MUNGU MKUU 18


 

SCENE 18: -

(Asubuhi ya siku ya pili yake Miriam anajiandaa kuondoka nyumbani)

Miriam :( anaonekana ana haraka Sana)

Ariana :( amekaa mezani anapata kifungua kinywa) upo busy Sana ndugu yangu siku hizi sikuelewi

Miriam :( anasimama na kumsikiliza)

Ariana: upo Kama kuna shemeji…

Miriam :( anacheka kidogo) hapana dada shikamoo

Ariana: marahaba… (Anapaka siagi kwenye mkate kwa kutumia kisu kidogo) kama una shemeji niambie jua mimi ni dada yako kwahiyo mambo mengi ni mimi ndo natakiwa kujua wewe ni mdada umeshaakuwa kwahiyo kuwa katika mahusiano ni jambo la kawaida

Miriam: najua dada ila bado sijapata boyfriend…

Ariana: usinitanie bwana…ulivyo mzuri tena mwenye bahati unakosa mwanaume?

Miriam: kabisa dada

Ariana:na yule aliyekuleta jana?

Miriam:ni boyfriend wa Vanessa yule

Ariana: kweli ee

Miriam: yes dada…

Ariana: nina shida…unajua Miriam

Miriam: shida gani dada, please talk to me

Ariana: Jeremy

Miriam:(anashtuka kidogo)

Ariana:(anamuangalia) Jeremy ameniandikia meseji amesema kuwa anaomba tusitishe uchumba wetu kwamba hataki kabisa mahusiano na mimi

Miriam:(anaguna) mama na baba wanajua?

Ariana: hapana hawajui nataka nimbembeleze Jeremy ili aendelee na mipango ya harusi

Miriam:(anaguna) mbona mtihani

Ariana: sio mdogo mdogo wangu, ni mtihani tena mkubwa sana

Miriam: mpigie simu uombe uongee nae jamani

Ariana: hapokei simu zangu nampigia mpaka nimesajili namba mpya nampigia ila naona haisaidii chochote maana hapokei

Miriam: ukimuuliza shida nini anasemaje?

Ariana: ana mwanamke anayempenda Kwa dhati, yaani wanaume wana majanga jamani

Miriam :( anaguna) yaani mbona majanga?

Ariana: tuombeane tu shoga yangu…naomba tu na wewe uwe makini maana wanaume wana mambo mengi sana

Miriam: sawa dada…nimekuelewa

Ariana: sasa naomba unisaidie jambo Fulani...

Miriam: nitakusaidia Kwa lolote utakaloniomba, likiwa ndani ya uwezo wangu kweli kabisa nitakusaidia dada

Ariana: ongea na Jeremy mwambie Mimi nampenda sana tena sana natamani tufunge ndoa, tutimize malengo ya wazazi wetu...Niombee mdogo wangu ongea nae sawa ee

Miriam :( kimya kidogo huku anamuangalia Sana dada yake)

Ariana: nambie utanisaidia au?

Miriam: nitakusaidia dada…

Ariana: Asante Sana mama…. (Anaendelea kunywa chai)

Miriam:(anajisemea moyoni) ni lazima niache huu ujinga naoufanya Jeremy ni mchumba wa dada yangu na dada yangu anampenda sana…ni lazima niachane na Jeremy mara moja

Ariana: mbona huendi sasa maana ulikuwa unajifanya una haraka

Miriam :( anashtuka kutoka kwenye mawazo) unasema?

Ariana: nenda bwana utachelewa huko ulipokuwa unaenda

Miriam: sawa baadae basi

Ariana: haya poa ila na wewe nitambulishe shemeji

Miriam: sina mtu dada...nipo tu…

Ariana: haya bwana wewe jifanye unanificha, mtakuja kusema tu

Miriam :( anacheka kisha anatoka nje) Ni lazima niachane na Jeremy

(Gari la Jeremy linaegeshwa mbele ya Miriam)

Jeremy: mrembo wangu uko poa?

Miriam: Jeremy hutakiwi kuwepo hapa

Jeremy: nimebadili gari hawatajua kuwa ni mimi…twende nikupeleke chuoni halafu baadae naomba tutoke dinner

Miriam :( anashusha pumzi) Jeremy

Jeremy :( anamfungulia mlango) comeon panda kwenye gari twende basi

Miriam :( anapanda)

Jeremy :( anamuangalia) are you okay?

Miriam: no

Jeremy: what happened? Unaumwa? (Anamgusa kwenye paji la uso) mbona joto ni la kawaida?

Miriam: siumwi…Jeremy

Jeremy: ila?

Miriam: tuachane Jeremy

Jeremy:(anashtuka) what?

Miriam: umenisikia vyema Jeremy…wewe ni mchumba wa dada yangu na dada yangu amesema anakupenda na anataka umuoe

Jeremy: what are you talking about?

Miriam: hatuna sababu ya kuwa wapenzi kwanza mimi ni mtoto mdogo sana

Jeremy: lakini nakupenda sana ni wewe baby ndo nataka nikuoe (anafungua mlango) naenda kuwaambia wazazi wako kuwa nataka kukuoa wewe

Miriam: ukitaka kuniudhi fanya hivyo…nitajirusha ghorofani nijiue…

Jeremy :( anafunga mlango) embu twende sehemu baby tukaongee naona umepaniki sana

Miriam: hakuna cha kuongea mimi na wewe sijui unanielewa…dada yangu anaomba sana kuwa na wewe, wewe unadhani atafanyaje siku akijua kuwa mimi na wewe ni wapenzi, ataona usaliti na hatawahi kunisamehe, nakupenda Jeremy ila nampenda dada yangu Zaidi

Jeremy: then let us fight for this love my love,

Miriam: sina hizo nguvu Jeremy

Jeremy: unazikosaje hizo nguvu jamani? Ok hold on...Nakupenda Sana Miriam tulia tutatoka tu kwenye huu usiri na ninakuhakikishia kila kitu kitakuwa sawa

Miriam: no Jeremy...no…please Kama humtaki dada yangu ni bora ukapende mtu mwingine na sio mimi…mimi ni mdogo wa Ariana na kwa ugumu mkubwa nimeyatengeneza mahusiano yangu na yeye

Jeremy: tafadhali usijifunge…

Miriam: naachaje…please try to understand jamani tusijifikirie wenyewe…tufikirie na wengine jamani

Jeremy :( Analia) that is not fair Miriam

Miriam: iam so sorry ila dada yangu ndo kila kitu kwangu siwezi kumdanganya dada yangu…siwezi kumsaliti

Jeremy: sitaki kuwa na mtu yeyote Zaidi yako Miriam

Miriam: jaribu kuwa muelewa basi jamani Jeremy…

Jeremy: No siwezi kukuelewa Miriam…nakupenda Sana…you are the woman of my life honey ni wewe ndo nataka uwe mama wa familia yangu…sio Ariana...Nimeshakuambia nilikuwa naona nimekuwa na pia umri unaenda ndo nikawaambia baba na mama wanaifanyie mpango wa kutafuta mchumba sikujua kama ningekutana na wewe baby...

Miriam: tuondoke tutaongea mbele huko

(Jeremy anawasha gari kisha analiondoa mahali hapo)

Post a Comment

1 Comments