I KILLED MY LOVER 1

 


SCENE 1: -

(Ni usiku mmoja mtulivu sana, mwezi angani unang’aa vizuri na kila kitu kina kinaonekena kipo katika utulivu, katika nyumba iliyo na giza kuna mtu anaonekana anaingia ndani kwa mwanaume mmoja ambae anaonekana amelala usingizi fofofo, lakini ghafla yule mtu aliyeingia anamchoma kisu mara kadhaa mwanaume yule aliyekuwa amelala)

Mwanaume :( anashtuka na anajihisi maumivu makali sana) jamani… (Kwakuwa ni giza haoni) we nani?

Mtu :( anaendelea kumchoma kisu)

Mwanaume:(anaishiwa nguvu na kupoteza maisha hapo hapo)

Mtu:(ananyanyuka maana alikuwa amekaa) pumbavu… (anachukua dumu lililokuwa limejaa mafuta ya taa kisha anaanza kuyamwaga sehemu mbalimbali za nyumba ile anafanya hivyo kwa muda na mwisho anawasha kiberiti kisha anatupia halafu yeye anakimbia)

(Nyumba inawaka moto ambao unawashtua majirani waliokuwa bado wako nje)

Mmoja wa majirani: jamani oneni nyumba ya Robert inawaka moto jamani…

Mama mmoja: eeh maskini wa Mungu halafu alikuwa amelala ndani

Jirani mwingine: twendeni tukasaidie kuuzima pengine tunaweza kumuokoa Robert

(Haraka majirani wanakimbilia kwa bwana Robert ili wamuokoe maisha, na kuuzima moto ule)

Mama: kwanini tusiwaite zima moto jamani hivi tutaweza kweli?

Mmoja wa majirani: mama Mgata upo sawa kabisa

Mwingine: tatizo huwa wanachelewa sana embu tujaribu

(Wanaendelea kumwaga maji wengine wanamwaga mchanga na wengine wanapiga simu kwa ajili ya msaada wa zima moto na wengine wanaita majirani wengine)

Mama: sijui kama Robert atakuwa mzima humo ndani huu moto ni mkubwa sana sijui umesababishwa na nini

Jirani: labda umeme…

(Wakati wanaendelea kuhangaika kuuzima moto huo, gari la zima moto linakuja na haraka askari wa zima moto wanaanza kazi yao, wanauzima moto huo kwa muda na hatimaye wanafanikiwa kuuzima. haraka wanaingia ndani kuangalia mtu aliyekuwepo ndani wanatoa mwili uliokuwa tayari umeungua vibaya sana na mtu yule alikuwa ameshafariki dunia)

Mmoja wa askari wa zima moto: tunasikitika kusema huyu mtu ameshafariki dunia…cha kufanya ni nyinyi kutoa taarifa polisi kuwa mtu huyu ameshafariki dunia

(Majirani wanasikitika sana)

Askari zima moto: cha msingi ngoja niite ambulance iupeleke mwili mochwari iili uhifadhiwe huko na kusubiri taratibu nyingine

Mama: yaani tunasikitika sana baba wa watu hakuwa na makuu na mtu alikuwa ni mtu wa watu

Askari:ni mpango wa Mungu

Mama:(Analia sana)

Askari: familia yake iko wapi?

Mama: wapo nchi za nje mke na watoto wake

Askari:(anapiga simu, inaita na hatimaye inapokelewa) ndio kuna mwili wa mtu mmoja umekutwa kwenye tukio la ajali ya moto…tafadhali naomba mje muuchukue ili uhifadhiwe katika chumba cha kuhifadhia maiti

Sauti: sawa nielekeze tunakuja baada ya muda

Askari: nakuandikia meseji sasa hivi

Sauti: sawa na asante sana kwa taarifa 

Askari:(anakata simu kisha anaandika meseji) sasa ni muhimu familia yake ikajua ili ipango ya mazishi ianze

Mama: sawa

Askari: hivyo vingine vitafanywa na mapolisi…sisi kazi yetu tumemaliza...

(Baada ya dakika kama kumi na tano, ambulance inafika mahali pale, haraka wafanyakazi wa hospitali ile wanashuka)

Kijana: jamani habari zenu

Majirani: salama…

Kijana: poleni kwa msiba huu…

Majirani: asante

(Yule kijana pamoja na wenzake wanachukua machela kisha wanabeba mwili wa bwana Robert na kuuweka kwenye ambulance kisha wanaondoka eneo hilo la tukio)

Askari: basi sawa sisi…ngoja na sisi tuondoke poleni sana kwa tukio hili la kutisha

Majirani: asante sana

(Askari wa zima moto na wenzake wanaondoka mahali pale, huku wakiwaacha majirani wakiongea mambo tofauti tofauti)

Mama: yaani nimesikitika sana kifo cha huyu mtu...

Jirani: acha tu mama Neema…embu yafikirie mateso aliyoyapata huyu bwana kabla hajafa…yaani ameungua sana…vidonda mwili mzima…

Mama Neema: yaani acha tu halafu jumba lake limeungua lote lilikuwa bonge la jumba…yaani Hassani nimesikitika mwenzio

Hassan: hunizidi hata kidogo

Jirani mwingine: ndo hivyo kila mmoja wetu ataonja mauti…njia yetu sote hivyo tusikitike jamani

(Wakati huo anakuja binti mmoja mwenye umri kati ya 23 au 24 ni mjamzito kati ya miezi mitano au mine nay eye anaonekana anaishi jirani hapo)

Binti: jamani kuna nini…nimesikia ving’ora vingi sana kuna nini?

Mama Neema: acha tu mdogo wangu…Bw. Robert kafariki kwenye ajali ya moto

Binti: maskini…inauma sana

Mama neema: sasa wewe umekuja juzi tu…sisi tuliyomuona kuanzia ndo anaanza kujenga nyumba yake yaani tumeumia sana

Binti: maskini…hatuna budi kumshukuru Mungu…

Mama Neema: kweli…hivi nimekuona hii ni wiki ya pili si umepanga chumba kimoja humo kwetu…nakuonaga unatoka na kuingia hata sikufahamu jina lako

Binti: naitwa Josephine au Liliana….

Mama Neema: ah!!sawa hilo la kwanza gumu ngoja nikuite Liliana au we unasemaje?

Liliana: sawa tu, ingawa jina nililozaliwa nalo ni Liliana au niite JO...

Mama Neema: sawa...haina shida…

Liliana: sawa najisikia vibaya na ishakuwa usiku sana ngoja nikalale tutaonana kesho asubuhi

Mama: sawa Jo

Liliana:(anaondoka zake)

Mama Neema: jamani mnaonaje na sisi tukapumzike tutaonana kesho asubuhi

(Majirani wanakubaliana na kila mmoja wao anaenda nyumbani kwake maana imeshakuwa usiku sana…wanapoondoka anakuja yule mwanamke aliyemuua Robert na kuchoma nyumba yake, haonekani sura na wala hatambuliki kirahisi ila tu ni mwanamke)

Mwanamke: sasa nafsi yangu imeridhika…wanaume wamekuwa ni watu wa baya sana kwangu… huyu alinichkulia kitu nilichokithamini sana katika Maisha yangu,hicho kitu ni cha thamani sana kwangu kisa mapenzi nilishindwa kumsamehe kabisa huyu alinichukulia dhaifu… alinidharau na kunikejeli nilishindwa kumsamehe Mungu wangu naomba unisamehe kwa hili najua nimekosea sana ila ilibidi nifanye maana alinisumbua sana huyu  mwanaume nimemkomesha (anacheka kidogo) apumzike kwa amani  (bila kuonekana uso anaondoka zake)

Post a Comment

1 Comments

  1. Hello my friends and family,thank you for your love and support,story ya kwanza imeisha nimeanza story mpya tafadhali naomba muendelee kuniunga mkono asanteni na ninawapenda sana

    ReplyDelete