SCENE
22: -
(Asubuhi
ya kesho yake, kuna gari zuri sana linafika nyumbani kwa kina Miriam, ndani ya
gari hilo kuna dereva mwanamke, na Vanessa)
Miriam:
wow, gari zuri sana
Vanessa:
ingia twende mwenzangu wasije wakatoka wakanipa maswali hapa nikashindwa
kuyajibu
Miriam:
tulia mtoto… (analishangaa gari) yaani Jeremy ana mambo huyu(anacheka)
Vanessa:
jamani...twendeni nyie
Dereva:(anacheka)
si anakupenda…mwenzio anakupenda kweli mwenyewe anasema wewe ndo mkewe
Vanessa:
jamani twendeni
Miriam:
okay twendeni
(Wanapanda
gari)
Keddy: (anatokea
ndani) hamjambo?
Vanessa:
eeh makubwa…yamenikuta
Vanessa:
hatujambo mama shikamoo
Dereva:
shikamoo
Keddy:
marahaba, hamjambo (anawaangalia kisha anaangalia gari) gari zuri
sana…halafu linaonekana la thamani…la nani?
Miriam:(anadakia)
la Vanessa…
Keddy:(kwa
mshangao) la Vanessa?
Vanessa:
huyu Miriam bwana hili gari ni la dada yangu…sasa ameona awe anatupa lifti ya
kwenda chuo…ili tupunguze gharama za nauli
Dereva:
ndio ni langu nawaonea huruma ndo nimeona niwe nawapa lifti kwa kipindi
nikiwepo
Keddy:
wewe unafanya kazi wapi? Maana dah!!! Gari la thamani sana hili
Dereva:
mimi nipo Nairobi nafanya kazi huko
Keddy:
wewe ni dada yake kabisa?
Dereva:
mimi ni mtoto wa mama yake mdogo
Vanessa:
eeh ma mdogo…(anajichekesha)
Keddy:
basi sawa haina shida...nendeni chuo mtachelewa
Vanessa:
haya...Mama…baadae
Keddy:
baadae
Miriam:
bye mama
Keddy:
bye baby
(Wanaondoka)
Vanessa:(anashusha
pumzi) yaani wewe na mumeo mtakuja kuniletea balaa wallahi
Miriam: embu tulia huko kwanza yameisha jamani ee (anacheka)
Dereva:(anacheka)
Vanessa:
yaani Jeremy aliponiambia nije nidanganye alikuwa anasema kirahisi kweli
Miriam:
sehemu ngumu ni ile mwanzoni ila sasa kila kitu kipo sawa…mama amejua kuwa wewe
ndo mwenye gari
(Wanacheka)
Vanessa:
sio mimi gari ni la dada yangu…umesahau?
Miriam:
oh yes…nilikuwa nimesahau
Dereva:
usishau maana mama yako anaonekana ana maswali jamani…(anaguna)
Miriam:(anacheka)
(Simu
ya Miriam inaita)
Miriam:(anapokea)
baby
Vanessa:
eeh…mwambie nimetoka jasho atume hela ya soda
Miriam:(anacheka)
jamani
Jeremy:
mambo…
Miriam:
poa…shikamoo
Jeremy:
marahaba…ni matumaini yangu mpo njiani mnaenda chuo
Miriam:
yes…baby nimeona gari daddy asante ni zuri
Jeremy:
usijali just for you my love…umelipenda?
Miriam:
vibaya sana
Jeremy:
tell me about it babe, mama au ma mdogo wameliona?
Miriam:
wewe mama ameliona tumejiumauma wewe (anacheka) ila tumeeleweka
Jeremy:
sasa je ulikuwa unaogopa…kifuatacho ndoa
Miriam:(anashangaa)
He--- jamani ...unataka niuliwe mimi eti?
Jeremy:
hufi bwana wataelewa
Vanessa:
mwambie nataka hela ya soda nimetoka jasho sana
Miriam:(anacheka)
msikie Vanessa… (anampa simu Vanessa)
Vanessa:
baby ake…hela ya soda ndugu yangu maana sio kwa jasho
Jeremy:
utaona mpesa imethibitishwa hapo...
Vanessa:
asante baby akeeee
Jeremy:
(anacheka) mwehu wewe (anacheka tena) haya poa…
Vanessa:
shika simu yako (anamrudishia simu Miriam)
Miriam:
nambie
Jeremy:
I love you…do you love me?
Miriam:
yes
Vanessa:
yes, nini si useme I love you too
Miriam:na
wewe ni Mbeya…
Vanessa:(anacheka)
Jeremy:
tell me baby…
Vanessa:
mwambie
Miriam:(anacheka
kwa aibu)
Vanessa:
mwambie sasa
Miriam: yes,
baby I love you
(Wanafurahi)
Jeremy:
asante baby...leo siku yangu itakuwa nzuri sana natumaini na yako itakuwa nzuri
kama yangu
Miriam:
lazima iwe nzuri
Jeremy:
we are soulmates baby...na sijui kwanini sikukuona mapema hata njiani nije
nikuchumbie badala ya dada yako…
Miriam:
umeanza sasa kuleta stori za Ariana baby unajua nikisikia Ariana najisikia
vibaya maana nampenda sana dada yangu na dada yangu anakupenda sana wewe
jamani…tusiwe tunamuongelea tukimuongelea tu najishisi kuachana na wewe
Jeremy:
basi poa nisamehe…sitaki kukuudhi…
Vanessa:
wacha we…huko kudeka vipi?
Miriam:(anacheka)
ila Vanessa nini lakini?
Jeremy:
tukutane lunch…sasa hivi una gari sitaki kuwa nakuja chuoni mara kwa mara
Miriam:
palepale pa jana?
Jeremy:
yes…
Miriam:
ok
(Wanakata
simu na safari ya kuelekea kwenda chuo inaendelea)

0 Comments