SCENE
44: -
OFISINI
KWA JEREMY: -
(Jeremy
yupo ofisini kwake amesimama anaanngalia nje kupitia dirisha lake kubwa liliopo
ofisini kwake, anaonekana ana mawazo mengi sana, anajikuta machozi yanamtoka)
Anita: (anaingia)
samahani boss
Jeremy: (anafuta
machozi kisha anageuka) naam
Anita: (anamuangalia
kwa umakini) ulikuwa unalia boss?
Jeremy:
hapana acha tu
Anita:
shida nini?
Jeremy:
kipenzi changu amewekwa ndani Anita
Anita:
Mungu wangu amefanya nini?
Jeremy:
acha tu… (anabadilisha mada) enhe nambie nini shida?
Anita:
kuna watu wawili nadhani mmoja ni rafiki yake wifi na mwingine
Jeremy: oh,
waambie waingie nilikuwa nawasubiri sana
Anita:
sawa (anatoka)
Jeremy:
(anakaa kwenye kiti kuwasubiri waingie)
(Mwanasheria
na Vanessa wanaingia)
Vanessa:
shemeji
Jeremy:
naam shemeji yangu
Vanessa:
shikamoo
Jeremy:
marahaba karibuni
Mwanasheria:
(anampa mkono) habari yako bwana Jeremy
Jeremy:
ah nipo nipo tu nimepoteza furaha kabisa…mpenzi wangu yupo jela
Vanessa:
sijaenda kumuona naona uchungu
Jeremy:
acha tu shemeji
Mwanasheria:
wameshamuamishia jela ni vigumu kuomba dhamana
Jeremy:
(Analia) ningejua ningemtorosha tukaenda kuishi mbali mimi ningekuwa
nakuja tu jioni narudi huko mbali
Mwanasheria:
usikate tamaa na naomba ujikaze halafu ukiwa unaenda usiwe unalia ukilia yeye
atakosa hata nguvu ya kuendelea kuishi she needs us more than ever…
Jeremy: yes, sure hata hivyo nimekuwa nikijikaza sana
kila nikiwa mbele yake
Mwanasheria:
unafanya vyema sana
Jeremy:
(anashusha pumzi) anyways advocate embu niambie kitu hapa kesi imekaaje?
Mwanasheria:
ina utata
Vanessa:
sijaelewa hapo…ina utata kivipi?
Jeremy:
mwili wa marehemu umezikwa kabla ya uchunguzi wowote
Jeremy:
lakini walisema wamefanya uchunguzi
Mwanasheria:
sidhani na kitu kingine nguo alizokuwa amevaa Miriam…zimepotea ghafla
Jeremy:
hata mimi niliona kuna utata hapa kwakweli
Mwansheria:
na kitu kingine ni statement ya Miriam
Jeremy:
ile ya kusema alipigiwa simu na Ariana…
Mwansheria:
tungepata simu ya Miriam
Jeremy:
simu yake imepotea
Mwanasheria:
tunaweza kuomba statement ya simu zake kwa siku hiyo
Jeremy:
yes, tujaribu hapo tukipata tutapata uhakika kuhusu Miriam kuwasiliana na Ariana
Mwanasheria:
exactly…
Vanessa:
Ariana atakuwa amehusika sana kumpeleka Miriam jela
Jeremy:
wewe umenena shemeji yangu
Mwanasheria:
kwanini mnasema hivyo?
Jeremy:
(anaguna) ni muhimu nikuambie…unajua nilikuwa ni kijana
niliyejitosheleza nilikuwa nina biashara za kutosha sio nilikuwa mpaka leo nina
biashara nyingi tu ila sasa sikuwa na mwanamke wa kuniliwaza kwa kifupi mke…
Mwanasheria:
(anasikiliza kwa makini)
Jeremy:
kila nikiangalia nikawa sioni nikaona niombe msaada kwa wazazi wangu wanisaidie
kutafuta mke…ndipo walipoenda katika familia ya mze Ken yaani baba yao kina
Miriam wakaomba uchumba na Ariana…siku naenda kutambulishwa rasmi nikamuona
Miriam…I swear nikampenda sana…sikuchelewa kumueleza hisia zangu na kwa uoga
akawa kigeugeu mara akubali mara akatae…mwisho akakubali tukaanza
mahusiano…mara Ariana akajua...akajifanya ameridhia kumbe ana lake jambo..akawa
anafanya vituko bila sisi kujua mara amteke Miriam mara sijui afanye nini yaani
chuki tu
Mwanasheria:
nimeielewa vyema stori yako kwa maana nyingine Ariana ametengeneza uadui na
Miriam kisa wewe Jeremy
Vanessa:
hapana Miriam sio mtoto wa mzee Ken ila walimchukua na kumlea kama mtoto wao
kabisa sasa hilo hakikumpendeza Ariana hivyo sasa alikuwa anamchukia Miriam
tangu enzi za zamani sio tu kwasababu ya Jeremy kwa maana nyingine Ariana
anaona Miriam anamuibia vitu vyake hivyo anamuona adui
Mwanasheria:
I see
Jeremy:
ndo hivyo…everything makes sense
Mwanasheria:
exactly…sasa (kwa Vanessa) kwa maana nyingine naomba usimame mahakamani
kuwaambia haya unayoniambia sasa hivi…
Vanessa:
sawa mwanasheria nitafanya kila kitu kwa ajili ya rafiki yangu
Mwanasheria:
safi…ni lazima niinue mjadala kuwa Ariana aliwasiliana na Miriam kabla ya tukio
na ana sababu za kutosha za kutaka kumuingiza Miriam kwenye shida ilia pate
upendo anaohisi Miriam kamuibia…
Jeremy:
yes…
Mwansheria:
kila kitu kitaenda sawa lakini Zaidi tunauhitaji ukuu wa Mungu uonekane
Vanessa:
kabisa
Mwanasheria:
huwa mnasali?
Vanessa:
sana
Jeremy:
Miriam amenifundisha kusali mtoto anasali yule kwakweli mahusiano yake na Mungu
ni ya karibu sana
Mwansheria:
ndo maana anampigania nimesikia historia yake kwa kipande kipande lakini
nimeelewa kuwa ni mbarikiwa.
Jeremy:
hata hili litapita ingawa (anaguna)
Mwansheria:
nini?
Jeremy:
inanisumbua sana yaani sijui tu
Mwanasheria:
acha tusubiri
Vanessa:
mnaenda lini tena?
Jeremy:
yaani mimi naenda kila saa…asubuhi naenda mchana naenda na usiku naenda
Vanessa:
ukiwa unaenda niambie twende wote
Jeremy:
haina shida shemeji yangu
Mwanasheria:
okay acha niende nikajiandae na kesi mahakamani itakuwa ngumu lakini najua
tutafanya kitu
Jeremy:
nakutegemea sana
Mwanasheria:
sawa (ananyanyuka anampa mkono Jeremy) basi nikuache uendelee na ujenzi
wa taifa
Jeremy;
siwezi bila kipenzi changu
Mwanasheria:
yataisha tujipe moyo
Jeremy:
kwakweli
Vanessa:
(ananyanyuka) na mimi naondoka ila ukiwa unaenda naomba unipigie ili twende
wote
Jeremy:
bila shaka kabisa
(Wanaondoka
huku Jeremy anabaki akiendelea na kazi zake)

0 Comments