MUNGU MKUU 35


 

SCENE 35: -

(Jioni nyingine iliyo tulivu mbele ya macho ya viumbe vyote vile vinavyoonekana na visivyoonekana, Miriam na mpenzi wake (Jeremy) wamekaa sehemu tulivu wakijivinjari na kutuliza akili zao)

Miriam:(anakunywa kinywaji chake)

Jeremy:(anakunywa juisi yake huku macho yake yakimuangalia mpenzi wake)

Miriam:(anaweka glasi chini baada ya kunywa kinywaji chake)

Jeremy:(anaweka glasi mezani pia) aah

Miriam: nini tena?

Jeremy: wala… (anaangaza macho yake katika eneo hilo zuri na la kuvutia) napapenda hapa…ni pazuri na pia ni pazuri Zaidi ukiwepo hapa

Miriam:(anacheka kidogo)

Jeremy: asante Miriam kwa kuja maishani mwangu…

Miriam: ilikuwa ni mtihani lakini nashukuru Mungu dada Ariana amekubaliana na sisi

Jeremy: ila mimi nina mashaka nae

Miriam: oh, comeon Jeremy…dada Ariana amekubali kuwa mimi na wewe tunapendana na hawezi kubadilisha hilo...hata mimi nilikuwa na mashaka nae ila tumezungumza basi nimeona kumbe hana shida dada wa watu

Jeremy: sijui lakini ila Ariana sio mtu mzuri hata kidogo yuko tofauti na wewe unajua?

Miriam: watu tunatofautiana lakini unajua?

Jeremy: nyie mmetofautiana sana…

Miriam: anyways, acha tuachane na hayo tuangalie mambo yetu

Jeremy: sijui kwanini lakini nafsi yangu inaniambia ni lazima nikuonye uwe makini sana na Ariana

Miriam: dada yangu anaweza kuwa ni mtu mwenye hasira sana ila nakuhakikishia kuwa hawezi kunifanyia mimi kitu kibaya

Jeremy: usijifanye umesahau Miriam…Ariana alikuteka na kukutesa sana nimekukuta nusu mfu nusu mzima

Miriam: (anakaa kimya)

Jeremy: usimuamini Ariana she is very evil

Miriam: sawa nakubali kuwa aliniteka na kunitesa sana…ila ameshabadilika sana…amebadilika na ametukubali pia

Jeremy: sio kweli. can’t you see baby…anavyotuangalia kila mara akituona pamoja ni kama kuna kitu anapanga na kibaya sana...

Miriam: hapana Jeremy dada yangu sio mbaya hivyo bwana

Jeremy:(anamuangalia usoni) nikuambieje ili uamini kuwa dada yako sio mtu mzuri na wala hakupendi hata kidogo?

Miriam: naomba nikuulize kitu Jeremy

Jeremy: go ahead…

Miriam: kwanini unamchukia sana dada Ariana?

Jeremy: simchukii…ila simuamini…na sidhani kama hata wewe unatakiwa kumuamini…kwa macho yangu mawili nilimuona anavunja kioo cha gari nililokununulia

Miriam: Jeremy tutagombana naona sasa unataka kunigombanisha na Ariana…Ariana ni dada yangu hata kama hatujazaliwa tumbo moja tumekuwa wote Jeremy…

Jeremy:(anatikisa kichwa ishara ya kusikitika)

Miriam: mimi na Ariana tumekuwa pamoja na baba huwa anatusisitiza kupendana

Jeremy: wewe unampenda ila mwenzio hakupendi…

Miriam: (kwa hasira) enough Jeremy...naona maongezi yetu yataishia kugombana…

Jeremy: utakuwa umependa wewe…ila kwa upande wangu mimi sitaki na wala sitamani kugombana na wewe

Miriam: basi usimseme vibaya dada yangu

Jeremy: Miriam

Miriam: Jeremy please don’t … (anamuonyesha ishara ya kumkatiza) tumekuja kuenjoi na sio kukerana

Jeremy:(ananyamaza huku anamuangalia Miriam kwa huruma)

Miriam:(anabadilisha mada) enhe nambie…tutaenda tulipopanga?

Jeremy:(anaitikia kwa unyonge)

Miriam: jamani ndo unaitika kama hutaki??

Jeremy: hamna kawaida…tu nipo poa mbona?

Miriam:(anakunywa kinywaji chake huku anamuangalia mpenzi wake)

Jeremy: anyways, tutaenda tulipopanga…

Miriam: cheka basi jamani

Jeremy: sijisikii kucheka Miriam

Miriam: kwasababu sijakusikiliza au?

Jeremy: hapana…huo ni uamuzi wako na wala sitaruhusu hili litie doa penzi letu…kuwa na Amani Miriam…ila nataka utambue kuwa sijui kwanini ila nahisi Ariana anapanga jambo baya sana…

Miriam:(anakaa kimya)

Jeremy: my queen naomba unisikilize kesho nitakuhamisha hapo nyumbani uke mbali nae...na pia akikuita sehemu usiende peke yako kama siku ile

Miriam:(anacheka kidogo) Jeremy hivi unadhani kunitoa nyumbani ni jambo rahisi?

Jeremy: najua sio jambo rahisi…okay nitakuoa…nitafunga ndoa na wewe Miriam…

Miriam: Jeremy, mimi nasoma bado

Jeremy: hiyo haina shida Miriam yaani haina shida utaona tu mimi nakuja kutoa mahari siku sio nyingi mpenzi wangu na pia baada ya hapo, tutafunga ndoa haraka iwezekanavyo ili utoke karibu na Ariana

Miriam:(anatikisa kichwa) hata sijui cha kufanya Jeremy…sijui nikumbieje ili ujue kuwa mimi na dada Ariana tumekuwa ni marafiki wakubwa sana...okay nimejaribu kukutoa kimaongezi ila naona hata hubadiliki

Jeremy: kwa vyovyote vile Ariana akikuita sehemu usiende hata kwa nini…nitamuomba dereva wako pia asikupeleke sehemu ambayo Ariana yupo...

Miriam: Jeremy…

Jeremy: nimemaliza…na mama yako ma mdogo Mary nimeshamwambia pia

Miriam: umemwambia wa nini?

Jeremy: kwa ajili ya usalama tu na sio vinginevyo

Miriam: yaani Jeremy…sijui Ariana alikufanya nini?

Jeremy: kwanini?

Miriam: humpendi na sidhani kama hata ana mawazo mabaya juu yangu ila tu kwasababu humpendi ndo unaamua kusema hayo maneno jamani sio vizuri

Jeremy:one day utaniambia kuwa Jeremy ulikuwa unaniambia ukweli

Miriam:(anatabasamu) yaani unaongea uko serious utasema polisi jamani

Jeremy: Miriam sikutanii niamini kuwa dada yako ndo adui wako wa kwanza Zaidi hapo kwenu

Miriam: okay sitaki kukuudhi hivyo nitafanya kama unavyotaka ili nisikuudhi

Jeremy: asante mke wangu…nitamwambia baba na mama kuwa ninataka nikuoe…najua watakubali maana hata wao wanakupenda sana (anacheka kidogo) jamani huwezi kuamini walikuwa wananiambia bora ningekuchumbia wewe

Miriam: waliponiona?

Jeremy: ndio…

Miriam:(anacheka)

Jeremy: unacheka nini?

Miriam:si unanidanganya

(Wanacheka)

Jeremy: nakwambia ukweli Miriam...nakupenda sana lakini wazazi wangu wanakupenda Zaidi

(Wanacheka sana)

Jeremy: kunywa juisi tuondoke bwana usije ukachelewa nyumbani bure

Post a Comment

0 Comments