MUNGU MKUU 28

 

SCENE 28: -

USIKU WAKE: -

(Majira ya saa nne usiku Ariana anafika nyumbani kwao akiwa ni mtu mwenye furaha sana, anapofika anawakuta wazazi wake wana wasiwasi sana)

Ariana: shikamooni

(Wanamuitikia)

Ariana: mbona hamna Amani kuna shida gani?

Mary: Miriam hajarudi mpaka sasa hivi

Ariana :( anacheka) za mwizi arobaini

Keddy: una maana gani?

Ariana: mnaniona mimi ndo mtenda dhambi wa nyumba hii (anajitupa kwenye sofa) kumbe mtenda dhambi yupo amejivika ngozi ya kondoo kumbe ni mbwa mwitu katika kundi la kondoo

Ken: bado sijakuelewa embu ongea vizuri acha kuongea kwa mafumbo sipendi mafumbo yenu

Ariana: Miriam ana mwanaume

Ken:(kwa mshangao) Mwanaume?

Ariana: ndio ana mwanamume

Ken: ameanza lini? na huyo mwanaume ni wa wapi?

Ariana:ni Jeremy

(Wote wanashangaa)

Mary: Mungu wangu huyu mtoto

Ken: Jeremy huyu mchumba wako?

Ariana: ndio…anatoroka chuoni anaenda kwa Jeremy kila siku

Ken:(anashikwa na hasira) Jeremy na Miriam wametusaliti sana hawa watoto…yaani sitaki kumuona Miriam

Mary: shemeji jamani…Miriam hana kosa kila mara Jeremy alikuwa anamlazimisha

Keddy: ina maana ulikuwa unajua?

Mary: nilikuwa nahisi tu dada

Ken: kwanini hukumkataza huyu mwanaume?

Keddy: jamani hawa watoto

Ken: amenitia aibu sana huyu mtoto sikutegemea tena shemeji yake?

Keddy:(anamtuliza mume wake) tulia baba…tulia

Ken: naomba simu yangu mama Ariana...nitamtukana huyu kijana na sitaki tena aje nyumbani kwangu…na mwanangu sitaki amuoe tena

Ariana: baba mimi bado nampenda

Mary:(anashangaa) we Ariana

Ariana: ndio ma mdogo au nikuite mama Miriam

(Ken na keddy wanapigwa butwaa)

Keddy: mama Miriam kivipi?

Ariana:(anacheka) jamani mbona mimi t undo wa kusema ukweli? Leo eeh (kwa mama yake) ndio mama ma mdogo ni mama mzazi wa Miriam

Ken:(anashangaa) Mary kwanini? yaani sielewi ilikuwaje?

Mary:(anabaki mdomo wazi anakosa la kusema)

Keddy: umenisaliti hata mimi Mary jamani? mimi si dada yako? mbona nilikupa nafasi nzuri tu ya kuwa karibu na mimi

Mary:(anabaki kimya)

Ken: yaani ilikuwaje mpaka Miriam akafika mlangoni kwetu na wewe kuwa msaidizi wetu wa kazi?

Keddy: nakumbuka tulikutana na wewe wakati tunatoka kutoa taarifa juu ya kupatikana kwa Miriam

Ken: nakumbuka tulitaka kumgonga

Keddy:(anafikiria kitu Fulani) na ndo maana ulikuwa unampenda sana Miriam...

Mary:(kimya huku machozi yanamtoka kwa fujo)

Keddy: kwanini Mary ulificha yote hayo? ungeniambia basi hata mimi iwe siri yangu tu jamani ukaona umwambie Ariana

Mary: ilitokea tu nimemwambia Ariana hata mimi nilipanga kukuambia wewe

Keddy: ikawaje?

Mary: nikaona sijui nini…nilihisi nikisema mwanangu atakosa sehemu ya kuishi

Keddy: kwahiyo unataka kuniambia kuwa Miriam ni mwanao?

Mary: ndio ni mwanangu dada (Analia)ni mwanangu wa kumzaa mwenyewe…ni maajabu na ukuu wa Mungu alipata familia…

Ken: mambo mengi kwa wakati mmoja mara huyo mwanao amemsaliti mwanangu (anajitupa kwenye sofa kama mtu aliyechoka sana) nimechoka haki ya nani

Ariana:(anacheka chinchini)

Keddy: ukweli huu umenishangaza kwakweli...(anaguna)tumekaa na wewe miaka 18 hata kusema Mary

Mary: nilikuwa nahofia mwanangu angekosa malezi mazuri nisameheni sana nimekosa naombeni mnisamehe (anafuta machozi) naomba muendelee kumpenda mwanangu kama mwanzo

Ariana:(anajisemea moyoni) mwanao hayupo tena duniani yaani hapa wakati wowote kutakuwa na habari kuwa mwanao amekutwa kafa (anacheka moyoni) oh nimeua ndege wawili kwa jiwe moja Mary na Miriam out na hivi huyu Mary alikuwa hana akili sijui ataishije?

Mary: nisameheni…kipindi hicho sikuwa na uwezo wowote wa kumlea mtoto mwanaume aliyenipa mimba hakunitaka tena, nyumbani nilikuwa nimefukuzwa…ningefanya nini…nikaona nije nimuweke hapo nje kwenu na Mungu akawa mwema mkamuona na kumchukua mmelea kama mtoto wenu kabisa…nimekuwa hapa nimeona upendo mnaomuonyesha Miriam…naomba msimtupe nifukuzeni mimi msimfukuze

Ken: Miriam amekosea kuwa na shemeji yake ila pamoja na yote Miriam ni mtoto wetu tumemjua kwa miaka 18 sasa…tunampenda na wala hatutamfukuza pamoja na kutukosea

Mary:(anafuta machozi) asanteni sana Mungu awabariki sana jamani…eeh Mungu unaendelea kuonyesha jinsi ulivyo Mkuu, asanteni sana

Ken: usijali ila kama kuna siri nyingine tuambie mapema…tu

Mary: hakuna siri nyingine shemeji

Keddy:(anatabasamu) usijali… kuwa na amani yataisha au yameisha

Ariana:(anajisemea moyoni) yaani mimi nimekuja kusema hivi ili wazazi wangu wakasirike wamfukuze huyu Mary badala yake wamemsamehe kirahisi hivi(anafyonza)I can’t believe it…yaani kirahisi hata wazazi hawajatia neno sana na wala hawajashangaa... (Anaguna)

Mary: asanteni Sana ndugu zangu kwa kunisamehe kwa hili

Keddy: usijali halikuwa kosa lako ni matatizo tu…

Ken: sasa nyie endeleeni kuongea mimi namfuata Miriam kwa huyo Jeremy

Keddy: ngoja nikusindikize mume wangu

Ken: twende

(Wanaondoka)

Mary :( kwa upole) mwanangu…mbona umeamua kuwaambia wazazi wako kuhusu Miriam?

Ariana :( Kwa ujeuri) niliamua tu kwani kuna tatizo?

Mary: (anatabasamu kidogo) unajua kwanini nilikuambia…? Nia yangu ilikuwa ni hiyohiyo uje uwaambie maana nilishidwa kuwaambia nashukuru umenisaidia sana

Ariana :( anafyonza) embu nitolee upuuzi wako hapa… (Anafyonza) halafu usiniite Mimi mwanao…siwezi kuwa mwanao Mimi huna hadhi ya kuwa mama yangu

Mary :( anatabasamu) sijui umechukua roho ya nani? (kwa upole) usipobadilika una hali mbaya sana mwanangu…sijui utabaki na nani

Ariana: nimekuambia usiniite Mimi mwanao husikii? (Anaondoka kwa hasira)


Post a Comment

0 Comments