangae dimples zako

Miriam:(anatabasamu)

Jeremy: haya bwana usiku mwema

Miriam:na kwako pia

(Kwa pamoja wanakata simu)

Miriam: mimi nimekuwaje? mbona kama nipo serious nampenda Jeremy? au nimempenda Mungu wangu na baba yake aliniambia nijifanye kumpenda mbona kama nampenda kweli? nampenda Jeremy…yes nampenda kweli kabisa

(Upande wa Jeremy)

Jeremy: nitafanya kila kitu kulitunza hili penzi, sitaruhusu mtu yeyote avuruge hili penzi…sio wewe mwenyewe Miriam maana naona kama unasita kwa mambo Fulani (anajikuta anashangilia mpira ghafla) GOOOOOOOOOOOOO!!!ushindi mara mbili… (anapiga makofi) mwanamke niliyemfatilia muda mrefu sasa nipo nae na hawa jamaa wamenisuuza roho yangu loh!!!mambo ni motoooooooooo

(Upande wa Miriam, anamaliza kuvaa nguo zake za usiku na kujilaza kitandani)

Mary:(anagonga mlango wa chumbani kwa Miriam) hodi...

Miriam: karibu ma mdogo

Mary:(huku anaingia) asante mwanangu…vipi haujalala (anakaa pembeni yake)

Miriam: nimetoka kuoga...sasa hivi

Mary: leo umechelewa kuoga…

Miriam: ah nimeoga mara mbili …nilikuwa nimelala sasa usingizi ukawa hauji ndo nikaamka kuoga tena

Mary: unakosa usingizi mwanangu

Miriam:(anaitikia kwa kichwa ishara ya kukubali)

Mary: una mawazo gani?

Miriam: ya masomo yangu…

Mary: soma mwanangu

Miriam: nasoma ma mdogo

Mary:(anatabasamu)

Miriam:(anamuangalia usoni) halafu ma mdogo mbona tunafanana hivi?

Mary:(anashtuka sana)

Miriam: unajua mimi natakaga kukuuliza sema huwa nakosa muda na nafasi

Mary:(anajichekesha) itakuwa kwa sababu tunapendana labda

Miriam: kwahiyo watu mkipendana mnafanana? kwahiyo nitafanana na Jeremy?

Mary:(anashtuka) unasemaje?

Miriam:(anajishtukia) sijasema chochote

Mary: Jeremy ni nani yako?

Miriam: kuna kaka anaitwa Jeremy darasani kwetu

Mary: mnapendana?

Miriam: huwa tunataniana

Mary: soma mwanangu sawa mama…lakini pia mheshimu Jeremy ni shemeji yako sawa ee

Miriam: sawa ma mdogo

Mary: haya usiku mwema (ananyanyuka na kuondoka zake)

Miriam: namheshimu vipi Jeremy huku nafsi yangu imeshampenda…nampenda na wala simuoni tena kama shemeji yangu, nimeanza kuota kuolewa na Jeremy… (anakaa kimya kidogo) hivi mimi nina akili kweli...eti jamani nampenda shemeji yangu…kama kumpenda Jeremy ni kosa niko tayari kuhukumiwa hata kifungo cha maisha...Nampenda Jeremy

(Upande wa Jeremy)

Jeremy: nampenda Miriam…nipo tayari kwa lolote, iam ready hata nipigwe vibaya na mzee Ken ila tu niwe na Miriam she is my everything

Post a Comment

0 Comments