MUNGU MKUU 41


 

SCENE 41: -

BAADA YA DAKIKA 15: -

JIONI HIYOHIYO: -

(Miriam anazinduka kutoka kwenye usingizi mzito aliokuwa amelala baada ya kuleweshwa, anajishangaa kuona ametapakaa damu)

Miriam: jamani hii damu vipi...na hiki kisu jamani? (anashangaa)kumetokea nini hapa? (anaangalia pembeni anamuona Colton) oh God Colton…amekufa? (anajingalia mkononi) nimemuua?

(Polisi wanafika)

Miriam: Mungu wangu polisi?

Polisi: kaa hivyo hivyo ulivyo dada kama hutaki shida

Miriam:(Analia) sijafanya chochote mimi…sijafanya chochote…mimi sijui nilikuja kuonana na dada yangu hapa

Polisi 1:(anamfikia anamfunga pingu kisha anamuamuru kusimama) simama

Miriam:(bila kugoma anasimama)

(Akiongozwa na polisi anapanda gari)

Polisi 2: tayari tumeshaita ambulance litakuja kuubeba mwili wa kijana huyu aliyeuliwa na mwanamke mwenye roho mbaya ona ulivyomuua kikatili

Miriam: sijafaya chochote naapa nieleweni

Polisi: twende kituoni huko ndo utaeleza vizuri kinagaubaga

Miriam:(analia sana) naombeni simu yangu

Polisi 2: ipi?

Miriam: yangu

Polisi 1: haipo…

(Gari la kubeba wagonjwa mahututi linafika mahali hapo, wahusika wanabeba mwili wa Colton na kuuingiza kwenye gari na kuondoka mahali hapo)

Polisi1: kwakuwa wameshaondoka na sisi tuondoke

(Wanaondoka)

Miriam:(Analia sana) naomba niongee na mchumba wangu...

Polisi 1: tukifika huko…

Miriam:(Analia kwa uchungu)

(Baada ya mwendo wa takribani dakika kumi na tano polisi pamoja n miriam wanafika kituo cha polisi kwa ajili ya mahojiano ya awali)

Miriam:(Analia sana)

Polisi1: huachi kulia una shida gani?

Miriam: sijamuua yule mtu haki ya Mungu kwanini hamniamini?

Polisi2: umekutwa eneo la tukio na ulikuwa umeshika kisu leo hii unasema hujaua

Miriam: naapa mbele za Mwenyezi Mungu…. sijamuua (Analia)

Polisi 1: acha kulia sasa…

Miriam: naomba niongee na mchumba wangu

Polisi 2: una dakika mbili tu (anampa simu)

Miriam:(anabonyeza namba za Jeremy kisha anapiga)

(Simu inaita)

Jeremy:(anapokea)

Miriam: Jeremy (Analia)

Jeremy:(anashangaa) Miriam?

Miriam: ndio Jeremy

Jeremy: nimekupigia simu sana Miriam

Miriam: nipo polisi Jeremy…wanasema eti nimeua mtu…

Jeremy: (anashangaa sana) what?? impossible Miriam sa ngapi?

Miriam: jioni…hii Jeremy

Jeremy: jamani...eeh Mungu wangu…ngoja nakuja mke wangu nakuja sasa hivi mama

Miriam:(anakata simu kisha anendelea kulia)

Jeremy: Oh God…ngoja niwapigia kina mzee Ken maana hii ni tatizo… (anaonekana kuchanganyikiwa na habari ile nzito na ya kushtua)

(Simu inaita)

Ken:(anapokea) naam baba upo na mwenzio…?

Jeremy: hapana baba yupo kituo cha polisi

Ken: what? impossible. kafanya nini? Jamani huyu mtoto mbona ana majanga hivi kafanyaje? Embu Jeremy niambie mbona unanichanganya?

Jeremy: hata mimi sijajua baba mimi mtanikuta kituoni (anakata simu)

Ken:(anashangaa) oh my God… (anabaki ameduwaa)

Post a Comment

0 Comments