MUNGU MKUU 31


 

SCENE 31: -

 (Ken, keddy, ariana na Mary wanafika hospitalini wanamkuta Jeremy amejiinamia huku anaonekana kuwa na mawazo mengi sana macho yake yamevimba sana kwasababu ya usingizi na kulia)

Mary: Jeremy

Jeremy :( anamkumbatia) ma mdogo (analia)

Mary: basi usilie tena, umeshalia Sana

Ariana: (anachukia kuona Jeremy Analia)

Ken:(anamkumbatia Jeremy) nisamehe mwanangu…nilichukia sana ingawa bado tunatakiwa kuwa na mazungumzo

Keddy: baba Ariana haya sio ya kuongea sasa hivi

Ken: najua

Mary: ilikuwaje umemkuta wapi?

Jeremy: kwenye jumba Fulani (anamuangalia Ariana) bovu…

Keddy: Mungu wangu natumaini hawajamfanya vitu vya ajabu mwanangu

Ariana :( anachukia Sana huku anajisemea moyoni) eti mwanangu (anafyonza) ovyooo (anaendelea kujisemea moyoni) sijui amepataje bahati ya kupona si angekufa tu mshenzi huyu yaani namchukia kuliko hata dunia inavyojua

Jeremy :( Kwa Keddy) uzuri amepigwa Tu... Ameumia tumboni na amepata majereha mengi sana kichwani

Mary :( Analia)

Ken :( Kwa Mary) usilie Mungu ni mkuu ameumia kidogo tu

Keddy: kwani madaktari wanasemaje?

Jeremy: hawajatoka

Ariana: pole unaonekana umeumia Sana

Jeremy: wewe hujaumia?

Ariana :( anajichekesha) unaonekana umeumia kuliko sisi ndugu zake

Keddy: huu sio wakati wa kutupiana vijembe

Ariana: simtupii mtu yeyote kijembe

Ken: acheni bwana sipendi kelele

Mary :( Kwa Jeremy) upo peke yako?

Jeremy: nilikuwa na mlinzi wangu akaondoka sasa nipo na wazazi wangu

Ken: wako wapi?

Jeremy: wapo nje...

Ken: oh, jamani wana moyo mzuri Sana…

Keddy: nataka kujua Miriam anaendeleaje

Jeremy: haturuhusiwi kwenda…nimeomba mara nyingi Sana ila wanasema nitulie tu

Ken: oh

(Wanakaa)

Ariana :( anamuangalia Jeremy Kwa hasira)

Mary: umesema ulimpataje?

Jeremy :( anajisemea moyoni) nikisema walienda kuonana na Ariana itakuwa msala kwa Ariana sasa nisemeje?

Keddy: baba, Mary anakuuliza kitu

Jeremy: (anashikwa na kigugumizi)

Keddy: vipi?

Jeremy: baba alipokuja Jana usiku akaniambia kuwa Miriam haonekani…kama ilivyojulikana mimi na Miriam tuna…

Ken: tunaelewa...Acha stori nyingi endelea kusema ulimpata wapi?

Ariana :( anajisemea moyoni) eti tunaelewa...Yaani hapa Mimi hawanifikirii kabisa Jeremy alikuwa mchumba wangu amechukuliwa na Miriam kila mtu anaelewa? (Anasikitika) huu ni ujinga hawa watu wananizingua tu nitaondoka muda sio mrefu

Mary: wewe Jeremy…endelea

Jeremy: nikampigia Vanessa akasema kuwa walienda kuangalia kazi Fulani naona huko ndo yakampata hayo makubwa

Keddy: dah…maana Jana akili ilikuwa haitulii kabisa…namfahamu sana mwanangu hana tabia za ajabu za kunitia aibu

Jeremy: namjua pia

Ariana :( anajisemea moyoni) huu ni upuuzi kila mtu anamsifu Miriam utasema ni malaika

(Wazazi wa Jeremy wanakuja walipo)

Ken :( Kwa baba Jeremy) oh David

David: Kennedy

(Wanakumbatiana)

Ken: pole bwana

David: pole pia

Ken: ila Mungu amedhihirisha ukuu wake naona mambo sio mabaya sana

David:ni kweli…daktari amesema kuwa hali aliyonayo sasa hivi sio hali aliyokuja nayo

Mary :( ananyanyua mikono juu) Asante Jehovah

Mama Jeremy :( kwa Keddy) mama Ariana

Keddy: Mama Jeremy…za siku nyingi?

Mama Jeremy: nzuri

(Wanakumbatiana)

Mama Jeremy :( anamuangalia Ariana)

Ariana: shikamoo mama, (Kwa baba Jeremy) shikamoo baba

(Wanaitikia)

Ken: tuna mazungumzo ngoja hili lipite

David: Ken nini tena?

Ken: tutaongea

Jeremy :( anamuangalia baba yake chinichini)

David :( anajisemea moyoni) nimeshajua…tatizo nini

Ken: Kwa sasa tujikite kujua hali ya Miriam

David: kabisa

Ken: ILA tusisahau kuwa tutakuwa na kikao cha dharula baada ya hili

David: haina shida ndugu yangu

Jacob :( anatoka chumba alichokuwepo Miriam)

Jeremy: dokta…

Jacob :( anamshika Jeremy bega) relax my friend...Mgonjwa amefumbua macho Kwa mara ya kwanza tangu amefikishwa mahali hapa (anatulia kidogo) naweza kusema huyu binti ana Mungu wake pamoja na kunyongwa sana…ameweza kuwa sawa

Ariana :( anachukia Sana)

Mary: Mungu ni mkuu jamani

(Wazee waliopo hapo wanakumbatiana kwa furaha)

Ariana :( anaonekana kukasirishwa na yote haya)

Jeremy :( anafurahi Sana) tunaomba tumuone

Daktari: anahitaji kulala maana pamoja ana kwamba alikuwa amefumba macho alikuwa hajalala amechoka, mtamuona kesho asubuhi (anatabasamu kisha anaondoka)

(Wanabaki wanamshukuru Mungu kwa muujiza huo)

Ariana:(anakasirishwa na ujumbe ule)

Post a Comment

0 Comments