MUNGU MKUU 37


 

SCENE 37: -

BAADA YA DAKIKA AROBAINI: -

KWENYE NYUMBA MPYA: -

 

(Baada ya dakika arobaini Miriam na dereva wanafika katika nyumba moja kubwa na mpya na pia ni ya kifahari sana)

Miriam:(huku anashuka kwenye gari) shoga yangu mbona nyumba inatamanisha hii ni ya nani? (nafunga mlango wa gari)

Dereva:(anashuka kwenye gari kisha anafunga mlango) ndo usubiri sasa shoga yangu

Miriam: usiniambie hi indo surprise uliyokuwa unaniambia

Jeremy:(amesimama nyuma yao) exactly my love

Miriam:(anashangaa sana) how come? (kwa madeko kidogo) jamani Jeremy sio vizuri

Jeremy:(huku anacheka) do you like it?

Miriam: oh My God iam so happy so very happy… (anajikuta anamkumbatia kwa upendo na furaha)

Jeremy:(anamkumbatia pia) nafurahi kuwa umeifurahia nyumba hii.

Miriam: baada ya harusi tutaishi hapa?

Jeremy: ukiniruhusu sasa hapa mimi sitakuwa baba mwenye nyumba nitakuwa naishi kwako…utaishi na mimi kwenye nyumba yangu ili niwe baba mwenye nyumba

(Wanacheka)

Dereva: unaogopa kuwa chini ya mwanamke?

Jeremy: vibaya sana

Dereva:(anabaki anacheka)

Miriam:(bado naishangaa nyumba ile ya kifahari) oh My God… (anacheka) this is crazy wallahi

Jeremy:(kwa Miriam) naona unashangaa sana unaonaje tukaingia ndani? tuione kwa karibu

Miriam: hapo sasa ndo umenena baba

(Wanaingia ndani)

Miriam: oh my God …hii ni paradiso au?

Dereva: una bahati shoga yangu ndo maana dada yako anakuchukia

Jeremy: (anaguna)

Miriam: jamani embu tusiongelee hayo maana sipendi kusikia dada yangu anasemwa vibaya

(Jeremy na dereva wanaangaliana)

Miriam:(kwa Jeremy) baby asante kwa zawadi hii...

Jeremy:(anakaa kimya)

Miriam:(naendelea kuangaza macho yake kwenye nyumba ile ya kifahari iliyojaa samani za thamani) sasa hapa jikoni ni wapi (anageuka alipo Jeremy)

Jeremy:(amepiga goti moja ameshika kiboksi Fulani mkononi)

Miriam:(anashangaa) Jeremy…mbona umepiga goti? una shida gani?

Jeremy: will you marry me?

Dereva: wow…jamani finally…

Vanessa:(anatokea nje)

Miriam: (amesimama kama sanamu iliyogandishwa)

Vanessa: wewe jibu sio umeganda kama sanamu

Miriam:(analengwa na machozi) lakini …baby mimi sikujua kama utakuwa unamaanisha ulichokuwa unasema, mi nilijua tu unajisemea

Jeremy: ndo nakuomba

(Wazazi wa pande mbili akiwemo Ariana na Mary wanafika mahali hapo)

Miriam:(anawaona anajikuta Analia kwa furaha) jamani mbona mpo hapa? Mmefikaje hapa si nimewaacha nyumbani?

Mary: kuna njia fupi ndo tumetumia

David: hukutaka au?

(Wanacheka)

Ken: jibu basi mwenzio anaumia… (anamsogelea Jeremy)

Miriam: yes…I will marry you my love

(Vigelegele n vifijo vinaendelea mahali hapo)

Ken:(anamsaidia Jeremy kunyanyuka) hongera sana umekuwa mume wa mtu mtarajiwa

Ariana:(anafura na hasira ila anajichekesha akigundua kuwa kuna mtu anamuangalia)

Keddy:(kwa Ariana) dada wa bibi harusi (anacheka)

(Wanacheka)

 Ariana:(anamkumbatia Miriam) hongera mdogo wangu nakuombea kwa Mungu awafikishe kwenye kusudi lako na mpenzi wako

Miriam:(anaangalia pete yake ya thamani)

Ariana:(anaangalia pete ile na roho inamuuma sana)

Miriam: asante sana dada yangu kwa maombi yako

Ariana: usijali mdogo wangu kwetu tupo wawili tu nitakusimamia mpaka siku ya harusi yako

(Vanessa, dereva pamoja na Jeremy wanaangaliana chinichini)

Ariana: (kwa Jeremy) shemeji harusi lini?

Jeremy: kesho…

Araina:(anashangaa) what?

Jeremy: what nini? Hutaki au?

Mma Jeremy:(anacheka) anakutania…

Ariana: nimejua tu kuwa ananitania haiwezi kuwa kesho

Jeremy: kwanini?

Ariana: hatujajiandaa

Jeremy:(anacheka kwa kejeli)

Mary:(kwa Miriam) hongera sana mwanangu umependeza na pete yako mwenyewe jamani Mungu awasaidie mama

Jeremy: amina mama na ninaombea Mungu awapige wale wote watakaokuwa kinyume na sisi na mipango yetu (anamuangalia Ariana chinichini)

Miriam: Jeremy kila mtu ni mwema kwetu hapa mipango yetu itaenda vizuri kwa jina la Yesu…

David: amina

Mama Jeremy:(kwa Jeremy) tuonyesheni basi jikoni

(Wanacheka)

Miriam: asanteni sana jamani nimefurahi sana utasema ni kumbukizi ya siku yangu ya kuzaliwa

 Keddy: you deserve the best my love

Ariana: :(anakasirishwa sana na maneno ya mama yake)

Mary:(anamuangalia Ariana)

Ken: tangazo…jamani mwanagu mkubwa pia amepata mchumba bado hatujamuona ila tunatarajia kumuona hivi karibuni...

(Watu wanafurahia sana)

David: habari njema sana naona tupange harusi siku moja itakuwa nzuri sana

Ken: wazo zuri sana mzee mwenzangu jamani

(Familia zote mbili zinabaki kuwa na Amani na furaha kwa habari ya uchumba wa binti wote wawili)

Post a Comment

0 Comments