SCENE
29: -
USIKU
HUOHUO
NYUMBANI
KWA JEREMY: -
(Ken
na mkewe wanafika nyumbani kwa Jeremy wakiwa wanaonekana kuwa na hasira na hamu
ya kumuona Miriam)
Ken:(anapayuka)
we Miriam
Jeremy:(anashtuka
usingizini) nani tena usiku huu? (ananyanyuka kutoka usingizini anatoka
moja kwa moja mpaka nje) baba?
Ken:
usiniite baba wewe mtoto mimi sio baba yako unaelewa vizuri
Jeremy:
shida nini? (anafikicha macho)
Ken :( Kwa
jazba) Miriam yuko wapi?
Jeremy:
una maana gani? Miriam hayupo hapa hajawahi kuja usiku hata siku moja
Keddy:
baba tunajua mna mahusiano
Jeremy
:( anaangalia chini kwa aibu)
Keddy:
ndo maana tunaomba kama yupo mwambie aje wala hatutafanya chochote kwa mtoto
wetu tutaenda nyumbani tutasahau ujinga wenu na kuendelea na maisha
Jeremy:
mama ni kweli mimi na Miriam tunapendana…na ni kweli tupo kwenye mahusiano ila
hatujafikia hatua ya kukaa pamoja mpaka usiku wa manane na isitoshe mimi na yeye
hatujaongea tangu mchana…
Ken:(anamzaba
kofi) huna haya na adabu unadiriki kusema wazi bila uoga kuwa unatembea na
mwanangu mdogo baada ya kumchumbia binti yangu mkubwa?
Jeremy:
baba hapa tunaongelea moyo baba
Ken:
kelele…nitasahau kuwa wewe ni mtoto wa rafiki yangu…nitasahau kwamba wewe ni
kijana na wa mzee wa kanisa mwenzangu…mnatutia aibu nyie watoto
Jeremy:
baba naomba mtusamehe…ni moyo ndo uliamua kumpenda Miriam, mimi na yeye
tulijikuta tunapendana tu pamoja na kupigana kinyume na hisia hizi
Ken:
unanitia kichefu chefu embu nipe njia niingie mwenyewe nimtafute mwanangu
Jeremy:
kuwa huru baba (anamuachia njia)
Ken:(anaingia
ndani)
Keddy:(kwa
Jeremy) mwanangu...
Jeremy:
naam mama
Keddy:
mmefanya vibaya sana mnajua
Jeremy:
tunaomba msamaha mama...ila kweli kabisa mimi sijui Miriam alipo yaani tangu
mchana namtafuta simpati
Keddy:(anasikitika)
sijui atakuwa wapi
Ken:(anapayuka)
Miriam...wewe Miriam toka kama umejificha wala sitakufanya chochote mwanangu
twende nyumbani
Jeremy:(anaingia
alipo Ken) dad...Miriam hayupo hata upayuke vipi hayupo
Ken:(anamnyooshea
kidole) wewe mtoto najua mwanangu yupo hapa na chochote kitakachotokea kwa
mwanangu wewe ndo utawajibika, naomba kesho nimuone mwanangu...
Jeremy:
baba mimi sijui Miriam alipo
Ken:
nimeshasema (kwa mkewe) twende mke wangu
(Wanaondoka)
Jeremy:(anabaki
ameduwaa)!!!!makubwa haya sasa Miriam kaenda wapi au ndo yupo kwa bwana wake?
ila hamna Miriam hayupo hivyo…kuna namna…au kuna kitu kimejificha hapo
sikielewi vizuri (anaingia chumbani na kuchukua simu yake) embu ngoja
nimpigie simu (anapiga simu)
(Simu
haipatikani)
Jeremy:
yuko wapi huyu mtoto... (anaonekana kuchanganyikiwa) hana tabia za disco
kama dada yake, hanywi pombe, hata kama ndo kaenda kwa bwana ndo alale huko? (anaangalia
simu yake) sasa ni saa sita na dakika ishirini na nane...hajarudi nyumbani
na wala haijulikani yuko wapi…(anaguna)sijui nimpigie Vanessa au Naila
au Ariana? ngoja niwapigie kila mmoja wao kwa wakati wake (anaanza na Vanessa)
(Simu
inaita)
Vanessa:(anapokea)
hello shem
Jeremy:
shem...samahani nimekusumbua
Vanessa:(sauti
ya usingizi) usijali…nambie
Jeremy:
eti Miriam yuko wapi?
Vanessa:(anaguna)
mi mara ya mwisho naongea nae ilikuwa saa 12 aliniambia anaenda kuonana na Ariana...ila
baada ya hapo simu yake ikawa inapokelewa na mwanaume
Jeremy:(anashangaa)
kumbe alienda kuonana na dada yake? wapi?
Vanessa:
mimi aliniambia kwenye sight yao na nyumba yao mpya
Jeremy:
nielekeze maana mwenzio nina msala imejulikana kuwa nina mahusiano nae na
wazazi wake wamekuja hapa…yaani
Vanessa:
muulize Ariana…ndo atakuwa anajua
Jeremy:
nielekeze tu hilo jumba lilipo…yaani nitaenda usiku huu huu bila kupoteza
muda…halafu baada ya hapo Ariana anatakiwa anijibu maswali yangu bila kukosa
Vanessa: anyways ngoja nikuelekeze(anamuelekeza)
Jeremy:
asante shemeji nimepaelewa
Vanesa:
Miriam aliniambia wanatoka mtoko na dada yake na mimi nikajua wamerudi ila
nikashangaa tu baada ya hapo simu yake ikawa inapokelewa na mwanaume amelewa na
sijui alikuwa disco hata sielewi
Jeremy:(anashusha
pumzi) asante sana umeupooza moyo wangu yaani ulikuwa unawaka moto kwa wivu
nilijua mpenzi wangu kanisaliti na mwanaume mwingine
Vanessa:
kuwa na Amani shemeji Miriam anakupenda wewe peke yake...yaani wewe nay eye ni
kitu kimoja usijali mimi naona tu hapo kuna namna maana na dada yake nae ni
mtata
Jeremy:
wewe unahisi atakuwa amemfanya nini?
Vanessa:(anaguna)
yaani siwezi kusema sana ila dada yake ni mtata yule yaani huwa hampendi Miriam
Jeremy:
usiniambie
Vanessa:
ndo nakwambia sasa shemeji tena nina uhakika hata hajafurahia huo uhusiano wenu
Jeremy:(anaguna)
mbona kama alichukulia poa?
Vanessa:
moyoni kwa mtu mbali shemeji na moyo wa mtu kichaka
Jeremy:ni
kweli kabisa… (anashusha pumzi) asante kwa taarifa ubarikiwe…naenda sasa
hivi huko
Vanessa:
unaenda peke yako?
Jeremy:
naenda na mlinzi wangu
Vanessa:na
nyumba unaicha peke yake
Jeremy:
right now...usalama wa Miriam ni wa muhimu kuliko nyumba
Vanessa:ni
kweli kabisa shemeji
Jeremy:
ngoja nikamcheki...nikimpata poa nisipompata tutaanzia hapo...utanisaidia
kumpata
Vanessa:
usijali daima nipo na nyie
Jeremy:
asante shem usiku mwema
Vanessa:
usiache kuniambia yaliyojiri
Jeremy:
usijali
(Wanakata
simu)
Vanessa:(anaendelea
kulala)
Jeremy:(anavaa
nguo maana alikuwa amevaa nguo za kulalia) ni lazima nimtafute mpenzi wangu
sasa hivi...haijalishi nini (anatoka nje akiwa ameshikilia ufunguo wa gari)
iam coming my love (anamuita mlinzi) rafiki…
Mlinzi
:( anatoka mbio)
Jeremy:
naomba unisindikize
Mlinzi:
nyumba tunaichaje (anapanda kwenye gari)
Jeremy
:( anapanda kwenye gari) wewe twende tu usalama wa malkia wangu ni
muhimu kuliko hii nyumba (anawasha gari na kuliondoa)
0 Comments