MUNGU MKUU 33


 

SCENE 33: -

BAADA YA SIKU TATU

NYUMBANI KWA KINA MIRIAM

(SIKU YA KIKAO CHA DHARULA)

 (Miriam yupo nyumbani na hali yake inaonekana kuwa nzuri na afya yake inaendelea kuimarika, amezungukwa na wazazi wa pande zote mbili yaani upande wake na upande wa Jeremy, Jeremy na Vanessa wapo pia)

David: unaendeleaje mama

Miriam :( bado anahangaika kuongea) naendelea—vizuri kiasi baba

Mama Jeremy: vizuri mama…

Miriam :( anatabasamu)

 Ken: nadhani Leo itakuwa siku nzuri ya sisi kuzungumza mambo mawili ambayo yalikuwa siri ila sasa yanajulikana moja ni kuhusu…ingawa natamani sana nisizungumzie ila nimeona nizungumze ili watu wasibaki gizani (anatulia kidogo) jambo la kwanza ni kuhusu ukweli kuhusu kuzaliwa kwa Miriam…

(Watu wanasikiliza Kwa makini sana)

Ken: Miriam ni mwanangu pamoja na yote…

Keddy :( anainamisha kichwa)

Ken: (anamuangalia Miriam) Miriam mwanangu, Kwa moyo mzito Leo naomba nikuambie ukweli wa jinsi ulivyozaliwa

Miriam :( anamsikiliza Kwa makini)

Ken :( anashusha pumzi halafu kwa sauti ya chini anasema ukweli) Miriam sio mtoto wetu wa kuzaa…tulimpata kwa njia ya ajabu

(David na mkewe wanashangaa sana)

Ariana :( anacheka chinichini baada ya kuona wazazi wa Jeremy wameshtuka) Miriam Jeremy kwaheri kwenye uhusiano (anacheka chinichini)

David: aisee yaani hatukujua na wala msingetuambia wala tusingehisi...Kabisa hongereni mmejua kukaa na kitu na kukichukulia vizuri

Mama: nyinyi ni wazazi wazuri sana…hongereni sana

Mary :( anafurahi)

Ken: mama mzazi wa Miriam ni Mary…

David: what? Na mlikuwa mnajua?

Ken: hapana ndo tumejua siku ile Miriam amepotea

Mama Jeremy: oh, Mary hongera kwa kuzaa mtoto mzuri kama Miriam

Ariana:(anachukia sana huku anajisemea moyoni) sasa inakuja ile pointi muhimu ya Jeremy na Miriam tuone kama watakubali(anaguna)pole sana Jeremy na Miriam mmejiona wajanja tuone kama penzi lenu litakubaliwa

Ken: Miriam mbona hujashangaa…? Ulikuwa unajua kuwa Mary ni mama yako? Yaani umepoa hushangai hufanyi chochote vipi mama?

Miriam :( anaongea kwa shida) hamna baba nilikuwa najiuliza kwanini mimi na ma mdogo tunafanana

Keddy: kwahiyo ukahisi kuwa anaweza kuwa mama yako?

Miriam: ndio

Jeremy :( anajisemea moyoni) najua unamzibia Ariana, najua uliambiwa na Ariana

Miriam :( anatabasamu)

Ken: pamoja na hayo ulitakiwa uonyeshe hata kushtuka lakini pia anyways tuachane na hayo baada ya kujua Mary ni mama yako unajisikiaje? Samahani kukuambia hivi wakati huu lakini Miriam sitaki kuendelea kukuficha umeshakuwa mkubwa

Miriam: usijali baba…nakuelewa na kuhusu kujua Mary ni mama yangu sijui cha kufikiria…nikitulia nitakuja na jibu

Mary :( anamshika Miriam kwa upendo)

Jeremy :( amesimama nyuma ya Miriam)

Ken: sawa ingawa nimebaki na maswali naamini hilo tumemaliza la pili…ni kuna kitu hapa sikielewi na wala sikipendi

David: kitu gani?

Ken :( anavuta pumzi) mzee mwenzangu

David: naam…

Ken: mlikuja na posa kumposa Ariana

Ariana :( anajisemea moyoni) enhe…muulize huyu mzee anayejifanya mlokole tena mzee wa kanisa

David:ni kweli kabisa mzee mwenzangu

Ken: sasa mbona leo hii nasikia Jeremy kamgeukia Miriam mnawachezea binti zangu?

Jeremy :( anaingilia) hapana baba...Nampenda Sana Miriam

David: Jeremy acha niongee (Kwa Ken) najua tulikuja na posa ya Ariana lakini njiani mambo yalibadilika

Ken: yalibadilika?

David: ndio…hata sisi tulimwambia Jeremy kuwa hii sio vizuri (anatabasamu kidogo) si unajua mambo ya moyo mzee mwenzangu tulitaka mpaka kumpoteza mtoto wetu…wanapendana sana na kwa niaba ya familia yangu ninaomba msamaha mzee mwenzangu, tusamehe sana

Ariana:(anajisemea moyoni) are you kidding me? yaani ni kosa lakini linachukuliwa kawaida

Mama Jeremy: tuwape nafasi watoto halafu isitoshe Ariana alikuwa sio kwamba kampenda mtoto wetu kumbukeni tulikuwa tunawalazimisha watoto na Mungu ameona hilo ndo maana hajaruhusu Jeremy na Ariana kuendelea

Ariana:(anajisemea moyoni) duh...aisee siamini masikio yangu

David: tuwaache wapendane

Ken: vipi kuhusu mwanangu Ariana

David: hakumpenda Jeremy sio jinsi Miriam anamvyompenda Jeremy

Ken :( Kwa Ariana) eti Ariana unalichukuliaje?

Jeremy :( anaingilia tena) alisema yupo sawa tu haina shida

Ken: eeh kumbe alikuwa anajua

Jeremy: ndio

Ken: vipi kuhusu wewe Miriam Ni kweli unampenda Jeremy

Jeremy :( anamshika mkono) usiogope huu sio wakati wa kuficha kitu mwambie ukweli usiogope

Miriam: ndio baba nampenda Jeremy

Ariana :( anainamisha kichwa) aisee

Ken :( kimya kidogo)

David :( kimya huku anamuangalia Ken chinichini)

Ken: kiukweli sijui nini cha kusema... (Kwa Ariana)

Ariana :( amechukia Sana lakini anapoangaliwa na baba yake anajichekesha)

Ken :( anatabasamu) unasemaje mwanangu

Ariana: Mimi sina shida baba wamependana haw ana kama wanapendana basi hatuna budi kukubaliana na haya yote

Keddy: are you all right Ariana?

Ariana: yeah

(Miriam na Jeremy wanashangaa)

Ariana :( anacheka) jamani mbona mnanishangaa kwani hamjui hata Mimi Nina moyo mzuri?

Mary: hakuna aliyekuhukumu Ariana

Ariana: ila nini? (anacheka kidogo) mbona watu wote wananishangaa

Keddy: tusamehe ila tunafurahi kama umekuwa mtu mzima kukubaliana na hili...

Ariana: sawa mama

Ken: basi sawa kikao chetu kimeisha kwa Amani

(Watu wanashikana mikono kuonyesha Amani na upendo kati ya familia zote mbili. Miriam na Jeremy upande mwingine wanaonekana hawana raha na wanamshangaa Ariana, Ariana anaonyesha furaha na wala chuki)

Miriam :( anajisemea moyoni) nina wasiwasi na dada

Post a Comment

0 Comments