MUNGU MKUU 32


 

SCENE 32: -

KESHO YAKE ASUBUHI: -

 (Ariana anaingia chumba alichopo Miriam, anamkuta bado kalala)

Ariana: lione…limelala kwa amani wakati mimi sina hata raha sina hata hamu ya kula

Miriam :( anaamka)

Ariana: sijui huwa unampa nini Mungu maana hii ni mara ya tatu unanusurika…

Miriam :( kimya maana hana uwezo wa kuongea kwasababu ya maumivu ya koo)

Ariana: unanitolea macho...ndio mara tatu mara ya kwanza nilikutupa wakati upo mdogo wakakutafuta ukapatikana, mara ya pili ajali iliyoua wanafunzi wengi ukanusurika ukawa haupo na mara ya tatu ni hii...Mara zote nimefanya mimi kasoro hiyo ya gari ila niliiombea

Miriam :( anamuangalia akiwa bado kimya)

Ariana: I hate you so much wewe Ni sababu ya huzuni yangu…nakuchukia Miriam nakuchukia Sana wewe na mama yako nawachukia wote

Miriam :( anamuangalia kimya)

Ariana: anyways, usifurahi kuwa sasa limepita Hilo…bado ndo kwanza mwanzo huu…welcome to hell my stupid sister (anacheka Kwa kejeli)

Jeremy :( anakuja ghafla)

Ariana :( anajifanya kumuweka vizuri Miriam) Shem

Jeremy: nilikuwa nakutafuta

Ariana: Mimi?

Jeremy: ndio…wewe Shem

Ariana: Mimi hapa sasa umenikuta

Jeremy: najua kuwa wewe ndo ulikuwa na Miriam mara ya mwisho

Ariana :( anashangaa Kwa kutoa macho mithili ya mjusi amebanwa na mlango)

Jeremy: unashangaa? Kumbe wewe ni mnafki ee unajifanya unampenda Miriam kumbe ndo adui yake mkubwa…kweli kikulacho ki nguoni mwako…sikutegemea

Ariana: nani amekuambia?

Jeremy: unataka kubisha?

Ariana: naweza kuwa ni wa mwisho kuonana nae ila nisiwe ndo niliyemdhuru

Jeremy: oh, comeon Ariana…mara ya kwanza nilikuwa nahisi naona vibaya maana sio kwa kumuangalia vibaya vile mdogo wako…nilihisi humpendi ila sasa nina uhakika kuwa humpendi na utafanya kila uwezalo kumdhuru

Ariana: sisi ni watoto tunaofatana ni kawaida kukasirikiana kila mara

Jeremy: najua ukweli juu ya familia yako nimewasikia wazazi wako wanaongelea…Miriam ni mtoto wa ma mdogo

 Mary

Ariana: kweli? Hata sikujua

Jeremy: ona unavyodanganya najua wewe ndo umewaambia maana nimewasikia wanamgombeza ma mdogo kuwa kwanini hakuwaambia zamani mpaka wewe ukawaambia

Ariana: (anashusha pumzi kisha anajichekesha) sawa nakubali yote nisamehe sasa

Jeremy: ulichomfanyia Miriam sio kizuri hata kidogo natamani kukusamehe nashindwa

Ariana: nisamehe na ninaomba usimuambie mtu yeyote kuwa mimi na Miriam tulikuwa pamoja ule usiku

Jeremy: nitakusamehe ila naomba uniambie kwa mdomo wako kuwa wewe ndo umesababisha haya kwa mdogo wako

Ariana :( anashusha pumzi) unanirekodi

Jeremy: sina hiyo tabia na pia nakupa neno langu kuwa sitamwambia mtu chochote hii itakuwa ni siri yetu sisi watatu

Ariana: sikwambii kitu Jeremy

Jeremy: hata usiniponiambia najua kuwa ilikuwa ni wewe ila sijui ni kwanini

Ariana :( kimya)

(Ken na polisi wanaingia)

Ken :( kwa Miriam) mama unaendeleaje mwanangu?

Miriam :( anatabasamu)

Mmoja wa polisi: huyu yuko poa mpaka anatabasamu (anacheka)

(Wote waliopo wanacheka kidogo)

Ken: najua bado koo linauma nimekuja na karatasi utuambie watu waliokufanyia unyama huo waandike kwenye karatasi

Ariana :( anaanza kuogopa)

Jeremy :( anamuangalia Ariana)

Polisi 2: uliwaona waliokupiga?

Miriam :( Kwa kuhangaika anaandika ndio)

Ken: unawajua?

Miriam :( anaandika hapana)

Polisi1 :( anashusha pumzi) duh kazi basi sawa wewe pumzika tutaendelea kuwasiliana… (Kwa Ken) mzee acha sie twende tutakuja tena

Ken: haya ngoja nikutoe…

(Wanatoka)

Jeremy :( Kwa Ariana) mdogo wako ana kupenda Sana

Ariana :( anafyonza moyoni)

Jeremy: Ariana please acha hizo Kama ni umechukia kuhusu huu uhusiano tulikuuliza mapema ukaonekana kuridhika sasa mbona inaonekana kuwa inakuumiza sana

Ariana: nani amekuambia ni kwasababu ya wewe?

Jeremy :( anamuangalia usoni bila kumwambia chochote)

Ariana: who do you think you are?

Jeremy: unapaniki

Ariana: wewe ndo umeanza so chukua hiyo

Jeremy :( anatikisa kichwa Kama kusikitika)

Ariana: usijipandishe kijana

Jeremy: sawa...Nadhani Kama ni hivyo sitasikia tena kuwa umemfanyia chochote mpenzi wangu

Ariana: mtajua wenyewe kwanza mnaendana wote hamna akili

Jeremy: sawa…nafurahi kuona na kusikia kuwa umetutema sasa tutakuwa vizuri hakuna shida…naombea tu hicho kikao cha dharula kitatupa ruhusa ya kupendana kwa amani bila kujificha

Ariana: mtajua wenyewe

Jeremy: unajifanya una majibu…huku una msala

Ariana: unataka nikutetemekee?

Jeremy: nitawaambia kila kitu

Ariana: nenda kawaambie wote wapo pale

Jeremy: Do not be stupid Ariana

Ariana: wewe ndo usiwe mjinga

Jeremy: una maana gani? Je natakiwa kuwa makini kwamba unaweza kumuua mpenzi wangu wakati wowote?

Ariana: nimuue wa nini na nani amekuambia kuwa nilimpiga mimi usichukulie kunyamaza kwangu ndo nimekubali?

Jeremy: iam watching you Ariana

Ariana :( anaondoka Kwa hasira) nimefanya nini kwanini nimegombana na Jeremy huku natakiwa kupatana nae ili siku wakiachana na huyu Malaya nitapata nafasi nzuri ya kuwa nae…nitamuomba msamaha

Jeremy :( Kwa Miriam) dada yako ni mtu hatari sana…tuwe makini sana

Miriam :( hajibu kitu)

Post a Comment

0 Comments