SCENE
21: -
(Majira
ya saa nane mchana, upepo mwanana unavuma, Jeremy na Miriam wamekaa katika
mgahawa mmoja wa kifahari wanapata chakula cha mchana huku kila mmoja
akifurahia hali ya hewa ya wakati huo)
Jeremy:
wow napenda hali hii ya hewa, it’s beautiful (anaachia tabasamu)
Miriam:(huku
anakula) of course ni nzuri sana hata mimi napenda sana hali hii (anacheka
kidogo)
Jeremy:(anatabasamu)
Miriam wewe ni mzuri sana
Miriam:(anacheka
kwa aibu kidogo) umeanza kwani tunaongelea uzuri wa nini si wa hali ya
hewa?
Jeremy:(anacheka)
basi tu nimeona niingize ya urembo wako…kwani nimefanya kosa?
Miriam:
okay bwana tuendelee kula...
Jeremy:(anakula
kijiko kimoja) nataka nikuoe…
Miriam:(anacheka
kidogo) mara hii? mbona mapema
Jeremy:
mapema? (anacheka kidogo) hapana sio mapema…bwana mimi tangu nimekuona
nimekuwa na wazo la kukuoa kwahiyo sio mapema
Miriam:
Jeremy…mimi bado mwanafunzi na isitoshe ndo kwanza nina miaka 18 acha nile
ujana kwanza
Jeremy:(anacheka)
wewe mtundu...kwani ukiwa mke wangu hutakula ujana?
Miriam:(anacheka)
sasa nitakulaje ujana huku nitakuwa mke wa mtu
Jeremy:si
tunakula ujana wote hata mimi nataka kula ujana mbona?
Miriam:no
baby…tusubiri
Jeremy:
honey...mbona wewe kila kitu hutaki? Unajua sikuelewi eeh
Miriam:
nimekataa nini tena jeremy?
Jeremy:(anacheka)
si umekataa gari?
Miriam:
jamani Jeremy...siwezi kupokea gari...unajua nitaulizwa sana nyumbani
Jeremy:
unawaambia la Vanessa
Miriam:
siwezi kudanganya hivyo maana wanajua maisha yake
Jeremy:si
atasema kuwa amepewa na bwana ake
Miriam:(anacheka)
yaani wewe…
Jeremy:
kwahiyo nitakuletea gari mpenzi
Miriam:mi
naogopa Jeremy
Jeremy:
usijali nitaongea na vanesa nitamfundisha cha kusema...nataka uwe na gari
litakalokuwa linakupeleka popote unapotaka my soulmate, sitaki udhurure njiani
kwa miguu wataniibia
Miriam:
hapo sasa ndo watu watashangaa…kunipeleka kila napotaka? By the way sidhururi
kwa miguu nyumbani kuna gari
Jeremy:
najua nataka tu uwe na gari Mirriam la kwako wewe kama wewe
Miriam:(anaguna)
anyways, hilo gari liko wapi?
Jeremy:
gereji kwangu, nyumbani kwangu
Miriam:
Jeremy una utani…si wanajua magari yako
Jeremy:ni
jipya--- relax baby usiogope hakuna aliyewahi kuliona…mpaka dereva yupo
Miriam: (anashangaa)
wewe Jeremy wewe?
Jeremy:
mwanamke…tutasema ni dada yake Vanessa
Miriam: (anatabasamu)
haya mimi sina cha kusema umeshaamua…
Jeremy:
okay baby…asante kwa kupokea zawadi zangu next itakuwa nyumba
Miriam: (anashangaa)
wewe Jeremy?
Jeremy:
you are my wife baby…lazima nikupambe na nikutunze
Miriam:(anatabasamu)
asante baby
(simu
ya Miriam inaita)
Miriam:(anaiagalia
simu yake) ma mdogo(anapokea)hello ma mdogo
Jeremy:(anataka
kuongea)
Miriam:(anamuwekea
kidole mdomoni ishara ya kumnyamazisha)
Mary:
Miriam uko wapi si umemaliza masomo yako saa saba sasa hivi ni saa nane na
dakika kadhaa…uko wapi?
Miriam:(anashikwa
kigugumizi) ah---- ah …nipo nakula na Vanessa…
Mary:mpe
simu niongee nae
Miriam:(anashikwa
kigugumizi) wewe Vanessa (anaendelea kuongea na simu) ma mdogo Vanessa
kaenda chooni
Mary:
akirudi nipigie…
Miriam:ma
mdogo jamani mbona hivyo? huniamini?
Mary:
Miriam nimekuona mara nyingi sana una ukaribu na shemeji yako mchumba wa dada
yako Ariana
Miriam:
sipo na Jeremy mbona, wasiwasi wako tu ma mdogo
Mary:
haya mama kuwa makini usije ukajiingiza kwenye matatizo
Miriam:
usijali ma mdogo...
(Wanakata
simu)
Jeremy:(anaguna)
hivi wewe una mahusiano gani na mfanyakazi wenu yule Mary sijui ndo mnamuita ma
mdogo
Miriam:
mahusiano kivipi?
Jeremy:mi
naona mnafanana kweli
Miriam:
halafu watu wengi wameniambia hivyo mi mbona sioni kama nafanana nae? anyway mi
sijui nachojua ni kwamba mfanyakazi wetu ila tunampenda kama ndugu basi hivyo
tu mengine sijui kwakweli
Jeremy:
kama ni hivyo sawa ila fatilia (anacheka)
Miriam: (anacheka)
anyways, mi nimeshamaliza kula…naona mwenzangu bado unajivuta
Jeremy:
nataka nikae na wewe…muda mrefu…napenda kukuangalia (anacheka)
Miriam:(anacheka
kisha anaguna) yaani wewe unajua hatuwezi kufanya hivyo, umeona hapa tu
nimeshapigiwa simu ya kuulizwa
Jeremy:
yatapita tu baby ipo siku tutakuwa pamoja kwa Amani na uhuru
Miriam:
dah sijui itakuwaje siku hiyo…baba ataniua
Jeremy:
hapana…nina Imani ataelewa…
Miriam:
sijui tu
Jeremy:
hivi unajua wazazi wangu mara ya kwanza walichukulia kama kunisaidia tu ili
nisijidhuru ila kwa sasa wanasema nikuoe wewe…wanani sapoti
Miriam:
bora yako…unajua kwa wazazi wangu bora usingekuja kwa ajili ya kumuoa Ariana
Jeremy:
tunapanga ila Mungu ana mipango yake labda Mungu alikuwa ananisukumia kwenu ili
nikutane na wewe…Miriam sikupanga kwamba nikija kwenu nikupende wewe…wazazi
wangu wanaelewa nina Imani na wazazi wako wataelewa tu tuwajaribu…tuone
Miriam:
tujaribu mapema maana hapa tunachofanya ni usaliti na inaniumiza
Jeremy:
naelewa my queen…nitamwambia mama na baba wakavunje uchumba wangu na Ariana
baada ya hayo basi tutawaambia
Miriam:
umeniambia kuwa umevunja uchumba na Ariana
Jeremy: yes,
baby nimevunja, kwanini unaniuliza?
Miriam:(anacheka
kidogo) unajua aliniambia niongee na wewe kuhusu wewe nay eye
kurudiana…halafu badala yake nipo hapa nina mahusiano na wewe kwakweli
najisikia vibaya sana unajua
Jeremy: najua...mpenzi
mimi na wazazi wangu tunajiuliza tuombe vipi msamaha kwa hili…na jinsi
tunavyochelewa ndo mambo yanazidi kuwa magumu...Wazazi wangu wanatamani hata
sasa hivi waje kwenu na kusema kuwa nakupenda wewe na sio Ariana ila wanaogopa
wazazi wako watasema…pamoja na hayo mimi naamini tukijaribu wataelewa
Miriam:
embu tusiyawaze hayo…nipeleke nyumbani kabla mama hajanipigia(ananyanyuka)
Jeremy:(huku
ananyanyuka) sasa mtu mwenyewe muoga...nakufikishaje nyumbani
Miriam:
unanishushia mbali…
Jeremy: okay...kesho
gari lako litakuja (ananyanyuka anamshika mkono Mirriam kisha wanaondoka)
0 Comments