MUNGU MKUU 34


 SCENE 34: -

(Kesho yake asubuhi Ariana amekaa sebuleni anapata kifungua kinywa huku anatazama runinga)

Miriam :( anatokea chumbani anaelekea nje)

Ariana :( anamuita) Miriam?

Miriam :( anarudi) abee dada

Ariana: umenipita bila kunisalimia shida nini?

Miriam: samahani dada

Ariana: usijali (anasimama na kumfuata aliposimama) Miriam bado umechukia niichokufanyia siku ile

Miriam: usijai dada nimeshasahau...Tugange yajayo

Ariana: vizuri mdogo wangu…nisamehe tu dada yako nilifanya bila kufikiria…ila kikubwa naomba usimwambia mama baba wala mama yako...

Miriam: hata usijali hata Jeremy sijamwambia

Ariana: Asante Sana mdogo wangu yaani unanipenda mpaka nafurahi (anatabasamu)

Miriam :( anacheka)

Ariana :( anakaa) njoo ukae na mimi…

Miriam :( anakaa pembeni ya Ariana)

Ariana: Mary ni mama yako

Miriam :( anakaa kimya)

Ariana: umelichukuliaje?

Miriam: sijakaa kuongea nae...

Ariana: ongea nae usipende kukaa Na kinyongo maisha Ni mafupi Sana kaa na mama yako huwezi jua unakufa lini? Au utapata tatizo gani? Lini na saa ngapi? Ongea na mama yako myamalize

Miriam: Ni kweli dada unachosema…nitaongea Na ma mdogo sorry MAMA

Mary :( anawasikia anajikuta anatabasamu mara baada ya kusikia Miriam amemuita mama) mwanangu (anatabasamu)

Miriam: nikitoka chuoni Mimi na yeye tutaongea Na nitamuita mama Kwa mara ya kwanza

Mary :( akiwa bado amesimama mbali nao) Asante mwanangu Kwa miaka mingi nimekuwa nikitamani uniite mama na leo hii nimesikia kwa mara ya kwanza (anafurahi)

Miriam: anyways…acha niende nitaongea Na mama baadae

Ariana: haya bwana…msalimie Shem Jeremy

Miriam :( anacheka) sitaonana nae Leo

Ariana: kwanini?

Miriam: ah nataka animisi (anacheka)

Ariana :( anacheka) anakumisi kila siku na kila saa...Una bahati sana kupata mwanaume anayekupenda kwa dhati hongera mwaya

Miriam: ila najisikia vibaya Sana

Ariana: kwanini?

Miriam: Jeremy alikuona kwanza wewe

Ariana: oh, comeon Jeremy hakuniona aliletwa tu...

Miriam: oh (huku ananyanyuka) jamani acha niende…naenda Kwa Vanessa kwanza ananisubiri kuna kazi ya chuo nataka tuimalize mapema

Ariana: msalimie Vanessa

Miriam :( huku anaondoka) sawa

Mary :( anakuja alipokaa Ariana) Ariana

Ariana: abee ma mdogo…

Mary :( anatabasamu) mlikuwa mnaongea nini na Miriam samahani lakini maana kwa mbali nimesikia maongezi yenu nikahisi labda naota ndo nikaona nikuulize kupata uhakika Zaidi

Ariana: amesema ataongea na wewe na atakuita mama kwa mara ya kwanza

Mary :( anafurahi Sana) kumbe nilisikia vizuri

Ariana: kabisa

Mary: nimefurahi Sana

Ariana: hongera kwa furaha yako…

Mary :( anamuangalia usoni) hata wewe una furaha?

Ariana: ndio Nina furaha nimeona tu niendelee na maisha yangu Jeremy ameshapenda pengine sina budi kukubali

Mary: vizuri Sana mwanangu…huko ndo kukua sasa ukisikia kukua ndo huko

Ariana :( anacheka) ma mdogo bwana

Mary: waache tu wapendane asije kukuumiza zaidi na zaidi unajua Jeremy alikuja hapa akiwa hana hisia na mtu alitaka tu mke huwezi jua labda ndoa yenu ingejaa majanga kila kukicha Mungu hutuepusha na mambo mengi

Ariana: uko sawa kabisa ma mdogo

Mary: acha niende mwanangu…

Ariana: haya mama acha mimi ninywe chai niende ofisini kwa baba

Mary: haya mama (ananyanyuka na kwenda zake)

Ariana :( anapohakikisha Mary ameondoka kabisa ananyanyuka Kwa hasira) watu wote wanaona kuwa mimi na Jeremy tusiwe pamoja na mimi nimekubali ila sijakubali kwa moyo wangu wote nimekubali nikiwa na mipango yangu… (Anacheka) eti waache wapendane kwani Mimi sitakiwi kupendwa? (Anabonyeza namba za mtu Fulani)

(Simu inaita)

Mtu :( anapokea)

Ariana: ule mpango wetu sasa ufanyie kazi hawa watu wananichezea acha niwafurahishe

Mtu :( anacheka)

Ariana: hii itakuwa ni kali ya mwaka

Mtu: asikuambie mtu

Ariana :( anacheka)

Mtu: Ni Bomu la mwaka (anacheka sana)

Ariana: muache Miriam afurahi nitampa mwezi mmoja wa kufurahi baada ya hapo kilio…hawezi kunichukulia mpenzi wangu kizembe halafu nikae kizembe mie

Mtu: nipo tayari kukutumikia Ariana

Ariana: vizuri sana na Asante…sana

(Wanakata simu)

Ariana: Miriam unadhani hata nakupenda? Sikupendi…wazazi wangu wanakupenda wewe kuliko wanavyonipenda Mimi…nimepata mwanaume wa kunituliza nae umemchukua halafu unaamini kuwa nimekubali sijakubali Miriam…Your hell begins now Miriam (anacheka)

Mary :( anakuja ghafla bila kutegemewa) Ariana ndo unachekaje hivyo?

Ariana :( anashikwa na kigugumizi) ma---mdo---

Mary: ah utakuwa umechekeshwa kwenye simu siku hizi kuna mambo mengi kwenye simu, nimeelewa (anacheka)

Ariana :( anashusha pumzi)

Mary: naenda sokoni tutaonana baadae

Ariana: hata Mimi naondoka

Mary: sawa (anatoka)

Ariana: yaani pona pona yangu ningekoma leo (anabeba mkoba wake) ngoja niondoke kabla sijazua balaa…niondoke kabla hata siri yangu haijavumbuka (anaondoka)

(Anaacha vyombo hapohapo)

Ariana: atatoa dada wa kazi au Mary mama Miriam... (Anaondoka)

(Mazingira yamekaa vibaya Sana vyombo vimebaki katika mazingira ya uchafu Sana

Post a Comment

0 Comments