I KILLED MY LOVER 59

 


SCENE 59: -

BAADA YA MIEZI MIWILI: -

HARUSI YA RAPHAEL NA LILIANA: -

(Ni siku nzuri tena iliyopambwa vyema Kwa hali ya hewa nzuri yenye upepo mwanana kutoka bahari ya Hindi, Liliana amekaa katika chumba kidogo cha kubadilishia nguo amevaa gauni la maandalizi (robes) amekaa anaonekana ana mawazo sana lakini Zaidi ana furaha sana)

Liliana: maisha yangu yote nimekaa naiwazia hii siku…siku hii ni ya muhimu sana kwangu…finally naenda kufunga pingu za maisha

Bianca: (anaingia) mama

Liliana: (anamnyanyua na kumuweka kwenye paja lake) mwanangu… (Anambusu) umependeza sana mama yangu

Bianca: (anatabasamu) wewe ndo umependeza

Liliana: muongo mimi hata sijavaa gauni langu

Anna: (anaingia akitokea nje) binamu

Liliana: yes binamu

Anna: hujajiandaa tu yaani huko mumeo anapiga simu kila mara

Liliana: (anacheka) na yeye akae Kwa kutulia jamani

Anna: lazima awe na wasiwasi

Liliana: asijali bwana

Anna: (anakaa kimya huku anamuangalia)

Liliana: (anatabasamu) nini binamu

Anna: historia ya maisha yako ni historia nzuri sna yenye mafunzo mengi

Liliana: oh binamu

Anna: umepitia mengi sana Liliana lakini pamoja na hayo hukuwahi kukata tamaa umesimama na Imani yako mpaka mwisho

Liliana: oh binamu

Anna: leo unaolewa kipenzi yaani nina furaha sana

Liliana: (ananyanyuka na kumkumbatia)

Anna: natamani shangazi na mjomba wangekuwepo au mama na baba yangu au aunt Bianca

Liliana: (machozi yanamtoka)

Anna: usilie Liliana yameisha si umeshasamehe? Yameisha mama

Liliana: yes, yameisha binamu

Bella: (anaingia) jamani bibi harusi hata hajavaa? Na mama mkwe wako anakuja

Liliana: acha aje tu

Lydia: (anasukuma mlango kidogo kasha anachungulia) jamani tunachelewa kanisani (anamuita Bianca) twende tutangulie

Bianca: (anamfuata Lydia na kuondoka nae)

Lydia: fanyeni haraka (anaondoka na Bianca)

Liliana: haya nivalisheni

(Anna na Bella wanamvalisha gauni lile kubwa lenye nakshi kila mahali ama hakika ni gauni la kifahari, baada ya kuhangaika kwa muda wanamaliza kumvalisha)

Anna: haya twendeni

(Wanatoka nje wanakutana na kundi kubwa la kina mama wanaowapokea kwa vifijo na nderemo nyingi)

Liliana: oh My God (anatabasamu)

Anna: kila mtu anaifurahia hii siku Liliana

Liliana: hata Mimi naona

(Wanatembea mpaka katika gari lililopambwa vizuri kabisa maalumu kwa ajili ya siku hii muhimu, wanapanda huku ngoma na tarumbeta zinawafata kwa nyuma)

Liliana: Leo ni siku kubwa sana yaani siamini (anageuka nyuma) ona magari

Bella: usijali hiki ni kidogo mpenzi kanisani ndo kuna raha yote

Liliana: kwanini?

Bella: si ndo alipo mumeo?

Liliana: (anatabasamu kidogo)

(Safari ya kuelekea kanisani kwa ajili ya kushuhudia muungano kati ya Liliana na Raphael)

Liliana: (moyoni) leo ni siku yangu muhimu sana yaani hata sijui nifurahi au nilie natamani wazazi wangu wangekuwepo na Zaidi mwanamke aliyenilea kwa upendo mkubwa kama vile mimi ni mwanae hata yeye natamani angekuwepo angalau akae pembeni yangu ashuhudie umati wa watu ulivyofurahi na mimi (anaguna) ila maisha yamenipitisha (anacheka kidogo) kuanzia kupoteza wazazi wangu mpaka kumpata mama yangu Bianca maisha ya kifahari niliyoish baada ya kuteseka mikononi mwa shangazi yangu mpaka kufikia kumuua hawara yangu baba mzazi wa mume wangu mtarajiwa aisee (anacheka kidogo) kila mtu kuna hadithi mwenyezi Mungu kamuandikia ni jukumu let utu kuipokea kwa Imani kwamba kesho itakuwa sawa au asubuhi itafika halafu mambo yawe sawa

Bella: (anamshtua Liliana) unawaza nini cousin?

Anna: tumefika kanisani

Liliana: (mapigo ya moyo yanamuenda kasi Sana)

Anna: relax hakuna kitakachoharibika not today my cousin

(Mlio wa harusi wa kiitaliano unasikika na watu wanaingia kanisani wakijiandaa kumpokea malkia wa siku hiyo)

Liliana: naona watu wamekaa kunisubiri…

Anna: relax acha sisi tuingie kanisani

Liliana: okay nawakuta huko

Bella: bye all the best

Gabriel: (anakuja) hujambo?

Liliana: sijambo shemeji shikamoo?

Gabriel: marahaba Mimi ndo nimekuja kukuchukua nitakusindikiza mpaka altareni

Liliana: (machozi yanamtoka) Asante Sana shemeji

Gabriel: usijali (anampa mkono) haya taratibu Anza kutembea

Liliana: (anaanza kupiga hatua taratibu)

Gabriel: hongera Sana

Liliana: Asante Sana shemeji

(Mlango unafunguliwa na kila mtu anasimama kumkaribisha malkia wa siku hiyo, malkia ni malkia kweli amependeza sio utani yaani gauni limekaa mahali pake na kila mtu anaushangaa urembo na umbo zuri alilojaaliwa Liliana)

Liliana: (hatua kwa hatua kwa madaha na tabasamu ang’avu anaisogelea altare alipo mchumba wake mpenzi Raphael)

Raphael: (anamuangalia kwa mapenzi makubwa) wow oh my God

Liliana: (anatabasamu akimuangalia mume wake mtarajiwa)

Raphael: beautiful

Liliana: (baada ya hatua kadhaa hatimaye anafika kwa mumewe mtarajiwa)

(Wapendanao hao wanashikana mikono kasha kwa upendo mkubwa wanaangaliana usoni, kisha wananagalia mbele kusikiliza maelekezo ya mchungaji)

Mchungaji: pandeni hapa altareni

Maharusi: (wanapanda)

Mchungaji: (anatoa neno kidogo)

Wageni: (wanaonekana kuwa na furaha sana mwenye kupiga picha tukio lile mwenye kuchukua video yaani kila mmoja na jinsi alivyopenda kuishangilia siku ile ya Liliana na Raphael)

Raphael: (anamng’oneza mkewe mtarajiwa) umependeza sana mke wangu

Liliana: (anatabasamu)

Raphael: Mungu amejua kuumba wewe ni mwanamke mzuri sana

Liliana: (anatabasamu)

Raphael: Mimi ni mwanaume mwenye bahati sana

Liliana: hata Mimi ni mwanamke mwenye bahati sana my love yaani najivunia kuwa wako Raphael

Raphael: (anaibusu mikono ya Liliana)

Mchungaji: (anatania) Kama mmemaliza kunong’onezana tunaweza kuendelea

(Watu wanacheka)

Liliana: (anacheka Kwa aibu)

Mchungaji: (anaanza ibada ya ndoa, baada ya kuongea maneno machache anaziita Pete)

Bianca: (akiwa amependeza Sana analeta Pete za ndoa na kumkabidhi mchungaji)

Mchungaji: Asante mtoto mzuri

Bianca: (anarudi kukaa alipo mama Raphael na Michael)

Mchungaji: (anampa Pete moja Liliana na nyingine Raphael)

(Maharusi wanapokea Pete hizo na kuzishikilia mkononi kusikiliza maelekezo ya mchungaji)

Mchungaji: (Kwa Raphael) nyanyua mkono (Kwa Liliana) haya fatisha maneno haya

Liliana: (anakaa tayari)

Mchungaji: mwenzangu pokea Pete hii

Liliana: (anafatisha)

(Zoezi la kuvalisha Pete linaendela na hatimaye linafika mwisho, watu wanashangilia sana na kulifurahia tukio lile takatifu)

Mchungaji: basi baada yahaya yote nawatangaza kuwa me na mue halali na alichokiunganisha Mungu mwanadamu asikitenganishe

(Nderemo, vifijo vinalipuka kanisani humo, watu wanawapongeza kwa hatua mpya maishani mwao, maharusi wanasaini vyeti vyao, picha zinapigwa kwa fujo, ngoma zinasikika kila kitu kinaonekana kuwa vizuri)

Liliana: (anajisemea moyoni) oh mama zangu natamani mngekuwepo muone furaha yangu leo

(Kwenye umati wa watu anaonekana mama yake mzazi Liliana pamoja na Bianca)

Liliana: (anatabasamu anapoona) kumbe mpo nawapenda Sana asanteni Kwa kuwepo hapa furaha yangu imekamilika

Mizimu: (inatabasamu kisha inatoweka)

Liliana: (anaendelea kufurahia pamoja na mume na ndugu, jamaa na marafiki)

Raphael: finally baby we are happy (anambeba mkewe Kwa upendo)

Post a Comment

1 Comments