MUNGU MKUU 36


 

SCENE 36: -

BADA YA SIKU TATU: -

NYUMBANI KWA KINA MIRIAM: -

(Asubuhi mpya na njema na ya kumpendeza Mungu na binadamu, jua linawaka kawaida na upepo mzuri unavuma vizuri na kila mtu anaendelea na shughuli zake. Miriam nae ni mmoja wa watu wanaoendelea na shughuli zao)

Mary:(anamuona Miriam) mwanangu

Miriam: mama…

Mary: dereva wako yupo hapo nje…

Miriam:(anashangaa) makubwa amekuja kufanya nini?

Mary: anasema ametumwa…

Miriam:na Jeremy?

Mary: lazima iwe na yeye au kuna mwingine?

(Wanacheka)

Mary: shoga yangu unapendwa mwayaaa

Ariana:(amesimama pembeni)

Miriam: karibia niwe mke wa mtu

Mary: shoga yangu…niambie huo umbea

Ariana:(anafyonza) pumbavu (anaondoka kwa hasira anachungulia dirishani anamuona dereva) lione lile nalo …(anafyonza)

Miriam:(anapita kuelekea nje)

Ariana:(anamuangalia Miriam) embu lione yaani simpendi mimi huyu mtoto sijui tu…

Miriam:(anamuona Ariana) dada Ariana

Ariana:(anajichekesha) abeee...(anajichekesha)

Miriam: natoka kidogo…shemeji yako kaniita

Ariana:(anajichekesha) haina shida we nenda tu uzuri baba na mama wanajua wewe na Jeremy mnapendana...nenda tu

Miriam: asante sana dada…okay acha mie niende

Ariana: msalimie

Miriam: usijali…. (anamgeukia mama yake mzazi) naenda mama

Mary: tutaonana mwanangu

Ariana:(anamuangalia Miriam kwa chuki sana)

Miriam:(anaondoka kuelekea lilipo gari lake)

Ariana: hesabu siku zako Miriam mwisho wako umefika… (anacheka kwa kejeli)

Dereva:(anamuangalia sana Ariana)

Miriam:(anafika kwenye gari lake anafungua mlango wa gari na kuingia)

Dereva: enhe mrembo embu niambie za kwako?

Miriam: nzuri shoga

Dereva: Vanessa yuko wapi?

Miriam: yupo tu…

Dereva: haonekani (anawasha gari) halafu mbona dada yako anakuangalia vibaya sana?

Miriam: umeongea sana na Jeremy eti eeh

Dereva: hapana sijaongea nae kwanza huwa hatuongei

Miriam: mna mawazo sawa yaani wote mnamuongea vibaya sana dada yangu mna shida gani?

Dereva: sio kumuongea vibaya ni ukweli usiopingwa wifi yaani anakuangalia vibaya sana mpaka inaogopesha

Miriam: wasiwasi wenu tu wenzangu mbona mimi na yeye tunapendana mpaka basi?

Dereva:(anaguna) labda ndo jinsi anavyoangalia…simjui vizuri mimi huwa namuona tu ila mara nyingi nikimuona huwa anakuwa ni mtu wa kukasirika sana sijui huwa ana shida gani...?

Miriam: mnamuwaza tu

Dereva: labda... (anaendesha gari kuondoka mahali hapo)

Miriam: tunaenda wapi?

Dereva: surprise…kuwa mpole utapajua tu shoga re

(Wanacheka)

Miriam: yaani Jeremy ameshakufundisha ujinga jamani…

Dereva: usijali jamani sio kwa ubaya jamani

Miriam: Jeremy yuko wapi?

Dereva: tulia mwanamke…(anashangaa)mbona una haraka wewe?

Miriam: jamani…nisije nikawa napelekwa

Dereva: kwani unadhani naweza kukupeleka mateka…? Jeremy anaweza kunisaka hata mpaka chini ya bahari…

(Wanacheka)

Post a Comment

0 Comments