MUNGU MKUU 38


 

SCENE 38: -

JUMAMOSI: -

(Familia zote mbili zimekusanyika katika jumba safi la mzee Ken kushuhudia utambulisho wa mchumba wa Ariana, kila mtu anaonekana ana furaha na Amani)

Mary:(anaona magari mawili ya kifahari) wanakuja jamani tujiandae

Keddy: naomba kwa Mungu kila kitu kiende vizuri…Ariana yuko wapi?

Ariana: nipo hapa baba

Jeremy:(amekaa kimya ila ana wasiwasi wa jambo Fulani)

Miriam:(anamuona mchumba wake) mume mbona hivyo?

Jeremy:  kwani vipi mke?

Miriam: una wasiwasi...sana shida nini?

Jeremy: Mungu akulinde tu mke…

Miriam: kwanini?

Jeremy: basi tu

(Wageni wanaingia)

Wenyeji: jamani karibuni sana

Wageni: asante sana

(Kuna furaha na amani inaendelea mahali hapo, familia ya mchumba wa Ariana na familia ya kina Ariana wanapokeana vizuri sana)

Miriam:(ananyanyuka na kuelekea jikoni)

Jeremy:(anataka kumfuata)

David:(anamuona) baba embu saidia wenzio

Jeremy: sawa baba

Miriam:(anaenda jikoni)

(Vinywaji vinaleta na mmoja wa watu wanaoleta vinywaji ni Ariana)

Ken: Ariana mama... (anamuonyesha ishara ya kumuomba aondoke)

Mzee: muache tu aisee anaonekana ana adabu sana…ni mke mzuri sana kijana wetu amejua kuchagua

(Wanacheka)

Jeremy:(anamuangalia sana Ariana)

Ken:(kwa mchumba) kijana unaitwa nani baba?

Mchumba: (kwa heshima) naitwa Colton

Ken: jina zuri sana kijana…

Colton: asante sana baba

Ariana:(anamwagia kinywaji Colton kwa bahati mbaya)

Colton: oh shit…

Ariana:(anamnong’oneza Colton) kazi yetu inaanza sasa hivi…

Ken: pole baba ni bahati mbaya pita nenda bafuni ukajisafishe… (kwa Jeremy) kwanini usikimbie nyumbani ukamletee nguo mwenzio

Jeremy:(kwa heshima) sawa baba… (ananyanyuka anapiga hatua kisha anajisemea moyoni) nimemuona Ariana anamwagia kinywani Colton kwa makusudi kabisa (anaguna)je kuna mpango wowote unaendelea? Colton anaenda bafuni na Miriam yupo jikoni… (anataka kurudi)

David: baba nenda ukamletee mwenzio nguo

Jeremy: sawa baba(anaondoka)

Colton:(anaenda jikoni badala ya bafuni)

Miriam:(anamuona Colton) wewe ndo shemeji yangu?

Colton: ndio (anamuangalia kwa matamanio sana) napenda matako yako (anamshika matako)

Miriam:(anamsukuma na kumpiga kibao) unikome…tena ukome uwe na adabu

Colton: nimesikia kuwa una mtindo wa kuchukua shemeji zako…

Miriam:(kwa hasira) nani amekuambia?

Colton: kila mtu anasema

Miriam: hapana mimi na Jeremy tumependana Sana na familia zetu zilikaa na kuongeaa tukakubaliana na sasa mambo yapo sawa

Colton:(ghafla anamkumbatia) mpenzi jamani umeniacha na kwenda kwa Jeremy kisa sina hela kama yeye?

Miriam:(anahangaika kumsukuma)

Colton:(anamg’ang’ania) nakupenda Miriam mpenzi wangu

(Familia zote mbili zimesimama zinashuhudia tukio hilo)

David: nini hiki Miriam?

Ariana:(anacheka chinichini)

Miriam:(anashangaa)

Colton: naomba niongee jamani…mimi na Miriam ni wapenzi muda mrefu sana alinisaliti nikaamua kumchumbia dada yake...

Ariana:(anajiliza) nina nini mimi kwanini Miriam ananifanyia hivi…?

Miriam: dada…

Ariana:(kwa Colton) kwanini hukuniambia kuwa wewe na Miriam mna mahusiano? kwa mara nyingine nimeumia…mara ya kwanza ilikuwa Jeremy na sasa ni Colton…kwanini lakini?

Ken: siwaelewi…kwamba nini?

Keddy:(amekaa kimya)

Colton:(kwa Ken) mimi na Miriam ni wapenzi…wa muda mrefu...amenisaliti na kuwa ana Jeremy…kisa Jeremy ana pesa…nimeumia sana ndo maana nikaamua kuwa na dada yake

Ariana:(anajiliza)

Ken: kijana…kwanini unasema uongo

Miriam:(Analia sana)

Ken: yaani eti kisa Miriam kakuacha ndo uje umchukue dada yake?

David: inawezekana ndio… labda amefanya kwa hasira

Mama Jeremy: baba Jeremy

David: wewe binti ni mhuni kumbe ee

Ken:(kwa David) mzee mwenzangu…embu ngoja… (kwa Colton) kwa heshima chukua wazazi wako uondoke hapa…sitakuruhusu umuoe mwanangu mana huna msimamo na pia ni muongo

Colton:(anaondoka yeye pamoja na wazee wake)

David: mwanangu hatoweza kumuoa mwanamke anayechanganya wanaume

Keddy: nimemlea Miriam na ninamfahamu…hakuwa na mahusiano na mwanaume mwingine yaani Jeremy ni mwanaume wake wa kwanza…

Ariana:(anakasirika sana)

David: kuna mambo mengine wazazi hatuyafahamu…kuhusu watoto wetu

Mary: tunamjua Miriam sana na sana na hata siku moja hajawahi kufanya jambo la aibu

David:(amekaa kimya)

Jeremy:(anarudi) kuna nini…jamani?

David: tumemkamata mchumba wako na mwanaume mwingine

Jeremy: nilijua tu kuna kitu Ariana anapanga

Ariana: mimi tena?

Jeremy: usidhani mimi mjinga umepanga yule kaka sio mchumba wako umempika tu…

Araina: kwa kuniona siwezi kupendwa au?

Jeremy: muogope Mungu utakufa vibaya sana Ariana… (anamkumbatia mpenzi wake)

David:ni muda wa kuondoka na hatutarudi tena hapa

Jeremy: basi sahau kuwa mimi ni mwanao

Mama Jeremy: jamani nyie

Miriam:(Analia sana)

Ken:(anamkumbatia Miriam) acha kulia tafadhali

Ariana:(anakasirika)

David: mnamuamini sana Miriam ee

Keddy: shemeji ni kwasababu tunamjua Miriam vizuri

David:(anakaa kimya)

Ken:(kwa David) tumshukuru Mungu kwamba kwa pamoja tumemjua na tumejua hila za huyu kijana hakuwa na nia nzuri kwa familia yetu

Jeremy: unadhani ni kwa ajili gani?

Ariana:(anajiliza)

Ken: acha kulia Ariana na umshukuru Mungu kwa kukuepushia hili pia…

Jeremy:(bado amemshika Miriam)

David:(anashusha pumzi) sijui niamini nini…

Mama Jeremy: baba Jeremy…wewe hujaona Miriam alivyokuwa najitahidi kumsukuma? na pia, hata kama walikuwa wapenzi tayari wameachana na Miriam ameamua kumchagua Jeremy…huyo kijan ameingia kuharibu maisha ya hii familia…ni hila za huyo kijana na bahati nzuri tumemjua... (kwa Ariana) pole mwanangu kwa kuwa mhanga wa huyo kijana usijali tumeshamjua…

David: basi sawa tufanye ilikuwa hivyo

Jeremy:(anamuangalia Ariana kwa jicho baya sana)

Ariana:(anajiliza)

David: pole sana mwanangu Ariana na pia Miriam nisamehe mwanangu

Ariana: usijali baba

David: haya tuendelee na mambo mengine

Jeremy:(anamfuta machozi Miriam) pole yameisha mpenzi

Miriam:(anashusha pumzi) asante sana

Ken: jamani nawashukuru sana tulisahau hili jamani

Keddy: kabisa

(Wanarudi sebuleni na kuendelea na shughuli zingine)

Post a Comment

0 Comments