SCENE
42: -
USIKU
HUO HUO
NYUMBANI
KWA MZEE KEN: -
(Mzee
Ken anagonga mlango wa Ariana, anaonekana kuchanganyikiwa kwa habari ile ya
kushangaza na kusikitisha)
Ken:(anagonga
mlango)
Ariana:(anajifanya
kutoka kwenye usingizi mzito)
Ken:
umelala mapema sana leo kwanini?
Ariana:
nilikuwa najisikia vibaya sana…nimelala tangu saa kumi…
Ken:
anyways tuna tatizo
Ariana:(anajisemea
moyoni) kumekucha (anajichekea moyoni)
Ken:
mdogo wako yupo kituo…cha polisi sijui amefanya nini…
Ariana:
nani amekuambia?
Ken:
Jeremy
Ariana:
aisee…atakuwa amefanya nini?
Ken:
sijui…nimeshawaambia mama yako na mama yako mdogo wananisubiri nje kwenye gari
nimekuja kukuamsha tuondoke mdogo wako anatuhitaji
Ariana:
sawa baba…ngoja nivae
Ken:
usichelewe
Ariana:(anaingia
ndani) mambo yamekuwa mambo…(anafyonza)alidhani ameniweza kumbe
kajiweza mwenyewe mjinga huyu…na ataozea jela mshenzi yule (anavaa)
Ken:(akiwa
nje ya chumba kile) Ariana bado…
Ariana:
nakuja dad… (anatoka nje) haya twende
(Wanatoka
nje walipo Keddy na Mary)
Ken:
haya jamani tunaweza kwenda (anapanda kwenye gari kisha anawasha gari)
Mary:(anasali
moyoni) Mungu mwanangu namuweka mikononi mwako wewe ni Mungu mkuu tenda
miujiza tangu kale umekuwa ukimtetea mwanangu naomba tena utende miujiza tena
baba…onyesha ukuu wako mfalme naomba mwanangu apone kwenye janga hili sina cha
kuongeza Zaidi
(Safari
inaendelea)
Ariana:(anajisemea
moyoni) maskini wamechanganyikiwa wengine si cha ajabu wanaombea akombolewe (anamuangalia
Mary)
Mary:(anaendelea
kuongea moyoni) najua Ariana ndo kafanya haya ila naamini ukuu wa Mungu ni
wa ajabu na kila kitu kitakuwa sawa kwa jina la Yesu
(Hatimaye
wanafika)
Ken:
tumefika jamani…tuombe sana
Keddy:
yaani hata sielewi amefanya nini...kwani Jeremy kasemaje?
Ken: ndo
tuingie tukasikie
Mary:(anavuta
pumzi ndefu)
Ken:
tulieni kila kitu kitakuwa sawa
(Wanaingia
ndani ya kituo)
Jeremy:(ameshafika
amemkumbatia mpenzi wake)
Ken:(anawafikia)
nambie…za hapa…mama (anamuangalia Miriam)
Miriam:(Macho
yamemvimba kwa kulia sana)
Ken:
pole mama…nambie nini shida kwanini wamekuleta na hizi damu imekuwaje embu
niambie
Miriam:
baba sijaua mimi…
Mary:
kwanini unaongelea kuhusu mauaji...?
Miriam:(kwa
Mary) Colton amekufa…
(Wanashangaa)
Miriam:
dada Ariana aliniita
Ariana:
loh acha uongo…mimi nimerudi nyumbani hata ma mdogo anajua
Keddy:
hata mimi nilimuona na hakutoka
Ariana:(kwa
Miriam) utakuwa unaota
Miriam:
labda, ila kuna mtu alinipigia nimefika pale sijui ikawaje nakuja kuamka nakuta
nimeshika kisu na maiti ya Colton pembeni yangu
Ken:
aisee…mbona moja kwa moja inaonekana ni mchezo?
Miriam:
ndo najaribu kuwaaambia hapa hakuna anayeniamini wameniambia nitalala hapa
Jeremy:(anasikitika
sana)
Miriam:
nafungwa maana nimeambiwa kila ushahidi unaonyesha kuwa mimi ndo nimeua…
Jeremy:
yaani hata sijui nitafanyaje…sijui naanzia wapi kukusaidia yaani hata sielewi
na wewe nakwambiaga usiwe unaenda sehemu peke yako
Miriam:(Analia
sana)
Ken:
basi sio muda wa kulaumiana kwa chochote kwa sasa embu tufikirie tunafanyaje
kwa hili ili tutatue hili tatizo
Jeremy:
tuanzie wapi?
Ken:
tutafute mwanasheria nitampigia kesho family lawyer wetu ili tuanzie hapo tujue
tunafanya nini
Jeremy:
wamekata kumuachia wamesema kuwa atalala hapa na kesi itasikilizwa haraka
iwezekanavyo
Mary:
Mungu wangu
Miriam:(Analia
sana)
Jeremy:
Miriam acha kulia jamani
Miriam:
sijaua mimi jamani nashindwa kuelewa imekuwaje
Polisi
1: muda umeisha naomba muondoke na mtuhumiwa anatakiwa aingie selo
Miriam:(anavua
pete na kumkabidhi Jeremy) nishikie…
Jeremy:(Analia)
Miriam
Miriam:(anaondoka)
Jeremy:
jamani Miriam (anaweka mfukoni pete ile)
Miriam:(anavua
viatu anapewa nguo nyingine)
(Ndugu
zake pamoja na mchumba wake wanabaki wanasikitika)
Mary:(Anazimia)
Miriam:(anageuka
kuwachungulia Analia sana)
Jeremy:(Analia
sana) Miriam mpenzi wangu…kipenzi changu…
Ariana:(anacheka
chini chini huku anajisemea moyoni) kutesa kwa zamu wakati nalia wao
walicheka sasa mimi nacheka wao wanalia haya Maisha bwana (anacheka sana)
(Ken
na mkewe wanamsaidia Mary aliyezimia)
Jeremy:
Mungu naomba uonekane kwenye hili nina uhakika kua mke wangu hajatenda hili…
Ariana:(anajisemea
moyoni) umerudishiwa hiyo pete nitafanya juu chini niivae mimi…
Jeremy:(Analia
sana)
Ken:
twendeni tutarudi kesho…tutarudi na mwanasheria…
Jeremy:
mimi nalala hapa…
Ariana:(anamshika
Jeremy) shemeji…
Jeremy:
embu niache mimi(anamsukuma)
Mary:(anazinduka
baada ya kupepewa na Keddy kwa muda mrefu)
Ken:
twendeni nyumbani
Jeremy:(anajisemea
moyoni) nitalala chini mpaka siku unatoka Miriam (wanaondoka)
0 Comments