SCENE
39: -
JUMAMOSI
USIKU: -
(Ariana
amekaa chumbani huku nafsi yake inaonekana kuwa imechafuka sana kwa tukio
lililotokea asubuhi yake)
Ariana:it
is not over untili it is over…huyu Miriam asidhani ameshinda kwamba
limeisha…halijaisha na sio kwamba Mungu wake atamsimamia milele kuna kipindi
Mungu wake hatakuwepo
(Simu
yake inaita)
Ariana:(anaipokea)
Colton yaani wewe ni bonge la mshamba…nilikuaminia sana kumbe wewe ni
fala tu (anafyonza)
Colton:
nipe nafasi nyingine Ariana nitakuonyesha naweza kufanyia yaliyo mazuri Zaidi
ya haya uliyoyategemea
Ariana:
sawa naomba unipe ahadi ya kitu Fulani…
Colton:
nini tena?
Ariana:
wewe ni muigizaji mzuri?
Colton:
ndio…sana tu…
Ariana:
kuna jambo la kutisha naenda kumfanyia Miriam hakuna atakaye msaidia hata Mungu
mwenyewe
Mary:(yupo
nyuma yake) unataka kumfayia nini mwanangu?
Ariana:(anashtuka
haraka anakata simu)
Mary:
unaongea na nani? (anachukua simu ya Ariana) Colton?
Ariana:
ndio Colton
Mary:
kwahiyo una mawasiliano na Colton? inamaana umekuwa karibu na Colton…labda
kutakuwa na ukweli juu ya kile alichokuwa anaongea Jeremy…alituambia kua ni
lazima utakuwa umempika Colton…kumbe unamchukia sana Miriam?
Ariana:
sana namchukia tangu alivyokuwa mdogo alikuja kupokonya penzi la wazazi wangu,
kuanzia hapo nikawa kama mtoto baki...nilivumilia ila sasa imekuwa ni too much nimechumbiwa
(anaongea kwa hasira sana) akamchukua mchumba wangu
Mary:
Jeremy alimpenda mwenyewe
Ariana: kwanini
hakukukataa?
Mary:
alijaribu
Ariana:
haikutosha…alimtaka tu
Mary:(anakaa
kimya)
Ariana:
nitamuadhibu Miriam n ukimwambia mtu nitamuua Miriam pamoja na wewe…usinichezee
Mary:
wewe sio muuaji
Ariana:
wazungu wanasema try me
Mary: Ariana
Ariana:(anamuangalia)
umeniletea maziwa?
Mary:(anampa)
Ariana:(hapokei)
kampe mwanao maana anaweza kuyakosa haya…mpe anywe kwa wingi
Mary:
utamfanyaje mwanangu
Ariana:(anamnong’oneza)
siri…(anacheka)unaweza kuondoka nina usingizi sana nataka kulala
Mary:
una roho ya nani we binti?
Ariana:
embu niondokee hapa
Mary:
dhambi ni mbaya sana na unajua hilo
Ariana:
toka chumbani kwangu tafadhali
Mary:(anaondoka)
Ariana:(anamfuata)
ole wako umwambie mtu…nitamuua mwanao na wewe kwa pamoja
Mary:(anamgeukia
anamuanglia kwa unyonge)
Ariana:(anafyonza
kisha anabamiza kwa hasira)
Mary:(anaenda
chumbani kwa Miriam) hodi mwanangu
Miriam:
karibu mama(anamfungulia)karibu mama…
Mary:(anaingia
ndani) hujalala?
Miriam:
naangaalia tamthilia
Mry:(anakaa
pembeni yake) tamthilia gani?
Miriam:
law of the heart inaonyeshwa hapa telemundo
Mary:
inaonekana nzuri sana…
Miriam:
sana
Mary:
kama wewe
(Wanacheka)
Mary:
nimepita kukuambia kuwa nakupenda sana mwanangu na nitafanya kila kitu
kuhakikisha unabaki salama
Miriam:
mama una maana gani?
Mary:
sina maana yoyote…mwanangu (anacheka) kwani siruhusiwi kukuambia maneno
hayo?
Miriam:
jamani…nakupenda mama
(Wanakumbatiana)
0 Comments