MUNGU MKUU 40


 

SCENE 40: -

BAADA YA SIKU TATU: -

(Majira ya saa kumi na mbili jioni, miriam anatoka chuoni baada ya kumaliza kipindi cha mwisho cha siku hiyo, anaongea na simu)

Miriam: leo nimechoka sana unajua…kwahiyo hatutaonana…

Jeremy: poa nitamtuma dereva wako aje akuchukue au unaonaje?

Miriam: afanye haraka…asiniweke

Jeremy: dakika moja tu

Miriam: okay namsubiri

Jeremy: I love you so much my love

Miriam: I love you too…baby

(Wanakata simu)

Miriam:(anasimama akiwa na lengo la kusubiri gari lake lije kumchukua na kumpeleka nyumbani)

(Simu yae inaita)

Miriam:(anapokea) dada Ariana vipi?

Ariana: chukua boda mara moja uje hapa mara moja nina shida naomba msaada wako

Miriam: wapi?

Ariana:(anamuelekeza)

Miriam: haya dada nakuja…

Ariana: fanya haraka mdogo wangu

Miriam:(anaita pikipiki anamuelekeza na mara moja anaondoka mahali hapo)

(Baada ya mwendo wa takribani dakika tatu, hatimaye anafika mahali ambapo ameelekezwa na Ariana)

Miriam:(anashuka kwenye pikipiki anamlipa kisha anamruhusu kuondoka)

Dereva pikipiki:(anaondoka)

Miriam: mbona simuoni tena… (anachukua simu yake kisha anampigia)

(Simu inaita)

Ariana:(anapokea) nakuona

Miriam: njoo basi naona giza linaingia

Ariana: una haraka sana?

Miriam: wewe unanijua kuwa sipendi kukaa nje kwa muda mrefu

Ariana: sasa hivi utapata nilichokuitia

Mtu:(anakuja nyuma ya Miriam na kumziba pua na mdomo kwa dawa ya usingizi)

Miriam:(analegea na kuanguka chini)

Mtu:(ni Colton)

Ariana:(anatokea kutoka kwenye maficho) leo ndo mwisho wako Miriam nitakachokufanyia sijui nani atamuokoa (anacheka)

Colton:(anajimwagia rangi inayofanana na damu, anachukua kisu anakipaka rangi hiyo kisha anamhikisha Miriam, anampaka rangi hiyo kwenye nguo zake)

Ariana: perfect

Colton:(anajilaza pembeni ya Miriam)

Ariana: Miriam ataamka baada ya muda gani?

Colton: kama dakika 15...hivi

Ariana: polisi watakuwa wapo hapa

Colton: nenda sasa

Ariana: this time, naomba usiniangushe hata kidogo sawa ee

Colton: usijali haya nenda…

Ariana: nawapigia simu jifanye umekufa …baada ya hapa tutaonana tena nitakupeleka mbali nitakupa pesa nyingi sana Colton hutaamini macho yako

Colton: asante sana

Ariana: poa usiniangushe…(anaondoka)

Colton:(anajilaza na kujifanya kuwa mfu)

Ariana:(anachukua simu nyingine tofauti na yake na kupiga simu polisi) hello kituo cha polisi?

sauti: ndio karibu tukusaidie…

Ariana: kuna mauaji yametokea(anawaelekeza)mwanamke Fulani amemuua mtu hapa sijuini kwanini njooni haraka kwenye eneo la tukio nimeshawaelekeza

Sauti: asante kwa taarifa...tunakuja muda sio mrefu

Ariana: asante… (anakata simu anamgeukia Miriam)

Miriam:(bado yupo kwenye usingizi mzito sana)

Ariana: umekwisha Miriam (anacheka kisha anaondoka zake)

Colton:(amejikausha kama mtu aliyekufa kweli)

Post a Comment

0 Comments