SCENE
30: -
USIKU
HUO HUO (SAA SABA NA ROBO)
JUMBA
BOVU: -
(Jeremy
na mlinzi wake wanafika katika jumba hilo bovu, wanaangaza kwa kumulika na
tochi kila sehemu)
Mlinzi:
kuna gizi kweli hapa
Jeremy:
hatutaondoka mpaka tumpate Miriam (anatembea tembea na ghafla anakanyaga kitu
anamulika na Tochi) Oh My God…Miriam...
Miriam
:( anahemea kwa mbali)
Jeremy:
baby…wamekufanyaje? Oh My God Asante Sana…Asante sana Vanessa…Miriam…
(Anamkumbatia)
Mlinzi
:( anamuangalia) anaonekana ana hali mbaya kweli unaonaje tumpeleke
hospitali?
Jeremy:
yes…tumpeleke
Miriam
:( haongei na wala hajitambui)
Mlinzi:
wamemuumiza kweli mmh sijui nani kafanya huu unyama
Jeremy
:( anaonyesha uoga) naomba uache kusema hivyo rafiki yangu nisaidie…
(Wanasaidiana
kumbeba Miriam aliyelala na wala hajitambui)
Mlinzi
:( anampima mapigo ya moyo) mbona hana mapigo ya moyo
Jeremy
:( anajikuta anachanganyikiwa) Mungu wangu (anapata nguvu ghafla za
kumbeba kipenzi chake)
Mlinzi:
sasa hapa hospitali gani boss
Jeremy:
tutajua mbele ya safari huko… (Anamuweka Miriam kwenye gari kisha anafunga mlango)
kaa twende hatuna muda
(Wanapanda
gari haraka Jeremy analiondoa gari Hilo, wakiwa ndani ya gari kila mmoja wao
anaonekana kuwa na mawazo sana jinsi ya hali ya Miriam ilivyo mbaya)
Mlinzi
:( anajisemea moyoni) hali ya shemeji mbaya kweli tunafika nae hospitali
kweli?
Jeremy
:( anajisemea moyoni) hali ya mpenzi wangu ni mbaya sana eeh Mungu
naomba usimchukue bado namtaka ndo kwanza hata ndoa hatujafunga…naomba Mungu
wangu unisaidie usimchukue kipenzi changu
(Miriam
bado amelala)
Jeremy
:( amechanganyikiwa Sana)
Mlinzi:
taratibu boss…
(Gari
linaenda kasi Sana na baada ya kutembea kwa muda hatimaye wanafika hospitali)
Jeremy
:( anashuka kwenye gari anambeba miriam anaingia nae ndani ya hospitali)
(Manesi
wamepitiwa na usingizi)
Jeremy :(
anapayauka) jamani naomba mnisaidie Nina dharula jamani nisaidieni
Mlinzi
:( Kwa manesi) nyie…
(Manesi
wanashtuka)
Mlinzi:
tuna mgonjwa hapa Ana hali mbaya sana tunaomba msaada wenu
Manesi
:( wanaamka kwa kujivuta)
Jeremy: (anashikwa
na hasira) inamaana hamuoni nawaita kuwa mpenzi wangu anaumwa sana? mbona
mnajivuta kazi yenu ni nini? nitairipoti hii kwa mabosi wenu
Mia:(mmoja
wa manesi) tusamehee kaka...ngoja niandae chumba naomba unifuate…
Jeremy:(akiwa
bado kambeba Miriam anamfuata Mia kwenye chumba cha wagonjwa mahututi)
Mia:
muweke hapa kaka ngoja nikawaite madaktari…
Jeremy:(anamlaza
Miriam kitandani)
Mia:
tusamehe kaka(anaondoka)
Jeremy:(anamshika
Miriam) usijali mpenzi utapona mama usikate tamaa kila kitu kitakuwa sawa
mama…naomba tu usikate tamaa nifikirie mimi na maisha ambayo tumepanga pamoja
baby naomba usikate tamaa Miriam
Miriam :(
bado hatikisiki wala kuongea wala kufumbua macho hali yake bado ni mbaya sana)
Jeremy
:( anashikwa na hasira sana) hawa madaktari wako wapi utasema tumekuja
kuomba msaada…
(Madaktari
na manesi wanaingia)
Jacob:(daktari
mkuu) ngoja nimuone mgonjwa (anamuangalia Miriam) oh mgonjwa hali
yake sio nzuri… (kwa manesi na madaktari) naomba tumhamishe haraka sana
(kwa Jeremy) kijana naomba utoke tufanye kazi yetu
Jeremy
:( anamuangalia Miriam) sawa dokta naomba mmuokoe mpenzi wangu akipatwa
chochote sitaweza kuishi
Jacob:
usijali tutajitahidi kufanya kazi yetu…na Mungu atusaidie
Jeremy:
najua Mungu ni mkuu atatenda miujiza yake… (Anatoka nje na kuwaacha
madaktari na manesi wafanye kazi yao)
Mlinzi
:( anamjia) boss vipi?
Jeremy
:( anatikisa kichwa) sijui tu…ngoja nimpigie mama na baba yangu simu
sina mtu yeyote wa kumwambia shida yangu hii… (Anachukua simu anabonyeza
namba ya baba yake)
(Simu
inaita)
Baba :(
anashtuka kutoka usingizini) nani tena usiku wa manane?
Mama :( anashtuka
anakaa maana alikuwa amelala) labda Jeremy…embu pokea...
Baba :( anaangalia
kwenya kioo cha simu) hata hivyo ni yeye (anapokea) baba yangu nini
usiku baba
Jeremy
:( Analia) baba
Baba :( anapatwa
na wasiwasi) nini wewe?
Jeremy:
nipo hospitali...
Baba:
kwanini? Una shida gani?
Jeremy:
Miriam amepigwa sana ameumia sana hafungui macho haongei wala nini...Yaani hali
yake ni mbaya sana baba
Baba:
Mimi na mama yako tunakuja tuambie ni hospitali gani mwanangu halafu wapigie
wazazi wa Miriam
Jeremy
:( anawaelekeza)
Baba:
nimepaelewa…tunakuja baba usijali tupo pamoja mwanangu
(Wanakata
simu)
Jeremy
:( anabonyeza namba za Mary)
(Simu
inaita)
Mary :( anashtuka)
nani tena? (Anaangalia kioo cha simu yake) Jeremy ananipigia usiku huu
kuna nini? (Anapokea) baba?
Jeremy:
ma mdogo…Miriam
Mary :( anashtuka)
mwanangu amefanya nini mbona unalia
Jeremy:
ana hali mbaya Sana yupo hospitali
Mary:
amefanyaje embu ngoja nakuja nielekeze nakuja sasa hivi
Jeremy :(
anamuelekeza)
Mary:
nakuja ngoja niwaamshe tunakuja usijali baba subiri hapohapo tunakuja… (Anakata
simu, anavaa nguo kisha anatoka anaelekea sebuleni) inabidi niwaamshe najua
muda umeenda Sana ila sina budi (anaangalia saa ukutani) karibia saa
kumi alfajiri (anaenda kugonga mlango wa Ariana)
Ariana
:( anaamka) ah nani ananisumbua (Anafyonza)
Mary :( anagonga
mlango wa Ken na mkewe)
Keddy :(
anatoka) nini shida?
Mary:
Miriam amepatikana
Ken :( anasikia
anakuja haraka) yuko wapi?
Mary:
hospitali
Ken: twendeni
si mnapajua?
Ariana
:( anatoka) kuna nini?
Ken:
twendeni hospitali
(Wanaondoka)
0 Comments