MUNGU MKUU 23


 

SCENE 23: -

(Jioni nyingine njema tena yenye kupendeza machoni pa Mungu na kwa wanadamu, jua linaanza kuzama na kila kitu kinaonekana kutaka kupata pumziko baada ya siku ndefu, Ariana anafika katika jumba la kifahari la mfanyabiashara kijana Jeremy)

Ariana:(huku anashuka kutoka kwenye gari) leo nataka kumpa surprise ya maisha huyu mwanaume (anachukua boksi kubwa na kuanza kutembea) mpaka asipate tena wazo la kutaka kuniacha mimi (anaangalia gari ambalo analifahamu) hili si ndo gari linalomleta Miriam siku hizi linafanya nini huku? (anapiga tena hatua) eeh (anauelekea mlango na kuufungua akiwa na lengo la kumfurahisha Jeremy)

(Anamkuta amemkumbatia Miriam)

Ariana: (kwa mshangao) Jeremy?

Jeremy:(anamuangalia)

Ariana:na mdogo wangu?

Miriam:(anaogopa sana)

Jeremy: Ariana listen, and iam so sorry hata mimi nilijitahidi sana kupigana na hisia zangu nimeshindwa nampenda sana Miriam ni mwanamke ninayetaka kumuoa

Ariana:(machozi yanamlenga) this cant be…please tell me it is a dream (analia)

Jeremy: usitoe machozi Ariana…mbona nilikuandaa kwa hili jamani?

Ariana: najua uliniandaa mapema sana Jeremy lakini hukuniandaa kwa hili…katika wote umemchagua Miriam? Jeremy jamani

Jeremy: iam so sorry Ariana…hata hivyo mbona mahusiano yetu hayakuwa ya karibu sana?

Ariana:(machozi yanamwagika) Jeremy nakupenda, jamani kwanini lakini?

Jeremy: sasa kwanini nini? mimi sina jibu la swali lako Ariana tulizungumzia hilo tena mara nyingi sana

Ariana: najua ni mara nyingi sana tulizungumzia hilo ila hatukumuongelea Miriam

Miriam:(anaonyesha wasiwasi)

Ariana:(kwa Miriam) kama ilivyo kawaida yako umenizunguka Miriam

Miriam: sio kweli dada…nilijaribu sana…ila...

Ariana: kimya…kimya sitaki kusikia chochote Miriam… (anafuta machozi kisha anatabsamu) usijali mdogo wangu unadhani nimekasirika…nimefurahi sana tu kuwa na wewe umepata boyfriend hongera sana Jeremy is nice guy

Miriam:(anashangaa) really? Are you sure? (anazidi kushangaa)

Ariana:(anafuta machozi) nilikuwa tu najifanya kukasirika baada ya kukuta hivi

Jeremy: are you sure? I mean are you serious?

Ariana: yes…iam serious

Jeremy: hujachukia?

Ariana: nachukia nini sasa huku Miriam ni mdogo wangu akipata kitu kizuri na mimi nimepata… si ndio baby sister?

Miriam: dada(anamkumbatia)asante sana dada yangu…nakushukuru sana...

Ariana: usijali sana mama... (anaweka boksi mezani) enhe mmeshawaambia wazazi?

Jeremy: wazazi wa pande moja ndo wanajua… (anacheka kidogo) upande mwingine hawajui...ila tutawaambia

Ariana: waambieni bwana mapema ili wajue tule wali sie

(Wanacheka)

Jeremy:(kwa Ariana) yaani siamini kama umekubali shemeji yaani nilivyokuwa nakuwazia ni tofauti kabisa na ulivyoonyesha

Ariana: kwanini jamani?

Jeremy: basi tu nilihisi hivyo kutokana na hali yenyewe… (kwa Miriam) my love umesikia sasa tupo watatu tutatetea huu uhusiano

Ariana: mkitaka nitamwambia baba na mama kuwa mnapendana najua watakubali tu...wanampenda sana Miriam na watamfanyia kila kitu…Miriam is such a lucky girl kila kitu kizuri anapata yeye upendo wa wazazi na mwanaume mzuri kama wewe Jeremy

Jeremy: hata usiseme hivyo shemeji mbona hata wewe wazazi wako wanakupenda sana? na pia huu sio mwisho mimi sikuwa tu mwanaume ambae Mungu amekupangia nimefurahi tu jinsi ulivyoochia mapema hivyo…sasa namuomba Mungu akusaidie na wewe upate mwanaume mzuri sana shem na tule ubwabwa kabla ya Miriam

Ariana :( anaguna) eti eeh

Jeremy: ndio

Miriam :( anaonyesha furaha)

Ariana:(anatabasamu)

Jeremy:by the way (anaangalia boksi) umeleta nini humo embu tufungue ulikuwa umeniletea mimi… (kwa Miriam) naomba tufungue box shemeji ametuletea zawadi

(Jeremy na Miriam wanafungua box)

Jeremy: wow…bonge la keki

Ariana:(anawafuata) kama nilijua nitawakuta wawili

Jeremy:(anaangalia ilivyoandikwa) I love you, Jeremy?

Ariana: sasa hapo iangalie hivi kwamba Miriam ndo amekuletea

Jeremy: good idea (kwa Miriam) eti unaonaje baby

Ariana: halafu nimeona gari hapo nje hilo gari huwa linamleta Miriam nyumbani ni la nani?

Jeremy:ni la Miriam nilimnunulia

(Maneno ya Jeremy yanajirudia mara nyingi sana kichwani kwa Ariana)

Miriam: Jeremy

Jeremy:(anatabasamu) nini, Ariana yupo upande wetu…ni msiri wetu mpaka pale tutakapoamua kuwaambia wazazi si eti Ariana?

Ariana: bila shaka kabisa

Jeremy:(kwa Miriam) anza kujifunza kuwa mke kalete kisu na sahani tukate keki tule

Ariana:(anaangalia saa)mi naona niwaache kuna sehemu nawahi(anaondoka bila kusikia chochote)Mungu wangu(Anatoka nje)wanadhani nimekubali (anatabasamu tabasamu la kiovu)sijakubaliana nao…Miriam atajuta kwanini aliamua kunisaliti na maisha yake yatakuwa mabaya kuliko zamani nitamfanyia kitu mbaya mpaka dunia itikisike…pendaneni Miriam na Jeremy pendaneni sana maana muda wenu wa kupendana unakaribia kuisha..pendaneni Zaidi na Zaidi…nitakurudia Jeremy…utakuwa wangu peke yangu…(anacheka kiovu)nikimuua Miriam hata wazazi watakulazimisha kunirudia mimi halafu tutafunga ndoa nitakuwa malkia wa himaya yako na mali zako zote.. zitakuwa zangu nitaringa mie (anacheka kisha anaingia kwenye gari lake analiwasha kisha analiondoa)

(Huku ndani walipo Jeremy na Miriam)

Miriam: nimeshangaa dada alivyochukulia poa mahusiano yetu

Jeremy: mimi nimepagawa…

Miriam: ila sijapenda ulivyo mwambia kuwa lile gari ni langu

Jeremy: kwani uongo Miriam?

Miriam: haikuwa kitu kizuri mtu baada ya kupokea mshangao wa maisha umuongezee jambo lingine

Jeremy: acha uoga…bwana. enhe ulikuja kuniambia nini? maana dada yako alikuja ndo kwanza ulikuwa unaingia ndo maana ametukuta tunakumbatiana (anacheka)

Miriam: kuna tour chuoni nadhani wikiendi hii kuna mengi ya kujifunza ila naona uvivu kwenda

Jeremy: kisa?

Miriam: nitakuwa peke yangu

Jeremy: Vanessa je?

Miriam: haendi

Jeremy: nenda tu baby si ni kujifunza?

Miriam: ndio

Jeremy: nenda tu nitakusindikiza mpaka mtakapopandia gari

Miriam: haya bwana kwakuwa umesema wewe ngoja nitaenda

Jeremy: that’s like my girl(anatabasamu)

(Wanatabasamu huku wanaendelea kumega keki taratibu)

Jeremy: I love you(anatabasamu)

Post a Comment

0 Comments