SCENE
58: -
BAADA
YA MIEZI MIWILI
HARUSI
YA COLTON NA VANESSA: -
(hayawi
hayawi mbona yamekuwa walisema haolewi mbona kaolewa, ndugu, jamaa na marafiki
wa Vanessa na Colton wamekusanyika pamoja katika kanisa la Tanzania Assembly of
God kushuhudia muungano wa wawili hao)
Miriam:
(yupo ndani ya gari lililopambwa kwa ajili ya bibi harusi) wow rafiki
yangu hatimaye umekuwa wifi yangu
Vanessa:
nani alidhani kuwa mimi na wewe tungekuja kuwa ndugu kabisa… (anacheka
kidogo) nani alijua kuwa mimi na wewe tungekuja kuwa karibu Zaidi
Miriam:
nakupenda sana Vanessa na Zaidi nashukuru kwa kuja katika maisha ya kaka yangu
Vanessa:
oh, Miriam my dear friend
Miriam:
sio friend ni wifi
(wanacheka
kisha wanakumbatiana)
Miriam:
tutoke dear wasije wakapaniki wakidhani tumegoma kushuka kwenye gari
(wanacheka)
Vanessa:
tushuke shoga yangu asije Colton akaanza kupaniki na hivi anajua
kuchanganyikiwa
(wanacheka)
Miriam:
(anashusha pumzi) it is time
Vanessa:
(anashuka amependeza kuliko kawaida) Miriam watu wako wapi?
Miriam:
(anacheka) wapo ndani wifi wewe ndo malkia unaingia wa mwisho na
utakapoingia kila mmoja atasimama
Vanessa:
my dream came true dear
Miriam:
absolutely (anamsindikiza mpaka mlangoni kisha anamuacha)
Vanessa:
mbona unaniacha?
Miriam:
tulia halafu tabasamu mlango unafunguliwa mlango muda sio mrefu
Vanessa:
(anashusha pumzi)
(mlango
unafunguliwa)
Colton:
(anamuona mkewe mtarajiwa) wow… she is so beautiful
Vanessa:
(anagongesha macho na mumewe mtarajiwa anatabasamu)
Colton:
(anatabasamu)
(watu
wananyanyuka)
Vanessa:
(anaanza kupiga hatua kuelekea alipo mumewe mtarajiwa)
Colton:
(anamsubiri kwa hamu kubwa)
Watu:
(wamesimama wengine wanampiga picha)
Ariana:
(anamuangalia Vanessa) jamani kamependeza kweli yaani
Mary:
wow…amenoga...jamani mtoto
Miriam:
(amekaa pembeni ya baba mtoto wake) wow jamani karafiki kangu
kamependeza sana
Colton:
(anajiweka vizuri kisha anatabasamu)
Vanessa:
(anakaribia kufika alipo mumewe mtarajiwa)
Colton:
I can’t believe she is going to be my wife in few minutes
Ariana:
eeh Mungu hata mimi natamani sana kuolewa natamani sasa na mimi nipate
wangu…najua nilikukejeli ilikuwa ni ujinga tu sasa nakiri ukuu wako naomba
unionyeshe kweli na mimi natamani kuolewa
Vanessa:
(anafika alipo Colton anatabasamu kisha anamshika mkono)
Colton:
(anapanda nae alipo mchungaji)
Vincent:
(anatabasamu) mwanangu
Colton:
(anaongea kwa kunong’ona) umependeza mpenzi wangu
Vanessa:
(anamuangalia kwa aibu) asante
Colton:
(anatabasamu)
Mchungaji:
(kwa utani) kama mmeshamaliza kuchekeana tuendelee na ratiba nyingine
(watu
wanacheka sana)
Colton:
(anacheka pia)
Mchungaji:
embu mfunue isije ukawa unamchekea mke wa mtu mwingine
(wanacheka)
Colton:
(anamfunua) wow
Vanessa:
(anacheka)
Mchungaji:
wow ee (anacheka huku anatikisa Kichwa) mrembo eeh
Colton:
(anacheka) ndio
Mchungaji:
ndo yeye??
Colton:
hakika
Miriam:
(anacheka)
Mchungaji:
basi sawa... (kwa watu) bwana Yesu asifiwe kanisa
Watu:
amina...
Mchungaji:
ndugu zangu leo tumekusanyika hapa kushuhudia muungano kati ya Colton Vincent
Mshana na mwenzake Vanessa Emmanuel Mpejiwa
Watu:
(wanasikiliza kwa makini)
Mchungaji:
(kimya kidogo)
Colton:
(anatabasamu)
Mchungaji:
(kwa Colton) Colton je unamchukua Vanessa Emmanuel Mpejiwa kuwa mke wako
wa ndoa na kwamba utamlinda, kumheshimu na kumpenda siku zako zote za maisha
mpaka pale kifo kitakapowatenganisha?
Colton:
ndio
(watu
wanashangilia)
Mchungaji:
(kwa Vanessa) Vanessa je upo tayari kumchukua Colton Vincent Mshana kuwa
mume wako wa maisha kwamba utamheshimu, na kumpenda siku zote za maisha yenu
mpaka pale kifo kitakapowatenganisha?
Vanessa:
ndio
(watu
wanashangilia)
Mchungaji:
basi kwa ukiri wenu kifuatacho ni zoezi la pete
(watoto
wawili wanaleta pete mmoja anampa Colton na mwingine anampa Vanessa)
Vanessa:
(anaipokea na kukaa nayo)
Colton:
(anafanya hivyo pia)
Mchungaji:
naomba mgeukiane…
(wanafanya
hivyo)
Mchungaji:
nitakuwa nasema maneno unayafatisha…naanza na mwananume…mshike mkono mwenzio na
kusema maneno haya…mwenzangu pokea pete hii
Colton:
(anafata)
Mchungaji:
iwe ishara ya mapendo na uaminifu wangu kwako…
Colton:
(anafata)
Mchungaji:
kwa jina la baba, na la mwana na la roho mtakatifu
Colton:
(anafata huku anamvalisha pete)
Watu:
(wanashangilia baada ya kuona Colton amemvalisha pete kwa ukamilifu)
Mchungaji:
(kwa Vanessa) utafanya kama alivyofanya mwenzio
Vanessa:
(anaitikia)
Mchungaji:
mwenzangu pokea pete hii
Vanessa:
(anarudia maneno yale)
Mchungaji:
iwe ishara ya mapendo na uaminifu wangu kwako…
Vanessa:
(anarudia)
Mchungaji:
kwa jina la baba na la mwana na la roho mtakatifu…
Vanessa:
(anarudia huku anamvalisha pete)
Mchungaji:
safi sasa… alichokiunganisha Mungu mwanadamu asiweze kukitenganisha
(watu
wanashangilia)
Vanessa:
(anamgeukia Miriam kisha anatabasamu)
Miriam:
(anatabasamu) hongereni sana
Mchungaji:
basi ndugu zangu nawatangazia kwenu bwana na Bibi Colton Mshana
(kanisa
linalipuka kwa shangwe na nderemo)
Mchungaji:
(kwa maharusi) naomba mje mnisainie vyeti vya ndoa…hongereni sana
Colton:
(anamkumbatia mkewe)
Mchungaji:
oh, samahanini sikuwaambia mpongezane
(watu
wanacheka)
Vanessa:
(anamkumbatia mumewe)
Miriam:
(anafurahi sana)
Vanessa:
(anatabasamu)
(maharusi
pamojana washenga wao wanasaini vyeti vya ndoa)
Mchungaji:
basi sawa mmekuwa mume na mke kamili
(maharusi
wanawaonyesha watu vyeti vyao vya ndoa)
Watu:
(wanafurahi sana)
Jeremy:
oh, hatimaye wametimiza lengo lao
Miriam:
na sisi Mungu atufanikishie…
Jeremy:
ni miezi miwili tu imebaki mimi na wewe tufunge ndoa mpenzi wangu…
Miriam:
oh, Jeremy wangu baba G wangu nakupenda sana
Jeremy:
mimi Zaidi
(watu wanaendelea kuwapongeza
maharusi kwa kufunga ndoa takatifu, maharusi wana furahi sana, picha nyingi za
ukumbusho zinapigwa na kila mtu anaonekana kuwa na furaha kubwa sana)

0 Comments