SCENE
24: -
SIKU
YA TOUR: -
(Asubuhi
nyingine njema mbele ya macho ya watu na Mungu wa mbinguni aliyeifanya hivyo,
wanachuo mbalimbali wamefika chuoni tayari kwa ajili ya kuondoka kuelekea tour
kwa ajili ya masomo yao. Jeremy na Miriam wanafika mahali hapo pia)
Jeremy:
baby nitakumisi sana unajua
Miriam:(anatabasamu)
narudi kesho tu hapa…
Jeremy:
siku moja bila wewe kiukweli kabisa sitaweza…
Miriam:
come down baby…simu zipo nitakuwa nawasiliana na wewe kila mara don’t worry
Jeremy:
simu tu haitoshi baby…nimezoea kukuona kila siku na kila saa
(Wanacheka)
Miriam:
wewe tulia tu bwana nikirudi tu nakuja kwako halafu ndo naenda nyumbani ingawa
(kuna kitu anafikiria ghafla)
Jeremy:
nini tena? Mbona umekuwa myonge ghafla?
Miriam:
nakosea sana Jeremy yaani nakosea kuwa na wewe
Jeremy:
umeanza baby mbona hata Ariana ameshakubaliana na uhusiano wetu kwani nyumbani
jana ulipoenda walikuambiaje?
Miriam:
hawakusema chochote ingawa ma mdogo Mary anatuhisi na huwa ananiambia nikuache
Jeremy:
oh (anamshika kidevu) sasa najua kwanini unakuwa na mawazo unamsikiliza
sana ma mdogo
Miriam:ma
mdogo ananipenda sana nimepewa hadithi kuwa alininyonyesha nilipokuwa mchanga
Jeremy:
kwanini sasa yeye akunyonyeshe?
Miriam:
mama yangu hakuwa na maziwa ya kutosha na ma mdogo alikuwa ametoka kujifungua
wakati huo
Jeremy:
mtoto akaenda wapi?
Miriam:
alikuwa si riziki
Jeremy:
maskini basi ndo maana anakupenda anaona wewe ni mwanae kabisa
Miriam:
sasa hataki hata kidogo kusikia nina mahusiano na wewe
Jeremy:
ah atazoea tu kwani sisi tulipanga kupendana si imetokea tu?
Miriam:
najua imetokea tu ila huoni kuwa ni kosa?
Jeremy:
huwa unaniudhi hapo hapo mke wangu yaani wewe unawaangalia sana hao ishi maisha
yako
Miriam:
unanifundisha vibaya (anacheka) sitakiwi kuwa na wewe
Jeremy:
nitakusubiri mpaka utakapokuwa tayari nitakuja kwenu kukuchumbia nitakuoa na
kuzaa na wewe vitoto virembo kama wewe vyenye tabia ya upole kama wewe
Miriam :(
anacheka)
Jeremy
:( anatabasamu)
(Rafiki
mmoja wa Miriam anawaona)
Rafiki:
wewe shuka humo huendi?
Miriam :(
anashusha kioo) wewe nakuja
Rafiki: oh,
kumbe upo na daddy?
Jeremy
:( anashangaa kidogo) daddy???
Miriam:
oh (Kwa Jeremy) wewe sio daddy wewe ni my boyfriend
Jeremy:
daddy si sponser?
Miriam:
baby anakutania jamani
Jeremy:
oh… (Anatabasamu) niliogopa kweli nikaona ee naonwa sponser huku mi
naona nimeshapata mke
(Miriam
na rafiki yake wanaangua kicheko)
Miriam:
jamani ee (anacheka)
Rafiki: Vanessa
Leo yuko wapi?
Miriam:
haji Leo hana hela
Rafiki:
sasa wewe (kwa Miriam) si twende au?
Jeremy:
bye baby (anambusu shavuni)
Miriam:
bye honey
Jeremy:(anatoa
kitita cha pesa na kumkabidhi) enjoy…(anatabasamu)
Rafiki:
ukiitwa sponsa unakataa
Jeremy:ni
wajibu wangu kumtunza nisipomtunza mimi nani atamtunza?
Rafiki:
kweli mwaya wanasema abiria chunga mzigo wako
(Wanacheka)
Miriam:(anakumbuka
kitu) je nikimuita Vanessa nimlipie nitakuwa nimechelewa?
Rafiki:
utakuwa hujachelewa mlipie tu
Miriam:
nitafanya hivyo… (anatoka kwenye gari) bye baby
Jeremy:
bye take care mpenzi wangu (anabusu viganja vyake kisha anampeperushia)
Miriam:(anambusu)
(Jeremy
anaondoka)
Rafiki:
mpenzi wako anakupenda kweli jamani hadi raha
Miriam:
kawaida tu mbona
Rafiki:
nasikia amekununulia gari na yuko mbioni kukununulia nyumba
Miriam:
yaani nyie wambea…wewe nani amekuambia?
Rafiki:
jamani mbona hiyo inasikika sana tu
Miriam:
najua itakuwa Vanessa huyo yaani na yeye ni mdaku
Rafiki:
jamani rafiki yangu mimi si rafiki yako naanzaje kukosa kujua mambo yako?
Miriam: Naila
jamani una mamlaka ya kujua mambo yangu wala sijasema hutakiwi kujua…unatakiwa
kujua sana tu
Naila:(anatabasamu)
ndo hivyo rafiki yangu tunajua kabisa kuwa jamaa ana mpango wa kukuoa na kuishi
na wewe
Miriam:(anacheka)
Naila bado nasoma siwezi kuchanganya hayo mawazo kwanza…
Naila:
ah wewe nae mbona watu kibao wanasoma huku wapo kwenye ndoa zao na wako kawaida
na maisha yanaendelea tu kama kawaida
Miriam:
eti mimi naona ni mbaya hiyo naona haijatulia hata kidogo
Naila:
acha ushamba bwana…unless Kama unataka kuzini…au tayari mmeshaanza?
Miriam:
Jeremy ameniambia kuwa atanisubiri
Naila:
sasa hawezi kukusubiri kwa muda mrefu sana yeye ni mwanamume
Miriam:
najua
Naila:
ndo uolewe kabla haijawa vituko
Miriam:
nitaolewa kwanza tumalize mambo yaliyopo hapo…wewe si unajua Jeremy alikuwa ni
shemeji yangu alikuja nyumbani kwa ajili ya kumuoa dada yangu ndo akatokea
kunipenda mimi kwanza nataka kwanza tumalize utata kwa wazazi kwanza halafu ndo
mipango mingine ifate
Naila:
nakuelewa shoga yangu ila una kazi
Miriam:
acha tu ndugu yangu sijui litakuja kuishaje
Naila:
kila kitu kitakaa vizuri usijali(anatabasamu)
(Dereva
anapanda gari kisha anapiga honi kuita wanafunzi waingie kweye basi kwa ajili
ya kuanza safari)
Naila:
shoga twende tukawahi siti
Miriam:
twende shoga yangu, ila Vanessa hajaja bado ingawa nimempigia simu
Naila:
twende bwana...atatukuta
(Wanaelekea
kupanda basi)
Dereva:
mpo tayari (anaangalia nyuma kisha anawasha gari na kuliondoa)
0 Comments