MUNGU MKUU 43


 

SCENE 43: -

KESHO YAKE ASUBUHI

KITUO CH POLISI: -

(Ndugu wa Miriam wakiwa pamoja na Jeremy wanafika kituo cha polisi ili wajue maendeleo ya kesi ya Miriam sambamba na wao yupo pia mwanasheria mzuri sana mjini hapo)

Afande 1: karibuni

(Wanaitikia)

Afande 1: niwasaidie nini?

Ken: tumekuja na mwanasheria sisi ni ndugu wa Miriam yule binti…

Afande 2: tunamfahamu huyo binti amekesha anasali tu yaani hajalala…

Jeremy: (anainamisha kichwa)

Ariana: (anajisemea moyoni) umekwisha hakuna atakayekuokoa Miriam (anacheka)

Mary: Mungu wetu ni mkuu…kama alimvusha usiku wa giza na mvua nyingi hakudhulika hata hili atamvusha…mwanangu atakuwa huru

Keddy: kabisa atakuwa huru nina Imani

Mwanasheria: tunaomba tumuone

Afande 2: bila shaka kabisa… (anaenda kumuita na baada ya dakika kadhaa anarudi na Miriam)

Jeremy: (anamuona) oh dear (anamuendea na kumkumbatia)

Ken: yataisha tu kijana wangu…wala usiogope

Ariana: (anafyonza moyoni) jipeni moyo (anatabasamu)

Jeremy: umelalaje?

Miriam: (machozi yanamtoka)

Keddy: usijali mwanangu haki ya Mungu tena utatoka labda sio Mungu tunayemuabudu

Ariana: (anajisemea moyoni) hawa watu wanachekesha sana

Mwanasheria: okay tuanze ili tusipoteze muda maana tuna mambo mengi sana…

(Wanakaa)

Miriam: (anakaa pembeni ya Jeremy)

Jeremy: (anamshika mkono Miriam)

Ariana: (anachukia kuona kitendo kile)

Mwanasheria: hii kesi ngumu maana kila ushahidi unaonyesha kabisa kuwa Miriam ameua

Ariana: (anafurahi sana lakini bila kumuonyesha mtu)

Mwanasheria: lakini kuna tumaini kama mnavyosema Mungu wetu ni mkuu sana na maajabu yake ni ya pekee hakuna wa kupingana nae anapoamua kutupigania

Mary: (Analia sana)

Keddy: Mary acha kulia hili litaisha

Jeremy: Dah (anakuna kichwa)

Mwanasheria: sasa (kwa Miriam) embu niambie ilikuwaje siku ile?

Miriam: (anamuangalia Ariana)

Jeremy: (anagundua) vipi mbona unamuangalia Ariana?

Miriam: dada alinipigia simu

Ariana: relax dogo una wenge najua unayopitia ni mazito tupo hapa kukusaidia ila usiniingize kwenye huo msala tafadhali

Keddy: Ariana alikuwepo nyumbani hakutoka kabisa chumbani kwake

Ariana: (anajisemea moyoni) nilipitia dirishani

Jeremy: lakini pia Miriam sio mjinga kusema hili mara ya pili

Ariana: shemeji…

Ken: haya nyamazeni…

Mwanasheria:  enhe sawa alipokuita?

Miriam: nikaenda ila sikumkuta… nimekaa pale kidogo sijui kilitokea nini ila nilipoamka nikakuta nina damu na kisu mkononi

Mwanasheria: sasa kwani mwili wa marehemu uko wapi?

Afande: (amesimama pembeni yao) umeshazikwa

Mwanasheria: hauwezi kuzikwa kabla haujafanyiwa vipimo yaani fingerprints na kadhalika

Ariana: (anaanza kuogopa)

Afande: ulipimwa…ukakutwa kweli kuna alama ya vidole ya mtuhumiwa

Jeremy: (anashika kichwa)

Miriam: I swear Jeremy sikumgusa yule mtu na kwanini nitake kumuua yule kaka hata simfahamu?

Ariana: acha uongo Miriam alikuwa bwana wako na alikuja akatuambia labda ulichukia alipokuja kukusemea ukaona usije ukapoteza danga lingine ambalo lina pesa Zaidi ukaona umuue una roho mbaya sana

Jeremy: (kwa Hasira huku anamnyooshea kidogo Ariana) Ariana…one more word na nitasahau kama wewe ni shemeji yangu kwanini unaongea uongo wa wazi kabisa

Ariana: kwahiyo mnamuamini sana Miriam?

Ken: hiyo sio kesi tunataka kupata ufumbuzi juu ya hili suala ili tumtoe mwenzetu

Mwanasheria: (anakaa kimya huku kuna kitu anafikiria sana)

Jeremy: something is not right… hapa

Mary: (Anajifuta machozi)

Afande: sasa kwasababu ushahidi umeshakusanywa hatuna budi kumpeleka mahakamani

Jeremy: (anasikitika)

Afande: na adhabu yake ni kunyongwa hadi kufa

Mary: (analia sana) onekana Mungu wa majeshi mwanangu sio muuaji mwanangu mimi hajafanya chochote…Mungu umemvusha kwenye mambo mengi sana mwanangu usiruhusu Mungu mwanangu afe akiwa mdogo hapana Mungu bado namuhitaji mwanangu nataka wajukuu…ukimchukua mwanangu nitaishije mimi Mungu (Analia sana) onekana Mungu wangu jamani baba yangu (analia sana)

Keddy: (anambembeleza Mary) ataonekana tu

Jeremy: Mungu onyesha dunia kuwa wewe ni mkuu

Miriam: (Analia sana)

Ken: (anafuta machozi)

Ariana: (anajisemea moyoni) yaani wanalia kabla ya msiba? Wanachekesha

Mwanasheria: sijawahi kukutana na kesi iliyoshika moyo wangu kama hii…hata mimi naamini kabisa kuwa hujaua… (kwa afande) naweza kupata nguo alizokuwa amevaa?

Miriam: hazionekani…

Mwanasheria: (anashangaa) kuna kitu hakijatulia hapo

Ken: hata mimi naona

Mwansheria: sawa haina shida acha sisi twende tutarudi... (kwa Miriam) tutalimaliza

Miriam: sawa

Jeremy: (anampa chakula) kula…please jitahidi nitakuja tena baadae

Miriam: (kwa unyonge) sawa

Jeremy: I love you

Miriam: me too

Ariana: (anajisemea moyoni) jipeni moyo

Afande: (anamchukua na kumrudisha rumande)

(Ndugu, mwanasheria pamoja na Jeremy wanaondoka huku wote wakiwa wamejaa uchungu na huzuni)

Post a Comment

0 Comments